what is it?

mail
Kweli kabisa bado nakua ..............ila mada tunayojadili imeeleweka? ni kuhusu maana sahihi ya upinzani sio kuhusu kukua kwangu hebu naomba hoja zijibiwe kwa hoja sio dhihaka hakuna haja ya dhihaka tunajadili mambo ya msingi hapa.
 
mail
Kweli kabisa bado nakua ..............ila mada tunayojadili imeeleweka? ni kuhusu maana sahihi ya upinzani sio kuhusu kukua kwangu hebu naomba hoja zijibiwe kwa hoja sio dhihaka hakuna haja ya dhihaka tunajadili mambo ya msingi hapa.

Soma hapo juu wakubwa walio tangulia kuona siku kabla yako wanavyo kuelimisha acha ubishi.
Ukisha maliza thread ifungwe
 
dogo umeongea point to be noted " Mara nyingin upinzani wa Tanzania umejikita katika propaganda na sio hoja" alafu broda ile issue ya kutafuta g.f kama mdau pale juu alivokuanika ni kweli! nakupa ushauri trust no body on-line sansana issue za kutafuta wachumba! basi kama ukipata mwambie akutumie picha nzima juu mpaka chini?! jitahidi sana kutongOza kavukavu.. uso kwa uso!! mwisho nakushauri CHAGUWA KIKWETE!! SAY NO TO SLAA!!
 
mail
Kwa kawaida huwa napenda kujadili kwa hoja na si kashfa wala mzaha hayo yana wenyewe mimi siyawezi
 
1. Upinzani ulikosoa mikataba mibovu wakatoa altenative ya kuifuta na kupeleka mahakamani wote waliohusika
2. Upinzani ulikosoa ufisadi ndani ya serikali na kuwataja kwa majina wahusika ili washughulikiwe
3. Upinzani ulikosoa bajeti za serikali na kutoa altenative bajeti tena isiyotegemea wafadhili by 100%
4. Upinzani ulipinga matumizi makubwa ya serikali na kutoa ushauri wa jinsi ya kupunguza matumizi hayo ili fedha nyingi iende kwenye maendeleo
5. etc, etc, etc, n.k, n.k..............................

Nini zaidi unataka wafanye ili wawe zaidi ya upinzani?????????
 
Nova hapo kidogo nakuelewa, upinzani ni zaidi ya kupinga, they suppose nao kuingia kusaidia wananchi katika mapambano dhidi ya umaskini, si kupinga kwa kila chama tawala kinachofanya, na kutaja figures mbalimbali za kushindwa. umejitahidi though nimepata mwanga who is Nova, and i think Nova, si kamwanfunzi kama kanavodai ila ni au basi naogopa infedelity....
 
Naomba nichangie hoja hii kwa kifupi tu, nimeshindwa hata kumalizia kusoma sawa sawa hayo yaliyo andikwa na jamaa pale juu. Anieleze yeye angefanyaje kama angekuwa kiongozi lakini si wa ngazi ya juu ya mwisho katika maamuzi, halafu anatoa ushauri sahihi na wananchi wanaona utawasaidia, halafu kiongozi mwamuzi anapuuzia na kufanya maamuzi ya makusudi tena ya kijinga na siyo ya kizalendo ila ni hujuma za wazi ! Je haitakuwa sahihi kuyaweka bayana hayo na hivyo wananchi kuyajua na kufanya maamuzi ya kumfukuza au kumngóa huyo mbovu kutoka kuwa na maauzi na kumpa yule anayeonekana kujali ! UONGOZI MBOVU NI LAZIMA UNGÖLEWE NA SI BLA BLA ZAKUOMBANA KILA SIKU KAMA WAO NI HAKI YAO KUTAWALA IWE IWEJE NA LAZIMA WABEMBELEZWE KUTEKELEZA WAJIBU WAO NA MWISHO WAABUDIWE NO, Wakati umefika lazima waondolewe!
 
