pembankwetu
Senior Member
- Dec 30, 2012
- 133
- 62
Hapa ndio umenena kuanzia leo nakukubali wewe ni embe
5: NIMEKUTANA NA SHEIKH PONDA
Milima huwa haikutani lakini binadamu wanakutana. Ndivyo sakata la ugaidi lilivyonifikisha gereza la Segerea na huko nikajikuta nawekwa selo moja na mjukuu wangu Issa Ponda mtoto kutoka Kigoma. Issa Ponda ni kiumbe wa mwenyezi Mungu wa aina ya pekee. Kwa nchi za wenzetu zilizoendelea mtu mithiri ya Ponda si mtu wa kuchukulia mzaa kama ninaouona ukichezwa hapa kwetu. Ni mtu ambaye fikra zake, ubunifu alionao kichwani na katika vitendo, hulka zake, nasaha zake, ushawishi wake, ujengaji hoja zake, uchaji wa Mungu wake, uswalihina wake na vingine vingi ni watu wachache sana unaoweza kukutana nao wakiwa navyo vyote kwa mpigo.
Ponda tofauti na namna mfumo unavyomchukulia, ni mtu ambaye angetumika vyema kwa kusikilizwa sehemu kubwa ya mawazo yake na yakafanyiwa kazi ipasavyo, nina uhakika mambo mengi tunayoyaona yana mitafaruku ya kidini yasingelikuwepo.
Tatizo wakubwa wanamuangalia kwa taswira ya upande mmoja ya kumuona mkorofi, mchochezi. Sijui na ndio maana nauliza, hivi ni mamlaka gani ya juu na yenye kauli ndani ya nchi hii imewahi kukaa na Ponda kwa karibu katika misingi ya kuheshimiana kwa dhati na kusikilizana ili kujua ana mawazo na mitizamo gani kwa masuala mbalimbali yaliyolalamikiwa na baadhi ya waislamu walio wengi?
Nimeishi naye zaidi ya siku 60 selo moja kwa masaa 24 karibu kila siku na masaa mengi tukiwa wawili tu, mimi na yeye. Ni mdadisi wa kupenda kujua, na ukisha mwelewesha ni mwepesi wa kuelewa na kujenga fikra mpya. Hivyohivyo siyo mchoyo wa kuyabania maarifa aliyonayo na elimu kubwa ya kidini aliyobahatika kuipata.
Alinielewesha kuwa kwenye dini ya kiislamu mtu anapokuwa amefikia kiwango cha kuitwa U-Ustadhi kwa lugha ya haraka inayoeleweka na wengi ni sawa na U-profesa.Hakika Sheikh Ponda ni profesa.
Nilipata fursa ya kujadiliana naye pia mambo ya msingi yanayolikabili hivi sasa Taifa letu. Moja wapo ni nguvu nyingi zisizo na sababu zinazotumiwa na polisi kushughulika na watu kama sisi ambao hata rungu hatuna. Nguvu kubwa inayotumika ya kumpeleka Ponda au Lwakatare mahakamani ili kesi itajwe tu na kurudi Segerea kulala ni sawa na kumlipa daktari wa muhimbili mishahara mizuri ya miezi miwili. Magari nane na mapikipiki kujazwa mafuta,vingora barabarani,askari polisi zaidi ya hamsini kuvunja shughuli nyinginezo kwa siku nzima, barabara kufungwa na mengine kuzuiwa wakati wa kupita n.k Mikwara yote hiyo ya nini?
Mfungwa mmoja aliyesoma kwa kiwango fulani alipoletwa kulala kwenye selo yetu na kuikuta mada hiyo, alichangia hivi, kawaida ya mtu yeyote anayelazimisha aonekane mbele ya wakubwa zake kwamba anafanya kazi ni lazima atengeneze mazingira yanayomfanya aonekane kweli anafanya kazi. Kisha kasema hivi nyie waheshimiwa ili wale waliowafungulia tuhuma za ugaidi na uchochezi lazima watoe taswira ya nje kwa umma kuonesha kuwa ninyi ni watu hatari sana na mkipewa upenyo wowote mnaweza kusababisha maafa makubwa sana wakati wowote kwa taifa. Kwa ufupi wanataka umma uwahukumu kinadharia kwamba mnahusika na tuhuma mlizoshtakiwa nazo hata kama mahakama haijazipitia tuhuma zenyewe kuona zina uzito gani.
Nilimuelewa vizuri sana na kukubaliana na huyo mfungwa maana vyombo vyetu hivi vya dola wakati mwingine vinapenda kutumia nguvu nyingi sana katika jambo dogo sana kwa sababu tu za kuridhishana na makundi fulani au kulinda nafasi zao za kazi ambazo hawazimudu.
Jambo jingine lililoangukia katika mijadala yetu ni hii migogoro ya makundi ya kijamii na hata mauaji na maumizano yanayojitokeza mara kwa mara. Sheikh Ponda alitoa changamoto moja muhimu ambayo naona ina mashiko sana. Alisema hivi; huko uswazi (mitaani wanakoishi watu wengi kwa kubanana) ambako nyumba moja wanapanga na kuishi zaidi ya watu hamsini, mchanganyiko wa waislamu kwa wakristo, mbona hakuna ugomvi? Mbona akina mama humo ndani waislamu kwa wakristo wanaachiana watoto kwenda sokoni? Mbona wanaazimana vijiko na masufuria? Mbona wanapeana mboga bila kuulizana? Ponda akatumbukiza na utani pia kuwa mbona humu selo ukileta chakula alichopika mama Frank siulizi na wala wewe chakula anachoniletea mama Mariam naona unabugia tu bila maswali yoyote?
Na mimi nikamwambia mbona ukiamka saa tisa usiku ukaanza swala zako za sunna mpaka alfajiri wakati wa Azanna na kisha swala zote tano za faradhi za siku nzima na lakhai zake mbilimbili humu humu ndani ya selo havijaingiliana na ibada zangu za Tumwabudu Mungu wetu? Selo yetu ndio msikiti wetu na ndilo kanisa letu. Haya mambo chanzo na chimbuko lake ni nini? Hayawezi kuwa yanatengenezwa na kundi maalum la watu kwa malengo maalum?
Swali hili la mwisho likanikumbusha somo moja tulilowahi kufundishwa kipindi fulani nilipokwenda Ujerumani kwa mafunzo ya Strategic Planning. Katika kipengele kimojawapo cha mafunzo hayo nakumbuka kuna kitu mwalimu alikiita Power Winning and Maintaining Strategy, kwa tafsiri nyepesi mkakati wa kuupata utawala na kuulinda.
Katika mkakati huo nakumbuka alitwambia, kuna wakati watawala fulani wanapoelemewa na mambo au jambo wakakosa majibu mbele ya watawaliwa wanaotaka kujua kulikoni ili kuzima mambo hayo aidha ni kutumia nguvu na fursa zilizopo kumshughulikia kinara mmoja anayeonekana kimbelembele kuhoji.
Mkisha mziba mdomo kwa njia zozote zinazowezekana walio nyuma yake wataufyata tu! Njia nyingine ni kuibua au kufanya jambo fulani kubwa bila kujulikana linaloweza kusaidia kuwahamisha watu kifikra toka jambo jingine lililopo ambalo ni hatarishi zaidi kiutawala.
Njia nyingine ni ile iliyotumika tangu ukoloni ya watawanye uwatawale (Divide and rule policy).
Ukiwapa nafasi au fursa watawaliwa wakakaa, wakapanga wakaelewana na nyie mpompo tu mkiwaangalia, jua siku watakapozua ajenda ya kushughulika na wewe, ujue umekwenda. Dawa ni kuwafanya siku zote wasielewane kwa kuwagonganisha vichwa wenyewe kwa wenyewe tena kwa mambo madogo yasiyo hitaji gharama kubwa na nguvu nyingi. Tulijadiliana sana na kwa urefu na Sheikh Ponda juu ya mambo haya lakini hatukupata jibu la mwisho na kwa bahati mbaya au nzuri Mungu akawa amezisikia dua zake na sala zake za masaa zaidi ya 18 kila siku akawa amechomolewa Segerea na kuniachia Sello No. 3. Najua Mungu atatukutanisha tena Inshallah! Ila, isiwe tena Segerea au Keko ili tuhitimishe mada hiyo.
Siku moja kabla ya kusomewa hukumu yake na Hakimu Nongwa (9/5/2013) tulijadili sana hukumu yake kwamba inaweza kuwa ya mwelekeo gani na maamuzi yapi. Panga pangua ilishindikana kueleweka mambo yatakuwaje kutokana na mazingira yaliyokuwa yakiizunguka kesi yenyewe. Mawakili wake walikuwa wameifanya kazi yao vyema bila kubakiza punje ya shaka. Lililokuwa likimpa faraja zaidi na kesi yake ni kusikia kwamba huyo hakimu ni mama mlokole, ameokoka. Hiyo ilikua ikimpa moyo sana kwamba atahukumiwa na kupewa haki yake sawa na lile lililozungumzwa na kuwasilishwa mbele ya hakimu Nongwa.
Nilimuuliza endapo hukumu itamuweka katika mazingira ya kumkata makali yake ya kazi ya utetezi anayoifanya na wakati huohuo upande wa pili wa system ukamtaka aanze kutoa Ushirikiano atafanyaje? Sheikh Ponda aliniambia kuwa haki huwa hainunuliwi wala kuombwa bali hudaiwa. Alisema atakuwa tayari kutoa ushirikiano kwa yeyote yule anayezungumzia utoaji na upatakanaji haki.Na akasema mdomo na nafsi vilivyodhamiria kuzungumzia na kuitafuta haki huwa havifungiki kwani vikifungika hata hiyo amani haiwezi kuwepo.
Nikiwa ndani ya selo nilimsikia Sheikh Ponda akimwaga mistari yake redioni baada ya kuhukumiwa. Kwa mara nyingine nikazidi kumuaminia Sheikh Ponda kwamba ni mmojawapo ya watu wachache tulio nao hivi sasa nchini wanaoweza kutembea na kuishi ndani ya maneno yao.
Lipo jambo moja muhimu ambalo tulikubaliana na Sheikh Ponda tulijadili na kulifanyia kazi kwa nia ya kuwanusuru watu wanaosota jela bila sababu endapo tungeliachiwa na kuwa huru uraiani. Namtafuta kwenye simu hayuko reachable. Nikishampata tukashauriana na likaonekana linatekelezeka, nitalitoa hadharani.
6: USHAURI WANGU MDOGO KWA VIONGOZI WETU WA DINI.
Mimi ni mtu mdogo sana na muumini wa kawaida ndani ya dhehebu la KKKT. Lakini natambua kanisa ni waumini na wajibu mkubwa wa kila muumini ni kuhakikisha anatimiza wajibu wake kama kanisa la Mungu linavyoelekezwa kupitia maandiko matakatifu ya Biblia. Wajibu mmojawapo sisi kama waumini ni kuonyana ( Ebr. 10:24 25).
Nawaombeni viongozi wetu wa dini zote wakristo kwa waislamu mtimize wajibu wenu mliokabidhiwa na Mungu, Imeandikwa kwa dini zote kwamba kila mmoja bila kujali wadhifa wake atahukumiwa sawa na matendo yake. Nawaomba simamieni na kuuzungumza ukweli(hata kama ni mchungu) mbele ya watawala na hata watawala watarajiwa.Ninyi mmepewa mamlaka na Mungu ya kuonya, kukemea, kuelekeza na kubariki na ndio maana watawala wote wanawaogopa na kuwaheshimu. Wengine huenda ninyi bila ya kuwatambua hutafuta njia za kujikomba kwenu ili wakipate wanachokitafuta.Yasemeni wazi na kuyahoji hata yale machache yanayoonekana au kusikika pasipo kificho.
Muulizeni Mheshimiwa Rais huyo waziri wake anayezungumzwa kila siku kwamba mchana kweupe alisema anao maadui zake wawili ambao ni waandishi wa habari na angewashughulikia, Rais analisemaje hilo? Maadam ni ninyi, nina uhakika Mheshimiwa Rais atajibu na atachukua hatua stahiki.
