We flash back: JK ziarani Mbeya

Lunyungu

JF-Expert Member
Aug 7, 2006
8,873
1,894
Najua wengine mtashangaa kwa nini Lunyungu anarudi nyuma lakini ni katika kuweka rekodi sawa .Ziara ya Kiongozi mkuu huyu iligubikwa na matukio mengi sana .Lakini TV yao yaani TBC walijitahidi sana pamoja na Uhuru kuweka sura ambayo si sura yake .Mbeya ilikuwa ngumu .Ilimfanya JK aanze kujibu hoja za JF akiwa Mbeya .Kumbe hawakumweleza ukweli kwamba watu wa Mbeya hawakuwa na beef naye kwa ajili ya Mwandosya bali ni watu wanao taka maendeleo lakini hawako na hawakuwa tayari kuimba wimbo wao wana CCM wa kusema Maisha bora .

Waliamua kuhoji kwa matendo na sauti pia na ndiyo maana JK alipata kushindwa mara kadhaa kusema na wananchi na badala yake akawa anawaita viongozi wa wilaya kataka na tarafa na kusema nao .Alipata bahati ya mkutano mmoja akiwa Mbeya lakini hakuweza tena kuipata bahati ile hadi anamaliza ziara .

Mawe yakarushwa na wananchi kuziba njia akidhani wana hamu naye kumbe walitaka kuona ahadi zake ziko wapi .Kwa mfano Tunduma hakuweza kufika maana hali ilikuwa mbaya na Mbeya mjini ilibidi awe na mikutano ya ndani pekee maana kwingineko anajua moto ulivyo kuwa .

JK ameanza kuamka na kujua kwamba U rais si lele mama na watanzania wamechoka na longo longo na wanataka ahadi za ukweli ?

Wote mnajua yaliyo jiri Mbeya sasa tuendelee kuangalia ilikuwaje ili tumsaidie kumweleza kwamba CCM haitakiwi tena .
 
Naomba mkishamaliza habari za hapa Dodoma turudi Mbyea kuona halisi
 
Najua wengine mtashangaa kwa nini Lunyungu anarudi nyuma lakini ni katika kuweka rekodi sawa .Ziara ya Kiongozi mkuu huyu iligubikwa na matukio mengi sana .Lakini TV yao yaani TBC walijitahidi sana pamoja na Uhuru kuweka sura ambayo si sura yake .Mbeya ilikuwa ngumu .Ilimfanya JK aanze kujibu hoja za JF akiwa Mbeya .Kumbe hawakumweleza ukweli kwamba watu wa Mbeya hawakuwa na beef naye kwa ajili ya Mwandosya bali ni watu wanao taka maendeleo lakini hawako na hawakuwa tayari kuimba wimbo wao wana CCM wa kusema Maisha bora .

Waliamua kuhoji kwa matendo na sauti pia na ndiyo maana JK alipata kushindwa mara kadhaa kusema na wananchi na badala yake akawa anawaita viongozi wa wilaya kataka na tarafa na kusema nao .Alipata bahati ya mkutano mmoja akiwa Mbeya lakini hakuweza tena kuipata bahati ile hadi anamaliza ziara .

Mawe yakarushwa na wananchi kuziba njia akidhani wana hamu naye kumbe walitaka kuona ahadi zake ziko wapi .Kwa mfano Tunduma hakuweza kufika maana hali ilikuwa mbaya na Mbeya mjini ilibidi awe na mikutano ya ndani pekee maana kwingineko anajua moto ulivyo kuwa .

JK ameanza kuamka na kujua kwamba U rais si lele mama na watanzania wamechoka na longo longo na wanataka ahadi za ukweli ?

Wote mnajua yaliyo jiri Mbeya sasa tuendelee kuangalia ilikuwaje ili tumsaidie kumweleza kwamba CCM haitakiwi tena .
Huo ni uzushi ziara ya JK Mbeya alikuwa ni nzuri sehemu zote alizotembele wananchi walifurika si mjini hata vijijini.Kwa tukio la mbeya wale aliozoza ni wapiga debe ambao hata wewe ukipita na gari zuri eneo la mwanjelwa utaitwa fisadi.Kuhusu kijiji cha kanga wananchi wa huko wanaandaa maandamano ya kulaani kitendo hicho.Vizuri kuongea ukweli hana kama humpendi JK.Kumbuka uzushi uongo ni dhambi.
 
Well. There is so much to write about this. The debate has been whether wananchi were so much eager to see him (as he claimed) or whether they really meant what they did. Kama kutupa mawe si kweli, basi nafikiri hakukuwa na haja ya JK kuagiza uchunguzi ufanyike kuhusu hilo tukio. Hata kama sio msafara wake (msafara mkuu) uliorushiwa mawe, bado kuna kila hali ya kuamini kwamba hawa wananchi hawakuwa na furaha na raisi wao. Hili ni tukio la kipekee katika historia ya nchi na dalili kwamba wananchi wamechoka na serikali nzima ya JK. Hilo jingine la kuzomewa huko Mbeya pamoja na Tabora juzi, ni muendelezo wa wananchi kuonyesha hasira na kutoridhishwa na jinsi serikali ya JK inavyoendesha nchi.
 
