CHADEMA Imejitofautisha na CCM Katika Kusimamia Maadili

Bams

JF-Expert Member
Oct 19, 2010
16,886
41,996
CHADEMA imedhihirisha kuwa inachukia matendo maovu, na kwenye uovu wamedhihirisha hawana subira wala simile, hawaangalii anayefanya hilo ni wa chama chao au mtu wa nje.

CHADEMA imejitofautisha sana CCM, chama ambacho siku zote kimekumbatia majizi, mafisadi, wala rushwa, wakwepa kodi, alimradi tu mwovu huyo awe ni miongoni mwao. Kama ni kada, kiongozi wa chama, haguswi.

Makamu mwenyekiti wa CHADEMA, mpigania haki, mtu aliyenyoka kwa matendo na kauli, mtu jasiri na mkweli wa nafsi, ndugu Tundu Lisu, hivi karibuni ametoa kauli ya kukemea uovu wa kutumia pesa kuupata uongozi ndani ya chama chake. Mambo hayo huwezi kuyasikia ndani ya Serikali ya CCM wala ndani ya CCM yenyewe, japo inafahamika wazi namna baadhi ya mawaziri wanavyowahonga wanaofanya vetting, ili tu waendelee kuteuliwa na Mh. Rais. Huwezi kuisikia kauli kali ya kukemea uovu kutoka Serikali ya CCM wala CCM yenyewe dhidi ya viongozi na maafisa wa serikali wanaofanya ufisadi, rejea ripoti za CAG. Huwezi kusikia kauli kama ya Lisu kutoka CCM wakati wa kura za maoni, japo tunafahamu jinsi rushwa inavyotembea kwa wajumbe wakati wa kura za maoni.

Tunafahamu kuwa hakuwezi kutokea serikali au chama chochote cha siasa chenye watu watakatifu wote, chama cha hivyo hakipo. Lakini tunatofautisha ubora wa vyama na Serikali kwa kuangalia serikali au chama kinachukua hatua gani dhidi ya waovu.

Hongera Lisu. Umeonesha njia.
 
Duh

Kinana anasema Chadema mlitaka mchakato wa marekebisho ya NEC uhusishe CCM na Chadema tu na vile vyama vingine mvitenge

Huo Ndio Uadilifu?!🐼
 
TAL inabidi apewe nchi, kukemea kwake rushwa kuendane na sheria kali zinazozuia hiyo rushwa isitokee labda nchi yetu hii itapiga hatua sana
 
CHADEMA imedhihirisha kuwa inachukia matendo maovu, na kwenye uovu wamedhihirisha hawana subira wala simile, hawaangalii anayefanya hilo ni wa chama chao au mtu wa nje.

CHADEMA imejitofautisha sana CCM, chama ambacho siku zote kimekumbatia majizi, mafisadi, wala rushwa, wakwepa kodi, alimradi tu mwovu huyo awe ni miongoni mwao. Kama ni kada, kiongozi wa chama, haguswi.

Makamu mwenyekiti wa CHADEMA, mpigania haki, mtu aliyenyoka kwa matendo na kauli, mtu jasiri na mkweli wa nafsi, ndugu Tundu Lisu, hivi karibuni ametoa kauli ya kukemea uovu wa kutumia pesa kuupata uongozi ndani ya chama chake. Mambo hayo huwezi kuyasikia ndani ya Serikali ya CCM wala ndani ya CCM yenyewe, japo inafahamika wazi namna baadhi ya mawaziri wanavyowahonga wanaofanya vetting, ili tu waendelee kuteuliwa na Mh. Rais. Huwezi kuisikia kauli kali ya kukemea uovu kutoka Serikali ya CCM wala CCM yenyewe dhidi ya viongozi na maafisa wa serikali wanaofanya ufisadi, rejea ripoti za CAG. Huwezi kusikia kauli kama ya Lisu kutoka CCM wakati wa kura za maoni, japo tunafahamu jinsi rushwa inavyotembea kwa wajumbe wakati wa kura za maoni.

