William Ngeleja arejesha fedha za mgao wa Escrow kiasi cha Tsh Milioni 40.4

Ha ha ha ha haaaa

Kama wamezitumia na hata hawana bakshishi lolote hata pakutoa zao wenyewe!? Kumbuka alizopewa wa leo ilikuwa kidogo sana, ni wale walipewa kama vile wapewe tu wabanane pamoja.
 
faida ya kutoka Toa msaada. heri uwe bairi hata ikilipuka unakuwa kivyako au unajitetea kivyako.
 
Kwanza aseme alipewa kwa madhumuni gani?Kama no msaada yeye no yatima au mbunge anayeishi mazingira magumu?
 
Habari wanaJF,

Waziri wa zamani wa Nishati na Madini na Mbunge wa Jimbo la Sengerema, William Ngeleja amerejesha rasmi Serikalini fedha alizozipokea kutoka kwa James Rugemalira mnamo tarehe 12/2/2014 katika mgao wa Escrow ambazo ni kiasi cha Shilingi Milioni 40.4 ili kukwepa kuendelea kuandamwa na kashfa hiyo.


Ngeleja amesema kuwa ''Nimeamua kurejesha fedha hizi hata kama aliyenipa msaada bado ni mtuhumiwa tu, kwa sababu sitaki kuwa sehemu ya kashfa/tuhuma hizo'' Ngeleja.

'Leo nina zaidi ya miaka 12 nikiwa kiongozi wa Umma lakini sijawahi kukumbwa na kashfa ya rushwa au ufisadi.

Kwa vile sasa imedhihirika kwamba aliyenipa msaada huu anatuhumiwa kwenye kashfa ya akaunti ya ESCROW nimeamua kuchukua hatua.

Kupokea msaada ni jambo la kawaida, ila ikibainika kuna harufu ya uchafu hata kama haujathibitishwa na vyombo husika ni vyema kujiepusha nao.

Nimerudisha fedha hizi ili kulinda maslahi ya nchi yangu na heshima ya chama changu, Serikali, wanasengerema, familia yangu na heshima yangu.

Nimepima na kutafakari, na hatimaye nimeamua, kwa hiari yangu mwenyewe, kurejesha kiasi cha Milioni 40.4 serikalini.


hahahaahah,sasa unarudisha tra kwani ndiyo waliokupa. Angetumia uungwana sana kama angezirudisha kwa aliyemlipa. Hata accounting procedures hazipo hivyo. Hii haimfanyi huyu mh. kuwa salama.
 
Izo pesa zilitakiwa zirudi na Riba ya asilimia 13.50% kwa mwaka. Maana kama zingekuwa katika mzunguko zingeendelea kuzalisha katika Taifa
 
JF Kwenu,
Nimemsikiliza Waziri wa zamani wa Nishati na Madini na mbunge wa Msalala Mh. Ngeleja akiwa anajulisha uma kuwa anarejesha Sh. 40.4 milioni alizopewa kama zawadi na Don Rugemalira. Alikuwa na karatasi mkononi, ushahidi kuwa amefanya transfer ya fedha anazorudisha.

Nimejiuliza, toka mwaka 2014 ilipotokea Escrow Scandal mpaka sasa ni miaka takriban mitatu, kwa nini amekaa kimya muda wote huo kama alijua amepokea fedha za wizi?
Amekuwa mjanja kutamka kuwa Don Rugemalira ni mtuhumiwa tu, bado mahakama haijathibitisha kuwa ana hatia.Pamoja na hayo, kwa nini ameamua kurudisha pesa ikiwa mtoaji bado hajatiwa hatiani?

Sheria ya Maadili ya Viongozi wa Uma inamtaka mtumishi wa uma anayepokea kama zawadi kiasi cha fedha kinachozidi Tsh. 50,000 kutoa taarifa kwa Kamati. Ameshafanya hivyo?

Amelipa fedha serikalini, ana uhakika hiyo fedha yote ni ya serikali?Kwa nini hakurudisha fedha kwa aliyempa?

Hoja nyingine ya msingi ni Je, anarudisha fedha kwa kuwa ana dhamira safi au kuna ahadi ya Uwaziri ambayo kuipata sharti 'kuokoka' hadharani?
Naomba tujadili.


Sent from my TECNO-W3LTE using JamiiForums mobile app
 
Back
Top Bottom