Binafsi nawaombeni kwa heshima na taadhima muache kuwa vuguvugu (si moto si baridi-Ufunuo wa Yohana 3:15-16) Baadhi yenu acheni kuogopa vivuli vyenu kwa maana ya kuhofia kunyimwa upendeleo au misaada ya serikali (i.e misamaha ya kodi) na baadhi kuutumia mwanya huo vibaya. Kama maandiko yanavyosema JIKANENI WENYEWE.
Lazima mtambue hawa jamaa wakati mwingine huenda wanaitumia fursa hiyo kama chambo cha kuwanasia pindi wanapokua wana taarifa zenu zote za fursa ya misamaha iliyotumika vibaya. Mnapaswa kushuhudiwa mema na watu walio nje (1 Tim 3:2-9)
Binafsi nawaomba msiwalee wala kuwabeba wale wote wenye dhamira chafu na nia mbaya ya kutaka kuyatumia madhehebu yenu kukidhi matakwa binafsi kwani wanachafua taswira zenu nzuri za madhehebu yenu mbele ya waumini wenu na umma kwa ujumla.
Lakini zaidi ya yote ni imani yangu mimi binafsi kwamba madhehebu yenu ni makubwa na yana mtandao mkubwa na wenye nguvu ndani na hata nje ya nchi.Kama inawezekana tumieni mtandao wenu kuisaidia serikali ambayo vyombo vyake vinaelekea kushindwa kuwabaini wahalifu wachache wanaoelekea kuchafua na kuivuruga amani tuliyoizoea ndani ya nchi yetu. Kwa bahati nzuri nimesoma na kusikia kwenye vyombo vya habari kwamba IGP Mwema amezishauri taasisi za kidini kuanzisha ulinzi shirikishi ndani ya misikiti na makanisa. Kama mambo serikali ya CCM imeyafikisha hapo, tumieni fursa hiyo kuziomba taasisi makini mnazozifikia nje na ndani ya nchi.
"
5: NIMEKUTANA NA SHEIKH PONDA
Milima huwa haikutani lakini binadamu wanakutana. Ndivyo sakata la ugaidi lilivyonifikisha gereza la Segerea na huko nikajikuta nawekwa selo moja na mjukuu wangu Issa Ponda mtoto kutoka Kigoma. Issa Ponda ni kiumbe wa mwenyezi Mungu wa aina ya pekee. Kwa nchi za wenzetu zilizoendelea mtu mithiri ya Ponda si mtu wa kuchukulia mzaa kama ninaouona ukichezwa hapa kwetu. Ni mtu ambaye fikra zake, ubunifu alionao kichwani na katika vitendo, hulka zake, nasaha zake, ushawishi wake, ujengaji hoja zake, uchaji wa Mungu wake, uswalihina wake na vingine vingi ni watu wachache sana unaoweza kukutana nao wakiwa navyo vyote kwa mpigo.
Ponda tofauti na namna mfumo unavyomchukulia, ni mtu ambaye angetumika vyema kwa kusikilizwa sehemu kubwa ya mawazo yake na yakafanyiwa kazi ipasavyo, nina uhakika mambo mengi tunayoyaona yana mitafaruku ya kidini yasingelikuwepo.
Tatizo wakubwa wanamuangalia kwa taswira ya upande mmoja ya kumuona mkorofi, mchochezi. Sijui na ndio maana nauliza, hivi ni mamlaka gani ya juu na yenye kauli ndani ya nchi hii imewahi kukaa na Ponda kwa karibu katika misingi ya kuheshimiana kwa dhati na kusikilizana ili kujua ana mawazo na mitizamo gani kwa masuala mbalimbali yaliyolalamikiwa na baadhi ya waislamu walio wengi?