Tunafahamu kuwa hakuwezi kutokea serikali au chama chochote cha siasa chenye watu watakatifu wote, chama cha hivyo hakipo. Lakini tunatofautisha ubora wa vyama na Serikali kwa kuangalia serikali au chama kinachukua hatua gani dhidi ya waovu.

Hongera Lisu. Umeonesha njia.
Ujinga kabisa! Mimi nilifikiri huyo Lissu ameufuta Uchaguzi kwa sababu umegubikwa na rushwa! Kumbe amekemea tu? Toothless bull dog!!!
 
Hizi pesa za abduli na mam'ake zimeleta balaa, hadi nyani ateme bungo.
 
Ujinga kabisa! Mimi nilifikiri huyo Lissu ameufuta Uchaguzi kwa sababu umegubikwa na rushwa! Kumbe amekemea tu? Toothless bull dog!!!
Ukiwa punguani, jaribu kuuficha kwa kiasi fulani.

Hujasikia maeneo ambayo uchaguzi wa viongozi wa CHADEMA ngazi ya mkoa, umefutwa kwa sababu ya kukiuka kanuni? Lisu siku zote anatembea juu ya maneno yake. Siyo mtu wa porojo kama wewe.

Lisu yupo hatua nyingi mbele kumzidi kiongozi yeyote wa CCM.

Kumbuka maneno ya jaji Warioba alipoulizwa endapo Lisu akiwa Rais. Warioba alisema:

"Nina imani atakuwa Kiongozi mzuri, ILA Lisu akiwa Rais, itabidi sote tujifunze kutii sheria na katiba"
 
Ukiwa punguani, jaribu kuuficha kwa kiasi fulani.

Hujasikia maeneo ambayo uchaguzi wa viongozi wa CHADEMA ngazi ya mkoa, umefutwa kwa sababu ya kukiuka kanuni? Lisu siku zote anatembea juu ya maneno yake. Siyo mtu wa porojo kama wewe.

Lisu yupo hatua nyingi mbele kumzidi kiongozi yeyote wa CCM.

Kumbuka maneno ya jaji Warioba alipoulizwa endapo Lisu akiwa Rais. Warioba alisema:

"Nina imani atakuwa Kiongozi mzuri, ILA Lisu akiwa Rais, itabidi sote tujifunze kutii sheria na katiba"
Sijasikia. Nitajie nifuatilie.
 
Sijasikia. Nitajie nifuatilie.

Sehemu mojawapo niliyo na uhakika, uchaguzi wa mwenyekiti wa mkoa na wajumbe wake ulifutwa kwa sababu ya kukiuka kanuni. Sikumbuki tarehe, lakini utarudiwa tena.

"Kamati Kuu ya CHADEMA imetangaza kurudiwa kwa uchaguzi wa Mkoa wa Njombe kwa ngazi zote kutokana na kukosekana kwa USIRI wakati wa kupiga kura na kuchanganya mabaraza yote ndani ya ukumbi mmoja wakati wa kupiga kura na udanganyifu mwingine uliofanyika ndani ya ukumbi.

Uchaguzi wa marudio utasimamiwa na Viongozi wa Chama kutoka Taifa"
 
CHADEMA imedhihirisha kuwa inachukia matendo maovu, na kwenye uovu wamedhihirisha hawana subira wala simile, hawaangalii anayefanya hilo ni wa chama chao au mtu wa nje.

CHADEMA imejitofautisha sana CCM, chama ambacho siku zote kimekumbatia majizi, mafisadi, wala rushwa, wakwepa kodi, alimradi tu mwovu huyo awe ni miongoni mwao. Kama ni kada, kiongozi wa chama, haguswi.