WATANZANIA UPINZANI SI KUPINGA NI KUTOA MAWAZO MBADALA
Inapofikia wakati watu wanapotoshwa kijinga jinga tu kuna hatari
taifa likaangamia au kutoweka kabisa. Kwa jinsi vyama vya upinzani
vilivyo Tanzania nachelea kusema kuwa maana ya upinzani haijaeleweka
hata kidogo na kwenye makala hii nitaweka wazi ili nieleweke vizuri
siwezi kuendelea kukaa kimya ilihali uwezo wa kuielimisha jamii ninao
kwa maana hata mwanaharakati Martin Luther King Jr anasema kuwa wale
wenye uwezo wa kuongoza wanapokaa kimya kwenye jamii sio tu kuna
hatari ya kuongozwa na wajinga ,King anasema hata mawe yatatawala ,
binafsi sioni sababu kwanini nifumbie macho propaganda zinazoendeshwa
na vyama vya upinzani ambazo kimsingi hazina tija kwa Tanzania ya leo
wala ya kesho, sasa naomba nizame kwenye mada yenyewe nayotaka
kuidadavua na kimsingi nitangulie kusema kuwa katika uchambuzi wangu
huu nitajitahidi kutoa ufafanuzi wangu kwa misingi ya hoja ili
nikibidi kujibiwa nijibiwe pia kwa misingi ya hoja na sio hoja bali
hoja zenye mantiki na mashiko pia.
Upinzani hauna maana nyingine ila kuharakisha maendeleo ya wananchi,
hata leo hii ukienda kwenye za magharibi vyama vya upinzani vimekuwa
mstari wa mbele kuhakikisha kuwa wananchi wanapata maendeleo iwe kwa
kuihimiza serikali au kushiriki moja kwa moja katika kusaidia wananchi
kujiletea maendeleo sasa hii ni tofauti na kwetu ambapo vyama vya
upinzani vimekuwa mstari wa mbele kuongelea umaskini wa watu pasipo
kusaidia watu hao kujiletea maendeleo, hapa kidogo inashangaza kuona
kuwa kiu ya watu ni maendeleo sio kuambiwa wao ni maskini kwa kiwango
gani lakini cha ajabu vyama vya upinzani hawalijui ili wao wanadhani
kazi yao ni kuwaminisha watanzania kuwa ni maskini sana kuliko watu
wote Duniani na wakitaka kuwa na maendeleo kama Marekani basi ni
kuing'oa madarakani CCM huku wakishindwa kujadili kisayansi juu ya
tofauti kubwa iliyopo baina ya Tanzania na Marekani kwa maana Tanzania
ina miaka 49 ya uhuru marekani ina miaka 250 ya uhuru, usawa uko wapi
hapa?
Upinzani ni lazima kuisaidia seikali kutimiza vipaumbele vya taifa,
nakumbuka falsafa ya rais wa awamu ya tatu wa Tanzani mzee Benjamin
Mkapa aliyepata kusema kuwa, katika maisha ni muhimu kuwa na
vipaumbele lakini ukikosa kutambua kipaumbele cha vipaumbele hakika
wewe ni mjinga , hapa Mzee Mkapa anatufundisha kuwa katika maisha ni
lazima kuwa na vipaumbele kwa mantiki hiyo kwenye uwanja wa siasa za
Tanzania ni lazima kama taifa tuwe na vipaumbele ambavyo vitaungwa
mkono na watanzania wote licha ya tofauti zao za kisiasa . Mfano mzuri
ni swala la elimu , hili si jambo la kuendeshwa kisiasa hata kidogo,
si jambo la kufanywa mtaji wa kisiasa kabisa, haiingii akilini kuona
kuwa wakati serikali ya CCM imejenga shule za kata vyama vya upinzani
vinapinga tu bila kutoa hoja za msingi sababu inayoimbwa kila uchao
ni moja tu nayo ni hazina maana shule hizo hazifai kabisa. Sasa hapa
kuna mambo ya kujiuliza, unawezaje kuitwa mume bila kuoa? Au unawezaje
kuwa na shule bora bila kuwa na shule kwanza? Au tuseme unawezaje
kuwa na nyumba bila msingi kwanza?, hapa kuna hatari kuwa vyama vya
upinzani Tanzania havijui vipaumbele vya kitaifa ndio maana wanataka
kutatua matatizo ya kielimu kwa mbinu za kisiasa(they seem to solve
academic problems on the basis of political techniques) kwamba sasa
badala ya kujadili jinsi gani ya kuboresha shule za kata ili ziwe na
