Mwenye update za Zanzibar jamani maana nasikia hali sio shwari huko
picha zi wapi?Hadi sasa ni machafuko matupu, mawakala wa CUF wametolewa kwenye vyumba vya kupiga kura kwa makosa haya;
(a). Wamegundua baadhi ya masanduku yamejazwa kura ambazo zimeshatatiwa tiki kwa mbunge wa CCM.
(b). Wamegundua kuwa kuna watu hawamo ndani ya daftari la kupiga kura ila wamekuja kupiga kura na walipo pinga ndipo POLISI walivyoamua kuwatoa.
(c) Chumba numba 6 imegundilika kwamba masunduku yote yamejazwa kura.
(d) Mazombi wameanza kupiga watu maeneo ya Fuoni kituo cha Kibondeni
(e) Katika kituo hicho cha Fuoni mabasi yamekua yakisomba watu na kuwaleta kupiga kura. Watu hao si wakazi wa jimbo la Dimani. Picha hapo chini inaonesha moja ya mabasi yanayotumika kusomba watu na kuwapeleka vituoni kupiga kura.
Chanzo; # Hababi_CUF
zawadi yake ipo!Jecha kashafanya yake huko Zanzibar
Wakati mwingine zile hatua wanazochukua watu wanaoonewa na kunyanyaswa kwa kusababisha damu ina mwagika kumbe sio dhambi. Kenya ilikuwa hivyo lakini sasa wanaheshimiana hakuna mjinga awezaye kufanya mambo ya hovyo namna hiyo kabla hawajamkamua tumbo!Haya niliyategemea sana.Hivyo Siwezi kushangazwa nayo ila NEC ndiyo ya kulaumiwa na Wapinzani Wenyewe hawachulii issue ya Uchaguzi kama sensitive issue.