Nimeishi naye zaidi ya siku 60 selo moja kwa masaa 24 karibu kila siku na masaa mengi tukiwa wawili tu, mimi na yeye. Ni mdadisi wa kupenda kujua, na ukisha mwelewesha ni mwepesi wa kuelewa na kujenga fikra mpya. Hivyohivyo siyo mchoyo wa kuyabania maarifa aliyonayo na elimu kubwa ya kidini aliyobahatika kuipata.
Alinielewesha kuwa kwenye dini ya kiislamu mtu anapokuwa amefikia kiwango cha kuitwa U-Ustadhi kwa lugha ya haraka inayoeleweka na wengi ni sawa na U-profesa.Hakika Sheikh Ponda ni profesa.
Nilipata fursa ya kujadiliana naye pia mambo ya msingi yanayolikabili hivi sasa Taifa letu. Moja wapo ni nguvu nyingi zisizo na sababu zinazotumiwa na polisi kushughulika na watu kama sisi ambao hata rungu hatuna. Nguvu kubwa inayotumika ya kumpeleka Ponda au Lwakatare mahakamani ili kesi itajwe tu na kurudi Segerea kulala ni sawa na kumlipa daktari wa muhimbili mishahara mizuri ya miezi miwili. Magari nane na mapikipiki kujazwa mafuta,vingora barabarani,askari polisi zaidi ya hamsini kuvunja shughuli nyinginezo kwa siku nzima, barabara kufungwa na mengine kuzuiwa wakati wa kupita n.k Mikwara yote hiyo ya nini?
Mfungwa mmoja aliyesoma kwa kiwango fulani alipoletwa kulala kwenye selo yetu na kuikuta mada hiyo, alichangia hivi, kawaida ya mtu yeyote anayelazimisha aonekane mbele ya wakubwa zake kwamba anafanya kazi ni lazima atengeneze mazingira yanayomfanya aonekane kweli anafanya kazi. Kisha kasema hivi nyie waheshimiwa ili wale waliowafungulia tuhuma za ugaidi na uchochezi lazima watoe taswira ya nje kwa umma kuonesha kuwa ninyi ni watu hatari sana na mkipewa upenyo wowote mnaweza kusababisha maafa makubwa sana wakati wowote kwa taifa. Kwa ufupi wanataka umma uwahukumu kinadharia kwamba mnahusika na tuhuma mlizoshtakiwa nazo hata kama mahakama haijazipitia tuhuma zenyewe kuona zina uzito gani.
Nilimuelewa vizuri sana na kukubaliana na huyo mfungwa maana vyombo vyetu hivi vya dola wakati mwingine vinapenda kutumia nguvu nyingi sana katika jambo dogo sana kwa sababu tu za kuridhishana na makundi fulani au kulinda nafasi zao za kazi ambazo hawazimudu.
Jambo jingine lililoangukia katika mijadala yetu ni hii migogoro ya makundi ya kijamii na hata mauaji na maumizano yanayojitokeza mara kwa mara. Sheikh Ponda alitoa changamoto moja muhimu ambayo naona ina mashiko sana. Alisema hivi; huko uswazi (mitaani wanakoishi watu wengi kwa kubanana) ambako nyumba moja wanapanga na kuishi zaidi ya watu hamsini, mchanganyiko wa waislamu kwa wakristo, mbona hakuna ugomvi? Mbona akina mama humo ndani waislamu kwa wakristo wanaachiana watoto kwenda sokoni? Mbona wanaazimana vijiko na masufuria? Mbona wanapeana mboga bila kuulizana? Ponda akatumbukiza na utani pia kuwa mbona humu selo ukileta chakula alichopika mama Frank siulizi na wala wewe chakula anachoniletea mama Mariam naona unabugia tu bila maswali yoyote?
Na mimi nikamwambia mbona ukiamka saa tisa usiku ukaanza swala zako za sunna mpaka alfajiri wakati wa Azanna na kisha swala zote tano za faradhi za siku nzima na lakhai zake mbilimbili humu humu ndani ya selo havijaingiliana na ibada zangu za Tumwabudu Mungu wetu? Selo yetu ndio msikiti wetu na ndilo kanisa letu. Haya mambo chanzo na chimbuko lake ni nini? Hayawezi kuwa yanatengenezwa na kundi maalum la watu kwa malengo maalum?