ubora sasa shule za kata zinataka kufanywa ndio sababu hasa ya
kuiondoa CCM madarakani, hata rais Kikwete alipata kunena kuwa
tusherehekee tofauti zetu lakini tubaki wamoja(let's celebrate our
differences but keep our unity) hapa nacholenga kukisema hapa ni kuwa
lazima tuwe wamoja kwanza tofauti baadae(unity in diversity) na sio
tofauti kwanza umoja baadae(diversity in unity), hivyo kwa mantiki ya
kawaida nilitegemea hoja za wapinzani kuhusu shule za kata zilenge
namna ya kuboresha shule hizo na sio wimbo wa hazina maana ambao
tumeanza kuuchoka.
Ni lazima kuunga mkono mambo ya muhimu , upinzani wenye tija ni ule
unaounga mkono serikali kwenye mambo ya muhimu ambayo hayahitaji
mijadala ya kisiasa ila yanahitaji utekelezaji wa wananchi wote licha
ya tofauti zao kisiasa mfano swala la kilimo kwanza halihitaji
mijadala ya kisiasa ila utekelezaji, hapa nategemea upinzani wenye
tija kuwahimiza watanzania kuunga mkono kauli mbiu hiyo kwa vitendo na
sio kupinga pinga tu bila hoja , kimsingi vyama vya upinzani vinapaswa
kujua kuwa sio kila linaloasisiwa na chama tawala ni lazima lipingwe
huu ni ujinga mambo mengine yanafaa kuungwa mkono bila kuangalia
chama gani kimeliasisi jambo hilo, cha msingi kinachopaswa kuangalia
je jambo hilo lina tija kwa taifa?
Popularism inajengwa kwa hoja sio propaganda, hili ni jambo lingine
ambalo ni muhimu vyama vya upinzani vikalifanyia kazi kwamba
popularism(umaarufu kwa wananchi) hauletwi kwa propaganda bali hoja
ambazo zinawagusa wananchi, hapa kuna la kujifunza kutoka kwa Obama wa
Marekani ambaye umaarufu wake haukuletwa kwa propaganda bali hoja kwa
maana hatari ya propaganda huwa zinaimbwa redioni na majukwaani na
zinakinaisha lakini hoja huwa zinaishi mioyoni mwa watu na kukaa
vichwani mwao. Mara nyingin upinzani wa Tanzania umejikita katika
propaganda na sio hoja, nitoe angalizo kuwa Intelligent people discuss
ideas(wenye akili zaidi hujadili hoja), Normal people discuss
events(wenye akili za kawaida wanajadili matukio) and stupid people
discuss people(na wajinga hujadili kuhusu watu), sasa kwa kawaida
propaganga hujikita kwenye kuwajadili watu kila uchao huu kwa maana
nyingine ni ujinga, upinzani wa Tanzania unapaswa kulijua hili.
Upinzani sio upingaji, bila shaka hili ndicho ambacho kinanifanya
niamini kuwa somo la upinzani halijaeleweka Tanzania kwa maana vyama
vya upinzani vimejigeuza majukwaa ya kupinga serikali yachama tawala,
huku ni kukosa maono kwa maana mpinzani sio lazima kupinga kila mda
wakati mwingine ni busara Zaidi kuunga mkono , kutokana na hulka hii
ya kupinga vyama vya upinzani vimekuwa havipo tayari kukubali hata
matokeo ya uchaguzi , kila baada ya uchaguzi maneno CCM wameiba kura
limekuwa ni kiitikio cha wimbo maarufu wa hakuna uwanja sawa wa
kisiasa nchini. Vyama vya upinzani vinapaswa kuwa vyama mbadala na
kutoa changamoto sasa ni wakati wa kuamka na kuwa vyama vya upinzani
hai na sio kuendelea kuwa vyama vya upingaji.
Naomba nimalizie makala yangu kwa shairi langu fupi nililotunga
mwenyewe ili vyama vya upinzani waweze kukumbuka na kuzingatia haya
niliyojadili kwa maana hata wanasaikolojia mabingwa duniani wanaamini
mashairi ni moja ya njia kuu za kufanya mtu akumbuke kitu fulani,
shairi langu ni kama ifuatavyo;
UPINZANI SI UPINGAJI
1. Inafaa kutambua , maana ya upinzani
Yafaa kuzingatia, kuyaweka akilini
Haifai kukandia, walio madarakani
Kiu ya watu maendeleo, malumbano hawataki.

