Wewe Askari Uliyezimikiwa Pikipiki Barabarani Punguza Ubabe

Faana

JF-Expert Member
Dec 12, 2011
31,920
33,353
Ujumbe huu ni kwa wewe askari uliyezimikiwa bodaboda yako mchana maeneo ya 88 Gloness Morogoro leo mchana, ulijua kabisa chombo chako hakina mafuta ya kutosha still ukaingia nacho barabarani, kimekatikiwa mafuta ukagandisha nacho barabarani ati hata wenye magari wakupishe, baada ya honi kuzidi ukashuka na kuanza kusukuma kisha ukakidandia na kuserereka nacho kuelekea kituo cha mafuta.

Sawa hukutaka kuumbuka lakini hukutumia busara, umefika kituo cha mafuta ukawataka wakuwekee mafuta, wakakuwekea baadaye ukajipapasa mfukoni ukashtuka kama vile umeibiwa pesa, ukataka kuondoka ati wauzaji wasubiri ukawachukulie fedha kama vile wanakujua.

Lakini bahati nzuri wauzaji wa mafuta walikukomalia ukabakisha chombo kijidhamini wewe ukaenda pembeni kuwapigia jamaa zako wakutumie fedha ili ukomboe chombo pale petrol station, nashauri askari unapokua umekwama tumia busara badala ya ubabe ujuaji na nguvu ili kulinda heshima yako na jeshi lako.
 
sawa, ila yalikuwa hayakuhusu...
kama ulikuwa kwenye gari uakapata upenho ungepita hivi.. umefatilia mtu hadi sheli isitoshe ni jambo la kawaida sana kuishiwa mafuta sababu inawezekama chombo sio chake au chake lakini alimpa mtu hakuwa muambinifu na route alizoenda so ikatokea anajua mafuta yapo ila empty... Unamfungulia mtu uzi utadhania kajamba kwenye maji, Wabongo tupunguze uswahili.!
 
Bila shaka wewe unafanya kazi kwenye hicho kituo cha mafuta,ndio maana umeijua mpaka story ya kilichotokea hapo kwenye hicho kituo.
 
habari umezipataje kama sio upuuzi na kukosa kazi kuacha mambo yako na kufatilia mambo ya watu.. wangetakiwa wapost wafanyakai wa kituo cha mafuta.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom