Mzee Mwanakijiji
Platinum Member
- Mar 10, 2006
- 33,478
- 39,996
Yafuatayo ni mambo ambayo yamekubaliwa kufanywa baada ya uongozi wa Mamlaka ya Bandari, Wizara ya Miundo Mbinu na Ikulu kukutana jana. Hebu tuyaangalie na tuamue ni yapi yalimhitaji Rais na yasingeweza kupendekezwa au kuamuliwa kufanya kwenye uongozi wa chini.
(a) Kuitaka Kampuni ya Kupakia na Kupakua Makontena (TICTS) katika Bandari ya Dar es Salaam kutekeleza wajibu wake ipasavyo kwa mujibu wa mkataba wake kwa kuongeza ufanisi na kuboresha kiwango chake cha utendaji kwa lengo la kupunguza mlundikano wa meli katika Bandari ya Dar es Salaam.
(b) Kuchukua hatua nyingine za kupunguza mlundikano wa mizigo katika Bandari ya Dar es Salaam kwa kuchukua mfululizo wa hatua ikiwa ni pamoja na:
(i) Kuhakikisha kuwa mizigo inaondolewa haraka kwa kadri inavyowezekana katika Bandari, kwa kutumia taratibu muhimu zilizopo, ikiwa ni pamoja na kontena kupigwa mnada baada ya kuwa zimekaa bandarini kwa siku 21 kwa mujibu wa sheria.
(ii) Ili kutekeleza jambo hilo la kuhakikisha kuwa mizigo inaondolewa Bandari haraka, TPA na TRA zimeagizwa kuhakikisha kuwa zinapiga mnada kiasi cha asilimia 30 ya makontena yaliyokaa zaidi ya siku 21 katika bandari hiyo, kama njia ya haraka ya kupunguza mlundikano wa mizigo katika Bandari hiyo.
(iii) Kuhakikisha kuwa kuanzia sasa kontena zote zinazopakuliwa kwenye meli, zinapelekwa moja kwa moja kwenye Vituo vya Kuhifadhi Kontena Nje ya Bandari (ICDs) na gharama za zoezi hilo zinakuwa sehemu ya kutoa mizigo katika Bandari hiyo.
(iv) Kuchukua hatua za kupunguza muda wa meli kusubiri pwani ya Bandari ya Dar es Salaam kwa kuhakikisha kuwa upakiaji na upakuaji mizigo unaharakishwa kwa TICTS kununua vifaa zaidi na pia kuhakikisha kuwa vifaa vya TPA vinatumika.
(v) Kuhakikisha kuwa maarifa yanatafutwa kuondoa magari yaliyoko Bandarini kwa sasa yakisubiri kuchukuliwa na wenyewe, ili kupatikane nafasi zaidi ndani ya eneo la Bandari hiyo kwa shughuli na mizigo mingine. Hili lifanyike kwa kutafuta eneo jingine nje ya Bandari kuhifadhi magari hayo.
(vi) Kuharakisha zoezi zima la kuondoa mizigo Bandarini kwa nyaraka muhimu za kufanikisha jambo hilo kujazwa na kupitishwa haraka iwezekanavyo na TRA.
(vii) Ili kufanikisha uharaka huo, TRA imeagizwa kuhakikisha kuwa sehemu ya kushughulikia nyaraka ya long-room inafanywa kuwa short-room kwa maofisa wa Mamlaka hayo kufanya kazi kwa saa 24, ikiwa ni pamoja na siku za Jumapili.
(viii) Kuongeza ushirikiano wa utendaji miongoni mwa taasisi mbalimbali zinazohusika na kuondoa mizigo katika Bandari ya Dar es Salaam, ili kuongeza ufanisi wa Bandari hiyo na kuiwezesha kupambana ipasavyo na ushindani kutoka kwa bandari nyingine katika eneo la Mashariki na Kusini mwa Afrika.
(ix) Kuchukua hatua za kuboresha ushindani wa Bandari ya Dar es Salaam kwa miaka ijayo, hasa baada ya ongezeko kubwa la mizigo litakalokuwa linapitia katika bandari hiyo baada ya Reli ya Kati kufanyiwa matengenezo makubwa ya kupanua geji yake.