2. Uzalendo si kelele, ni kupenda nchi yako
Changamoto ziko tele, onyesha mchango wako
Taifa lisonge mbele, kutoka hapa tuliko
Upinzani sio kupinga, inafaa kutambua.

Makala hii imeandikwa na Novatus Kambota wa Vijana Zaidi na Kuhaririwa
na Gama , mwandishi wa makala hii anapatikana kwa anwani ya barua
pepe; novakambota@gmail.com au mtembelee kwenye blog (wavuti) yake ya;
www.novadream.blog.com
 
Naona wanajukwaa hamjanishawishi kwa hoja kwa hivyo nawapa mda jipangeni kesho nakuja kivingine
 
mail
Naona hoja imehama bwana imekuwa sio maana ya upinzani tena ni kuhusu mimi kutafuta girl................aah...........binafsi sidhani kama hilo lililoibuliwa litatusaidia kuelewa maana ya upinzani hebu tujadili mambo ya msingi..............nimechambua kwa hoja inabidi nijibiwe kwa hoja sio mzahamzaha .........tuchambue mambo yenye tija kwa taifa ......tujadili kwa mantiki mzaha sio mda wake huu.............kama umeshindwa mada haijaeleweka ni heri kaa pembeni kwa maana kujiuzulu sio udhaifu tu wakati mwingine ni ujasiri kuyaacha yapite(resigning does not only mean you are weak , sometimes it means you are strong enough to let it go)


Kama mheshimiwa fulani sio!!

Hapa vipi? "TUMEHUZUNIKA PAMOJA, TUTASHINDA PAMOJA"

Hawa jama kwa kujifariji tu na kuwafanya watanzania ni wajinga! haya endeleeni tu, IPO SIKU!!
 
mail
mimi na hoja tu ila zipo kwenye makala yangu ............narudia tena upinzani ni zaidi ya kulalamika.............upinzani wa kweli unajali vipaumbele vya taifa sio kuendesha propaganda kila uchao.............bwana mutu hebu jaribu kuchambua hoja zangu sio kuniuliza iwapo na hoja au la? Mimi hoja ninazo za kutosha tu lakini hebu chambua hoja zilizopo kwenye makala yangu kaka.


unaweza kutuambia kipaumbele cha taifa hili?
 
Nova hapo kidogo nakuelewa, upinzani ni zaidi ya kupinga, they suppose nao kuingia kusaidia wananchi katika mapambano dhidi ya umaskini, si kupinga kwa kila chama tawala kinachofanya, na kutaja figures mbalimbali za kushindwa. umejitahidi though nimepata mwanga who is Nova, and i think Nova, si kamwanfunzi kama kanavodai ila ni au basi naogopa infedelity....