Swali hili la mwisho likanikumbusha somo moja tulilowahi kufundishwa kipindi fulani nilipokwenda Ujerumani kwa mafunzo ya Strategic Planning. Katika kipengele kimojawapo cha mafunzo hayo nakumbuka kuna kitu mwalimu alikiita Power Winning and Maintaining Strategy, kwa tafsiri nyepesi mkakati wa kuupata utawala na kuulinda.
Katika mkakati huo nakumbuka alitwambia, kuna wakati watawala fulani wanapoelemewa na mambo au jambo wakakosa majibu mbele ya watawaliwa wanaotaka kujua kulikoni ili kuzima mambo hayo aidha ni kutumia nguvu na fursa zilizopo kumshughulikia kinara mmoja anayeonekana kimbelembele kuhoji.
Mkisha mziba mdomo kwa njia zozote zinazowezekana walio nyuma yake wataufyata tu! Njia nyingine ni kuibua au kufanya jambo fulani kubwa bila kujulikana linaloweza kusaidia kuwahamisha watu kifikra toka jambo jingine lililopo ambalo ni hatarishi zaidi kiutawala.
Njia nyingine ni ile iliyotumika tangu ukoloni ya watawanye uwatawale (Divide and rule policy).
Ukiwapa nafasi au fursa watawaliwa wakakaa, wakapanga wakaelewana na nyie mpompo tu mkiwaangalia, jua siku watakapozua ajenda ya kushughulika na wewe, ujue umekwenda. Dawa ni kuwafanya siku zote wasielewane kwa kuwagonganisha vichwa wenyewe kwa wenyewe tena kwa mambo madogo yasiyo hitaji gharama kubwa na nguvu nyingi. Tulijadiliana sana na kwa urefu na Sheikh Ponda juu ya mambo haya lakini hatukupata jibu la mwisho na kwa bahati mbaya au nzuri Mungu akawa amezisikia dua zake na sala zake za masaa zaidi ya 18 kila siku akawa amechomolewa Segerea na kuniachia Sello No. 3. Najua Mungu atatukutanisha tena Inshallah! Ila, isiwe tena Segerea au Keko ili tuhitimishe mada hiyo.
Siku moja kabla ya kusomewa hukumu yake na Hakimu Nongwa (9/5/2013) tulijadili sana hukumu yake kwamba inaweza kuwa ya mwelekeo gani na maamuzi yapi. Panga pangua ilishindikana kueleweka mambo yatakuwaje kutokana na mazingira yaliyokuwa yakiizunguka kesi yenyewe. Mawakili wake walikuwa wameifanya kazi yao vyema bila kubakiza punje ya shaka. Lililokuwa likimpa faraja zaidi na kesi yake ni kusikia kwamba huyo hakimu ni mama mlokole, ameokoka. Hiyo ilikua ikimpa moyo sana kwamba atahukumiwa na kupewa haki yake sawa na lile lililozungumzwa na kuwasilishwa mbele ya hakimu Nongwa.
Nilimuuliza endapo hukumu itamuweka katika mazingira ya kumkata makali yake ya kazi ya utetezi anayoifanya na wakati huohuo upande wa pili wa system ukamtaka aanze kutoa Ushirikiano atafanyaje? Sheikh Ponda aliniambia kuwa haki huwa hainunuliwi wala kuombwa bali hudaiwa. Alisema atakuwa tayari kutoa ushirikiano kwa yeyote yule anayezungumzia utoaji na upatakanaji haki.Na akasema mdomo na nafsi vilivyodhamiria kuzungumzia na kuitafuta haki huwa havifungiki kwani vikifungika hata hiyo amani haiwezi kuwepo.
Nikiwa ndani ya selo nilimsikia Sheikh Ponda akimwaga mistari yake redioni baada ya kuhukumiwa. Kwa mara nyingine nikazidi kumuaminia Sheikh Ponda kwamba ni mmojawapo ya watu wachache tulio nao hivi sasa nchini wanaoweza kutembea na kuishi ndani ya maneno yao.
