Wote tuungane tuseme "hatudanganyiki"

Oct 19, 2010
29
2
Wapendwa nawaandikia ili msidanganyike. Sulaiman Mohammed Yahya Al Adawi hajawahi kuwa na si mmiliki wa Dowans. Ujio wake ni simema iliyopangwa kwa ustadi mkubwa ili kutuhadaa na hatimaye tuingie mkataba mwingine fake wa kununua umeme wa Dowans hata baada ya kuwalipa fidia. WaTZ tuweke msimamo - Mitambo ya Dowans NO. Ni heri tukakaa gizani kuliko kuwa na umeme kwa kuwanufaisha mafisadi wachache. Tunaweza kufanya yafuatayo kama tuna nia njema na mustakabali wa Taifa letu - Aidha tuitaifishe mitambo ya Dowans chini ya sheria ya uhujumu uchumi au Mmiliki apewe muda wa kuiondoa nchini aipeleke anakakotaka. Zingatia - Mmiliki halisi wa Dowans anafahamu bei ya kila kiongozi wa nchi hii na haishangazi kuona baadhi ya wabunge wameanza kuwa na msimamo laini dhidi ya Dowans. Wakati umefika wote tuseme HATUDANGANYIKI
 
Back
Top Bottom