WACHA UBISHI NA WEWE INA MAANA UNASHINDWA ATA KU_GOOGLE WHO IS NOVA? BASI ATA KUSOMA HAPA?

NARUDIA TENA, NOVA IS...

Posted: 16/08/2009, 12:21
Iam a boy aged 20 years living in Arusha Tanzania East Africa iam looking for a girl of any age the one who will love the one to care me. For more about me visit www.novadream.blog.com and my phone number is +255766730256 talk to me and welcome to mt kilimanjaro the highest peak in Africa.
Posted By: nova kambota
Location: United Republic of Tanzania
Email: novakambota@gmail.com

 
Nova Kambota,
Mkuu kwanza labda ujifunze kutokana na mada hii kwamba Upinzani ni kutokubaliana na maamuzi ya mwingine iwe hata ktk hoja hii umepata Upinzani. sasa sii lazima wakuunge mkono kwa kila analoongea ila pia sii lazima wakubaliane na hoja nzima.

Nitakupa mfano, Uliposema watu wasizungumzie Umaskini, hapo unaweza kuwa na uzito wa hoja lakini kosa linakuja pale unaposema kwamba wasizungumzie Umaskini umaskini wa watu pasipo kusaidia watu hao kujiletea maendeleo, na ukaendelea kudai kwamba hata nchi za magharibi Upinzani hushiriki iwe kwa kuihimiza serikali au kushiriki moja kwa moja katika kusaidia wananchi kujiletea maendeleo.

Ni maneno mazuri sana kuyasoma, yanavutia sana lakini hapa umeshindwa kabisa kuonyesha role ya vyama hivyo tofauti na vyama vya Tanzania kwa sababu Chadema, CUF na TLP hizi zote zinafanya kazi hiyo hiyo unayodai hawafanyi ktk majimbo waliyoshinda uchaguzi. Ikiwa unawalenga haswa Chadema, nenda Karatu, Tarime na Kigoma utazame kazi waliyoifanya kuwakilisha wananchi wao..

Na katika kuhimiza serikali sijui kama umefuatilia sana mijadala ya bunge pamoja na hata makala za wabunge wa Upinzani ambao hawakuchoka kuzungumzia Mapungufu ya mikakati iliyopo ktk kuharakisha maendeleo hayo. Tojka maswala ya Ufisadi hadi ahadi za Kikwtete hakika wanaowakumbusha CCM siku zote ni Vyama vya Upinzani..Kama chama tawala kingekuwa kikiwasikiliza Upinzani na kufuata maagizo yao sidhani kama tungefikia hapa tulipo leo.

Pili umelenga kutozungumzia Umasikini kwa sababu hawa watu wanataka kufananisha Tanzania na Marekani.. Hapo pia unaweza kuwa na hoja ya msingi lakini makosa yako yanarudi palepale kupata upinzania unaposema Ati Marekani ina mikaa 250 ya Uhuru na Tanzania ina miaka 50.

Labda nikukumbushe tu kwamba kuwa huru miaka mingi haina maana ya maendleo zaidi kwani kama ingekuwa hivyo Haiti na hata Ethiopia zingekuwa na maendeleo makubwa sana..Nchi kama Oman ambazo Sultan wake alifikia kututawala sisi mbona nazo maskini ikiwa Umri ndio kielelezo cha maendeleo, wakati huo huo nchi kama Purto Rico na Malaysia zimeweza kubadilika in the last 30 yrs of independence. Soiuth Afrika waliendfelea hata kabla ya Uhuru kwa hiyo unataka kusema hawakuwa na haja ya Uhuru?.. kitu gani kinachoshabihisha maendeleo ya Uhuru?...

Kwa hiyo mkuu hatuwezi kulinganisha Tanzania na Marekani kwa sababu ni nchi mbili tofauti zenye Watu na Mazingira tofauti lakini sio sababu ya Umri. Na kibaya zaidi ni pale tutakapo fikiria kwamba taifa letu ni changa sana hivyo hatuna haraka wala sababu ya kuendelea sasa hivi..

