IGUDUNG'WA
JF-Expert Member
- Oct 22, 2011
- 2,071
- 1,314
nimeangalia taarifa ya habari mlimanitv wameyalipua magamba kwa kuonesha magari yaliyokodiwa kupeleka watu jangwani
hakika ccm kwisha habari yake
hakika ccm kwisha habari yake
Leo ndani ya jangwani mambo yalikuwa mabaya kwa ccm baada ya waziri magufuli kutangaza kuwa wanaotaka kurudisha kadi na kujiunga upya wajitokeze, watu wachache sana na hawafiki hata 100 na hakuna hata mmoja aliye enda kujiunga upya, baada ya kuona hali ni tete ndipo nape akalopoka kuwa hawapokei wanachama upya mpaka baada ya uchaguzi ndani ya CCM.
Nilikuwa napita maeneo ya kwa azizi Ali nikaona kundi la wakina mama wanatembea wanadai 5000 zimewatokea puani kwani Yale mafuso yaliowapeleka yameingia mitini
Utakuwa unatania, nani awaombee! kwanini wasitubu na kuomba wao wenyewe?Huo ni mkutano wa kisiasa mambo yakiwa mahakamani hutakiwi kuyaongelea hadhalani. Acheni mambo ya ushabiki ambao hauna tija. Kama kitu kizuri lazima usifie. Kuna sometime Mungu anatupa laana kutokana na kuongea mambo yasiyo na maana. Kwanini tusikae na tuwaombee viongozi wetu?
Hizi ndizo kauli za wasichana wanaobishana sokoni kuhusu mvulana yupi ni mzuri. Na ccm imeishaujua ujinga wa watanzania na ndio maana inawatongoza na inapowapata inawatumia ipasavyo.
Ccm inawahadaa watu kama wewe mithili ya mvulana anayemtafuta msichana!!! Inawatongoza kwa vitisheti vya njano na vikofia vya kijani; Inawapa lifti; inawalisha wali kuku; inawatumbuiza kwa taarabu; inawaahidi maisha bora na kisha inawahonga elfu tano!! Kwa ulaini wananchi wanakubali kufanya mapenzi na ccm. Wanapewa mimba, wanazaa ufukara na kisha wanatelekezwa kwa maisha duni!
Nionavyo mimi: Watanzania wakiteseka na mazingaombwe ya ugumu wa maisha ni sawa tu!! Ni haki yao!! Waendelee tu kutaabika kwa kuwa dhiki, mahangaiko na ufukara wanavitaka wenyewe!!
Ni kweli mkuu ndio nafika nyumbani nasubiri tamko la UAMSHO kwani Waislamu wametukanwa bila sababu yeyote makanisa wachome magamba lawama ziende UAMSHO sisi CDM tunawaheshimu na kura zao ni muhimu kwetu lakini nyinyi mnawaita majambazi mtakoma mwaka huuLeo utalala hoi mkuu.
nilihudhulia mkutano wa chadema jangwani,nilicho gundua ni kwamba chadema ni wazuri wa kulalamika matatizo yaliyopo ila hawawezi kusema wakichukua nchi watatatua vipi matatizo hayo! one major weakness of chadema wazuri wa kulaumu but they are poor to walk the talk hata majimbo waliyo chukua kama iringa mjini,mwanza,ubungo,msoma,mbeya bado wabunge wao wamekaa mkao wa kulalamika utadhani sio wabunge! leo jangwani mkutano wa ccm nitahudhulia nijue udhaifu wa ccm na uzuri wao!
kwa unafiki aliouonyesha kwenye swala la richmond hakika huyu si mtetea haki za walala hoi ikumbukwe leo watanzania tunalipa mabilioni kwasababu ya unafiki wake...sema anauafadhali ukimlinganisha na walioko ndani ya ccm
yaani pale
- 25% wako kikazi, kwamba ni viongozi chama katika nafasi mbalimbali au watu wa usalama (kasoro polisi, hawa wamenawiri sana, kweli wanakula mema ya nchi)
- 70% wameletwa na mabasi tena hawa walikua wanashuka unajiuliza mara mbilimbili kama wanaelewa hata nchi inavoendeshwa wengi wana afya mbovu kuonesha hali yao ilivvyo ngumu, wamekonda na wako dhoofu sana, sijajua kitu gani kiliwafanya waje, labda ni watu walikusanywa wakapewa pesa, wengi walikua na tshirt za ccm mpya ila ni za wakati wa uchaguzi wa 2010, inaelekea kuna stock ilibaki ndio wametumia
- 5% ndio kama sie tulioenda kuangalia hawa wenzetu wanakipi kipya
Lowassa mwamba wa kaskazini hakuwepo ccm kwisha!!!!!!