Makamu mwenyekiti wa CHADEMA, mpigania haki, mtu aliyenyoka kwa matendo na kauli, mtu jasiri na mkweli wa nafsi, ndugu Tundu Lisu, hivi karibuni ametoa kauli ya kukemea uovu wa kutumia pesa kuupata uongozi ndani ya chama chake. Mambo hayo huwezi kuyasikia ndani ya Serikali ya CCM wala ndani ya CCM yenyewe, japo inafahamika wazi namna baadhi ya mawaziri wanavyowahonga wanaofanya vetting, ili tu waendelee kuteuliwa na Mh. Rais. Huwezi kuisikia kauli kali ya kukemea uovu kutoka Serikali ya CCM wala CCM yenyewe dhidi ya viongozi na maafisa wa serikali wanaofanya ufisadi, rejea ripoti za CAG. Huwezi kusikia kauli kama ya Lisu kutoka CCM wakati wa kura za maoni, japo tunafahamu jinsi rushwa inavyotembea kwa wajumbe wakati wa kura za maoni.

Tunafahamu kuwa hakuwezi kutokea serikali au chama chochote cha siasa chenye watu watakatifu wote, chama cha hivyo hakipo. Lakini tunatofautisha ubora wa vyama na Serikali kwa kuangalia serikali au chama kinachukua hatua gani dhidi ya waovu.

Hongera Lisu. Umeonesha njia.
Chadema ipi? Hii iliyozunguka nchi nzima ikimtangaza Lowasa Fisadi baadaye ikamchukua kuwa mgombea uraisi baada ya kuhongwa ikamwacha Slaa kuwa mgombea?
 
Ukiwa punguani, jaribu kuuficha kwa kiasi fulani.

Hujasikia maeneo ambayo uchaguzi wa viongozi wa CHADEMA ngazi ya mkoa, umefutwa kwa sababu ya kukiuka kanuni? Lisu siku zote anatembea juu ya maneno yake. Siyo mtu wa porojo kama wewe.

Lisu yupo hatua nyingi mbele kumzidi kiongozi yeyote wa CCM.

Kumbuka maneno ya jaji Warioba alipoulizwa endapo Lisu akiwa Rais. Warioba alisema:

"Nina imani atakuwa Kiongozi mzuri, ILA Lisu akiwa Rais, itabidi sote tujifunze kutii sheria na katiba"
Lisu mla mla rushwa mkubwa ukiona anamsema kiongozi mkubwa anataka hongo la Hela akipewa anaufyata .

Yeye ndie alikuwa kinara wa kusema Lowasa fisadi alipopewa pesa za hongo akaufyata na akiwemo mchungaji Msigwa alidai na Mimi je mbona hamjanipa Hela? Lissu akasema Lowasa mtu safi baada ya kuhongwa Hela na Lowasa akasema ruksa kugombea uraisi Kisiki Cha kupenda Rushwa Kwa kutukakana viongozi wakubwa ili waje kumhonga ilikuwa Kwa Magufuli Hadi akakimbia Hadi nchi .

Magufuli alikuwa haendekezi rushwa kuwahonga wanaomtukana kisiasa

Sasa hivinLisu anatukana wee ni invitation to treat ni mayowe ya kutaka rushwa kuwa kama hamtaki niendelee kuwatukana leteni pesa kama Lowasa alivyofanya pale

Lisu sio mwanasiasa ni muwinda rushwa na hiyo tabia kaianza siku nyingi alikuwa akitukana makampuni ya madini anatoa mimacho utafikiri mtetezi sio Ndio huyu wakimpa pesa anaufyata serikali ikitaka kukomaa maeneo Yale alipiga Domo kuwa makampuni ya madini yanatuibia anaanza kuwatetea kuwa oh msiwaguse mtapelekwa mahakama za Kimataifa za MIGA

Akitukana viongozi lengo kuwaita mezani wamhonge anyamaze Kisiki alikwaa Kwa Magufuli na Sasa anakwaa Kwa Samia hakuna mtu wa kumpa Rushwa aendelee kubwabwaja Hadi Domo likauke mate hakuna Rushwa atapata
 
Back
Top Bottom