Kwa hiyo, mkuu wangu ni makosa kweli kuzungumzia Umaskini pasipo kufanya lolote lakini kama vyama vya Upinzania vimeweza kuzungumzia Umaskini kwa lengo la kubadilisha katiba, kupinga Ufisadi, kuhimiza serikali kupunguza baraza la mawaziri na hata kukata matumizi makubwa ya anasa basi huu ndio upinzani unaojenga isipokuwa CCM kwa kiburi chake ndio hawataki kusikiliza.

Na sii kweli kwamba haitakiwi kabisa kuzungumzia Umaskini kwani hili ndilo tatizo letu linalotakiwa kuwa wazi kabisa..Binadamu kuficha au kukana maradhi ni kutafuta kifo kwani huwezi pata dawa wala kinga ya maradhi ulokuwa nayo pasipo kutambua kwanza unaumwa nini?. Na ili tupate kupiga hatua moja mbele ni lazima ufahamu tumesimama wapi. Umaskini wetu ni sawa na maradhi hatuhitaji kuficha wala kuukana, ni lazima umaskini huu uzungumziwe kwani ndipo tuliposimama. Hata ukiuliza nchi za nje kuhusu Afrika au Tanzania kitu cha kwanza kinachowaingia akilini ni umaskini wa nchi hizi.

Mwisho, mkuu wangu haya maneno ya Kikwete ati tusherehekee tofauti zetu lakini tubakie wamoja (let's celebrate our differences but keep our unity)..Ndipo inapoleta Upinzani kwani mimi naona kachapia.. angesema Let's keep our differences but celebrates our (in) Unity ningemwelewa vizuri zaidi..No doubt, together let's us continue build the nation and consolidate UNITY which is the pillar of our society that make us stand tall. But U have to accept being challenged 'cause we may have our differences focusing on finding solutions. The thing is, we must always share the vision of a brighter future for our country. And that's what Opposition stand for!

Wapinzani wanachopinga sio kuwepo kwa shule za kata au ongezeko la shule nchini isipokuwa mkakati huu umelenga kitu gani.. Maadam malengo ya chama sasa hivi ni kuwa na shule nyingi zaidi nchini badala ya kuhakikisha elimu bora ndio msingi wa ujenzi wa shule hizo (Quality of education) kwa nini wasipinge?.. Wewe tueleze ubora wa kuwa na shule nyingi Quantity against Quality tutapata kukuelewa kuliko kupinga Upiznani pasipo kueleza sababu zao za msingi kuwa hazina maana.

Nadhani nimekujibu vya kutosha kwa leo....
 
Mkandara ulivyosema Oman ni nchi masikini sijakuelewa. Navyojua GDP per capita ya Oman ni kubwa kuliko TZ.
Mkandara wrote "Nchi kama Oman ambazo Sultan wake alifikia kututawala sisi mbona nazo maskini"
 
Nenda kawakusanye viongozi wa upinzani halafu wahutubie maana ya upinzani basi. Hayo yote unayoyasema wapinzani wanayafanya. Jaribu kufauatilia tena na utagundua hayo. Acha kuwa na mawazo yaliyofungwa, jaribu kupanuka kidogo au vipi!!
 
