Sigara Kali
JF-Expert Member
- May 28, 2017
- 3,623
- 8,428
Ama kweli kuishi na mke kunahitaji uvumilivu Sana
Nimekuwa na mwanamke huyu almost miaka 8, tuna watoto wawili.
Mke wangu ni muajiriwa na analipwa vizuri tu,siku za nyuma tulikuwa tunaishi kwa furaha Sana japo ni mikoa tofauti ila ni ya jirani
Kwa miaka 7 tumeishi bila ndoa Hadi tulipoamua kufunga ndoa ya bomani mwaka huu.
Mke wangu huyu ni mtu mwenye wivu kupindukia na ana asili ya kukaa na kinyongo moyoni Hali inayopelekea tuwe na migogoro ya hapa na pale.
Sasa miezi kadhaa nyuma alikuja mkoa ninaoishi ,akakutana na majirani akapewa umbea kwamba kuna binti wa nyumba ya jirani namla,basi Yeye na majirani wakaweka mtego,wife akaniaga anarudi kwake na hapo tayari tulishagombana,nikamwambia poa kumbe kajificha Ili amkamate yule binti
Sasa nilimpigia simu binti aniletee mboga kutoka sokoni,ile anaingia tu ndani wife nae kaingia kaanza kumpiga yule binti ,bahati nzuri binti akakimbia.
Hali ya mgogoro na wife ikawa mbaya zaidi,nikamwita rafiki angu tukaongea na wife na nikamwomba samahani, tukayamaliza akaondoka.
Sasa tangu wakati huo mawasiliano yamekuwa finyu Sana,nimejaribu Sana kumwomba msamaha lakini naona mwenzangu hataki suluhisho,sina mchepuko na nimeachana kabisa na mipango ya kando.
Hivi karibuni nimekuja kumtembelea wife na kuwaona watoto naona mwenzangu hana time na Mimi na ana tabia ya kukumbushia mambo yaliyopita miezi zaidi ya 5 sasa, hatuna amani,tangu nije hakuna mazungumzo yoyote, hata unyumba sijapewa na nimekosa kabisa mzuka nae.
Nikiri hata yeye na ndugu zake akiwemo mama yake walinikosea Sana ila mi nilisamehe na maisha yakaendelea.
Sasa nashindwa kuelewa huyu mwenzangu anataka nini hasa kama msamaha nilimwomba ila naona bado ana kinyongo miezi zaidi ya 5 sasa hadi furaha na mzuka wa kuwa nae umeniisha kabisa yani tunaishi Ili mradi tu.
Naombeni ushauri nifanyaje Ili huyu mwanamke aache kisirani chache na kuninunia!? Manake nimemvumilia Hadi nimechoka sioni sababu ya yeye kuendelea kununa na kuwa na mawasiliano hafifu na Mimi kana kwamba yeye hajawahi nikosea na nikamsamehe.
Sometimes najiuliza au kazi na mshahara mzuri alio nao ndo unampa kiburi Hadi anione mi mkosaji na kila siku akumbushe makosa yangu..!!?
Ushauri tafadhali.
Nimekuwa na mwanamke huyu almost miaka 8, tuna watoto wawili.
Mke wangu ni muajiriwa na analipwa vizuri tu,siku za nyuma tulikuwa tunaishi kwa furaha Sana japo ni mikoa tofauti ila ni ya jirani
Kwa miaka 7 tumeishi bila ndoa Hadi tulipoamua kufunga ndoa ya bomani mwaka huu.
Mke wangu huyu ni mtu mwenye wivu kupindukia na ana asili ya kukaa na kinyongo moyoni Hali inayopelekea tuwe na migogoro ya hapa na pale.
Sasa miezi kadhaa nyuma alikuja mkoa ninaoishi ,akakutana na majirani akapewa umbea kwamba kuna binti wa nyumba ya jirani namla,basi Yeye na majirani wakaweka mtego,wife akaniaga anarudi kwake na hapo tayari tulishagombana,nikamwambia poa kumbe kajificha Ili amkamate yule binti
Sasa nilimpigia simu binti aniletee mboga kutoka sokoni,ile anaingia tu ndani wife nae kaingia kaanza kumpiga yule binti ,bahati nzuri binti akakimbia.
Hali ya mgogoro na wife ikawa mbaya zaidi,nikamwita rafiki angu tukaongea na wife na nikamwomba samahani, tukayamaliza akaondoka.
Sasa tangu wakati huo mawasiliano yamekuwa finyu Sana,nimejaribu Sana kumwomba msamaha lakini naona mwenzangu hataki suluhisho,sina mchepuko na nimeachana kabisa na mipango ya kando.
Hivi karibuni nimekuja kumtembelea wife na kuwaona watoto naona mwenzangu hana time na Mimi na ana tabia ya kukumbushia mambo yaliyopita miezi zaidi ya 5 sasa, hatuna amani,tangu nije hakuna mazungumzo yoyote, hata unyumba sijapewa na nimekosa kabisa mzuka nae.
Nikiri hata yeye na ndugu zake akiwemo mama yake walinikosea Sana ila mi nilisamehe na maisha yakaendelea.
Sasa nashindwa kuelewa huyu mwenzangu anataka nini hasa kama msamaha nilimwomba ila naona bado ana kinyongo miezi zaidi ya 5 sasa hadi furaha na mzuka wa kuwa nae umeniisha kabisa yani tunaishi Ili mradi tu.
Naombeni ushauri nifanyaje Ili huyu mwanamke aache kisirani chache na kuninunia!? Manake nimemvumilia Hadi nimechoka sioni sababu ya yeye kuendelea kununa na kuwa na mawasiliano hafifu na Mimi kana kwamba yeye hajawahi nikosea na nikamsamehe.
Sometimes najiuliza au kazi na mshahara mzuri alio nao ndo unampa kiburi Hadi anione mi mkosaji na kila siku akumbushe makosa yangu..!!?
Ushauri tafadhali.