Imetolewa na:
Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais,
Ikulu,
DAR ES SALAAM.
(a) Kuitaka Kampuni ya Kupakia na Kupakua Makontena (TICTS) katika Bandari ya Dar es Salaam kutekeleza wajibu wake ipasavyo kwa mujibu wa mkataba wake kwa kuongeza ufanisi na kuboresha kiwango chake cha utendaji kwa lengo la kupunguza mlundikano wa meli katika Bandari ya Dar es Salaam.
(b) Kuchukua hatua nyingine za kupunguza mlundikano wa mizigo katika Bandari ya Dar es Salaam kwa kuchukua mfululizo wa hatua ikiwa ni pamoja na:
(i) Kuhakikisha kuwa mizigo inaondolewa haraka kwa kadri inavyowezekana katika Bandari, kwa kutumia taratibu muhimu zilizopo, ikiwa ni pamoja na kontena kupigwa mnada baada ya kuwa zimekaa bandarini kwa siku 21 kwa mujibu wa sheria.
(ii) Ili kutekeleza jambo hilo la kuhakikisha kuwa mizigo inaondolewa Bandari haraka, TPA na TRA zimeagizwa kuhakikisha kuwa zinapiga mnada kiasi cha asilimia 30 ya makontena yaliyokaa zaidi ya siku 21 katika bandari hiyo, kama njia ya haraka ya kupunguza mlundikano wa mizigo katika Bandari hiyo.
(iii) Kuhakikisha kuwa kuanzia sasa kontena zote zinazopakuliwa kwenye meli, zinapelekwa moja kwa moja kwenye Vituo vya Kuhifadhi Kontena Nje ya Bandari (ICDs) na gharama za zoezi hilo zinakuwa sehemu ya kutoa mizigo katika Bandari hiyo.
(iv) Kuchukua hatua za kupunguza muda wa meli kusubiri pwani ya Bandari ya Dar es Salaam kwa kuhakikisha kuwa upakiaji na upakuaji mizigo unaharakishwa kwa TICTS kununua vifaa zaidi na pia kuhakikisha kuwa vifaa vya TPA vinatumika.
(v) Kuhakikisha kuwa maarifa yanatafutwa kuondoa magari yaliyoko Bandarini kwa sasa yakisubiri kuchukuliwa na wenyewe, ili kupatikane nafasi zaidi ndani ya eneo la Bandari hiyo kwa shughuli na mizigo mingine. Hili lifanyike kwa kutafuta eneo jingine nje ya Bandari kuhifadhi magari hayo.
(vi) Kuharakisha zoezi zima la kuondoa mizigo Bandarini kwa nyaraka muhimu za kufanikisha jambo hilo kujazwa na kupitishwa haraka iwezekanavyo na TRA.
(vii) Ili kufanikisha uharaka huo, TRA imeagizwa kuhakikisha kuwa sehemu ya kushughulikia nyaraka ya long-room inafanywa kuwa short-room kwa maofisa wa Mamlaka hayo kufanya kazi kwa saa 24, ikiwa ni pamoja na siku za Jumapili.
(viii) Kuongeza ushirikiano wa utendaji miongoni mwa taasisi mbalimbali zinazohusika na kuondoa mizigo katika Bandari ya Dar es Salaam, ili kuongeza ufanisi wa Bandari hiyo na kuiwezesha kupambana ipasavyo na ushindani kutoka kwa bandari nyingine katika eneo la Mashariki na Kusini mwa Afrika.
(ix) Kuchukua hatua za kuboresha ushindani wa Bandari ya Dar es Salaam kwa miaka ijayo, hasa baada ya ongezeko kubwa la mizigo litakalokuwa linapitia katika bandari hiyo baada ya Reli ya Kati kufanyiwa matengenezo makubwa ya kupanua geji yake.
Imetolewa na:
Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais,
Ikulu,
DAR ES SALAAM.