mail
Mimi na hoja tu ila zipo kwenye makala yangu ............narudia tena upinzani ni zaidi ya kulalamika.............upinzani wa kweli unajali vipaumbele vya taifa sio kuendesha propaganda kila uchao.............bwana Mutu hebu jaribu kuchambua hoja zangu sio kuniuliza iwapo na hoja au la? Mimi hoja ninazo za kutosha tu lakini hebu chambua hoja zilizopo kwenye makala yangu kaka.
Bila kuwa na propaganda chama cha siasa hakiwezi kudumu. Moja ya sababu kuu za kuanzishwa chama cha siasa ni kushika dola siku moja. Sasa watafikiaje hapo? Inabidi wawe na hoja mbadala, kuumbua uozo wa serikali iliopo madarakani, kuamsha watu waelewe siasa ni ni nini ( japo hiki ni kisu chenye makali pande zote ambacho wanasiasa wengi wa Kiafrika wanakiogopa kukijenga).
Kwa hiyo siyo jukumu la upinzani kwaonyesha jinsi ya kujisahihisha japo wataibua wanapokosea. Bahati mbaya ndio ukweli wa demokrasia inavyotekelezwa vinginevyo ni ku cantonise kama wa Siwsi japo pia kuna ugumu wake, unpredictability of popular voting
 
Mkandara Umonge Hoja ya Msingi, pongezi kwako.
Nilipokua na umri kama wako (NOVA KAMBOTA) Nilibahatika kusoma shule kama yako, (St...) Nilipokua shuleni mwalimu wetu wa Civics alikua ni mjumbe wa nyumba kumi wa ccm huko anapoishi. Nakumbuka maneno yake ambayo kwa wakati ule niliyaamini, nanukuu "CCM ndio chama Tawala kwa wakti huu na kitadumu milele", alizidi kwa kusema bila ccm nchi hii haitokua na amani. Kwa wakati ule nilikua nawashangaa wapinzani hasa wa CUF kwa kudiriki kuandamana kiasi cha kupigwa mabomu na virungu. Baada ya kumaliza elimu yangu na kuingia mtaani. mambo ambayo nimeyakuta hasa mikoani nikiwa katika biashara zangu ndogondogo za ujasilia mali nimejifunza mengi. turidi kwenye mada.
Ndugu yangu Nova hiyo CCM ambayo wewe unayoitetea imetokana na vyama vilivyokua vya upinzani dhidi ya ukoloni. kama kusingekua na vyama vya upinzani ambavyo vingeipinga serekali ya ukoloni leo hii tungekua bado tuna lima kwenye mashamba ya wazungu.
Pili usitegemee Kwa kuitete CCM labda utaonekana mtu wa maana, la hasha unadhalilisha usomi wako. Wanachama wengi na makada wa ccm wanajulikana kwa level yao ya elimu ya Darasa la saba pamoja na kukosa utu achana nao unapoteza a kudhalilisha utu wako. am so sorry abt your mom but hizo ni sera mbovu za afya, pamoja na social securities ambazo zimewekwa na serekali yako. Zinduka na Uamke kijana wewe ni tegemeo kwa taifa hili sitaki kukupoteza mnamo 31 oct kwani kura yako inahitajika kuleta ukombozi kwa taifa letu na familia yako kwa ujumla. Najua utaniambi kua sina hoja kwani ndio respond yako.
 
mail
Umaskini mkubwa unaotutafuna watanzania ni kuwa na upeo finyu(narrow mind) hili ni tatizo kubwa sana lingine ni kufata mkumbo na kushabikia bila kutafakari................narudia kusema tena upinzani wa Tanzania umejikita katika propaganda zaidi sio hoja ifike mahali wapinzani wanapawsa wajue kuwa hata nyuki ni mkali ila mwisho wa siku mwanadamu anarina asali mi naona ni heri watafakari kwa kina ushauri wangu wa bure niliowapa kuliko kutoa majibu mepesi kwa hoja nzito............kimsingi hoja zangu zimejikita kwenye utaifa, kupanua demokrasia nchini na kutoa elimu ya uraia.........mshangao naoupata ni kuwa wanaonijibu wanajibu hoja za kitaifa kwa misingi ya kisiasa na kwa ushabiki wa vyama vyao haitoshi hoja zao zimejikita katika ushabiki kuliko mantiki............hili ni tatizo kubwa kwa maana inapaswa kupangua hoja zilizoko kwenye makala yangu sio kuanika hisia zako za kisiasa.
 
Back
Top Bottom