Lipo jambo moja muhimu ambalo tulikubaliana na Sheikh Ponda tulijadili na kulifanyia kazi kwa nia ya kuwanusuru watu wanaosota jela bila sababu endapo tungeliachiwa na kuwa huru uraiani. Namtafuta kwenye simu hayuko reachable. Nikishampata tukashauriana na likaonekana linatekelezeka, nitalitoa hadharani.
6: USHAURI WANGU MDOGO KWA VIONGOZI WETU WA DINI.
Mimi ni mtu mdogo sana na muumini wa kawaida ndani ya dhehebu la KKKT. Lakini natambua kanisa ni waumini na wajibu mkubwa wa kila muumini ni kuhakikisha anatimiza wajibu wake kama kanisa la Mungu linavyoelekezwa kupitia maandiko matakatifu ya Biblia. Wajibu mmojawapo sisi kama waumini ni kuonyana ( Ebr. 10:24 25).
Nawaombeni viongozi wetu wa dini zote wakristo kwa waislamu mtimize wajibu wenu mliokabidhiwa na Mungu, Imeandikwa kwa dini zote kwamba kila mmoja bila kujali wadhifa wake atahukumiwa sawa na matendo yake. Nawaomba simamieni na kuuzungumza ukweli(hata kama ni mchungu) mbele ya watawala na hata watawala watarajiwa.Ninyi mmepewa mamlaka na Mungu ya kuonya, kukemea, kuelekeza na kubariki na ndio maana watawala wote wanawaogopa na kuwaheshimu. Wengine huenda ninyi bila ya kuwatambua hutafuta njia za kujikomba kwenu ili wakipate wanachokitafuta.Yasemeni wazi na kuyahoji hata yale machache yanayoonekana au kusikika pasipo kificho.
Muulizeni Mheshimiwa Rais huyo waziri wake anayezungumzwa kila siku kwamba mchana kweupe alisema anao maadui zake wawili ambao ni waandishi wa habari na angewashughulikia, Rais analisemaje hilo? Maadam ni ninyi, nina uhakika Mheshimiwa Rais atajibu na atachukua hatua stahiki.
Binafsi nawaombeni kwa heshima na taadhima muache kuwa vuguvugu (si moto si baridi-Ufunuo wa Yohana 3:15-16) Baadhi yenu acheni kuogopa vivuli vyenu kwa maana ya kuhofia kunyimwa upendeleo au misaada ya serikali (i.e misamaha ya kodi) na baadhi kuutumia mwanya huo vibaya. Kama maandiko yanavyosema JIKANENI WENYEWE.
Lazima mtambue hawa jamaa wakati mwingine huenda wanaitumia fursa hiyo kama chambo cha kuwanasia pindi wanapokua wana taarifa zenu zote za fursa ya misamaha iliyotumika vibaya. Mnapaswa kushuhudiwa mema na watu walio nje (1 Tim 3:2-9)
Binafsi nawaomba msiwalee wala kuwabeba wale wote wenye dhamira chafu na nia mbaya ya kutaka kuyatumia madhehebu yenu kukidhi matakwa binafsi kwani wanachafua taswira zenu nzuri za madhehebu yenu mbele ya waumini wenu na umma kwa ujumla.
Lakini zaidi ya yote ni imani yangu mimi binafsi kwamba madhehebu yenu ni makubwa na yana mtandao mkubwa na wenye nguvu ndani na hata nje ya nchi.Kama inawezekana tumieni mtandao wenu kuisaidia serikali ambayo vyombo vyake vinaelekea kushindwa kuwabaini wahalifu wachache wanaoelekea kuchafua na kuivuruga amani tuliyoizoea ndani ya nchi yetu. Kwa bahati nzuri nimesoma na kusikia kwenye vyombo vya habari kwamba IGP Mwema amezishauri taasisi za kidini kuanzisha ulinzi shirikishi ndani ya misikiti na makanisa. Kama mambo serikali ya CCM imeyafikisha hapo, tumieni fursa hiyo kuziomba taasisi makini mnazozifikia nje na ndani ya nchi.
"