Well. There is so much to write about this. The debate has been whether wananchi were so much eager to see him (as he claimed) or whether they really meant what they did. Kama kutupa mawe si kweli, basi nafikiri hakukuwa na haja ya JK kuagiza uchunguzi ufanyike kuhusu hilo tukio. Hata kama sio msafara wake (msafara mkuu) uliorushiwa mawe, bado kuna kila hali ya kuamini kwamba hawa wananchi hawakuwa na furaha na raisi wao. Hili ni tukio la kipekee katika historia ya nchi na dalili kwamba wananchi wamechoka na serikali nzima ya JK. Hilo jingine la kuzomewa huko Mbeya pamoja na Tabora juzi, ni muendelezo wa wananchi kuonyesha hasira na kutoridhishwa na jinsi serikali ya JK inavyoendesha nchi.

Wakuu hilo la kuzomewa Tabora mbona sikulidakuwa vyema? nipeni link wakuu lilipo dadavuliwa vyema! Ilikuwaje hadi huko zahma ikamfika? duu.. Tz ya sasa si ya 47! habari nene hiii
 
ziara imekwisha FLASHBACK YA NINI?

WA MBEYA kwa umbeya ni wenyewe tena unafanywa na wasomi?kumbe si lolote si chochote.baada ya kushindwa kuendeleza mkoa. wanawajaza wananchi kwa majungu kwananchi kwa majungu.
 
wa mbeya kwa umbeya ni wenyewe tena unafanywa na wasomi?kumbe si lolote si chochote.baada ya kushindwa kuendeleza mkoa. Wanawajaza wananchi kwa majungu kwananchi kwa majungu.

ama kweli kua oyaone;

kama kuna mtanzania anaweza kusema mbeya wameshindwa kuendeleza mkoa wao, basi haijui tanzania kabisa: Kwa mtanzania yeyote aliyetembelea nchi yake atakubali kwamba mbeya iko juu, nimetembea mikoa 19 na karibu wilaya zote ZA MIKOA HIYO - wenzetu mbeya wamewahi, angalia maisha yao, infrastructure, shule na hospitali na vituo vya afya, mifugo, mashamba, watoto wa shule wakiwa na basic needs (si midabwada na araiyoo) hata chakula kipo; bwana saidsabke badili kauli yako - kama huijui tanzania jifunze na sio kuangalia atlas na magazeti

kwa kuongeza tu, kila kwenye upinzani utakuta level ya community development ni kubwa na upeo wa kuamua ni mkubwa; naridua tena, futa usemi huo kwa si wa kiungwana
 
Kama kuna wakati mgumu katika maisha yake ya Urais ulimkumba JK basi ni Mbeye majuzi .It was so hard kiasi kwamba hata mikutano aliifanyia ndani kwa kuongea na viongozi wa kata, Wilaya na mikoa .Mbeya was hard just like tarime na yeye anajua hili kwa uwazi kabisa .Ukisema alishangiliwa then naamini kwamba wana JF tunasema kwa kuwa tu tuna kaa Ulaya na US ama ugenini na hai halisi hapa nyumbani hatuijui ila sisi wa hapa tunajua kinacho endelea regardless magazeti kuacha kuandika ukweli .JK na Mbeya hawapendani .
 
Kama kuna wakati mgumu katika maisha yake ya Urais ulimkumba JK basi ni Mbeye majuzi .It was so hard kiasi kwamba hata mikutano aliifanyia ndani kwa kuongea na viongozi wa kata, Wilaya na mikoa .Mbeya was hard just like tarime na yeye anajua hili kwa uwazi kabisa .Ukisema alishangiliwa then naamini kwamba wana JF tunasema kwa kuwa tu tuna kaa Ulaya na US ama ugenini na hai halisi hapa nyumbani hatuijui ila sisi wa hapa tunajua kinacho endelea regardless magazeti kuacha kuandika ukweli .JK na Mbeya hawapendani .
:D lugha tatizo kwako
Kamanda punguza kupika majungu...
 
Una ushahidi gani kama huo ulikuwa ndio wakati wake mgumu hadi sasa? Yaliyotokea huko Mbeya kwake yanaweza kuwa ni changamoto ya kujua hali halisi na kuuona ukweli wa mambo, zaidi ya kuwa ni wakati mgumu!

Kumbuka kuwa hata mara moja hakuwakimbia wananchi hao, zaidi ya kuongea nao pasipo jazba ya aina yoyote... Huo wakati mgumu unaosema wewe ni upi hasa?

Anyway vipi Mbeya wanasemaje huko? Au wikiendi hii upo Dom?
 
Una ushahidi gani kama huo ulikuwa ndio wakati wake mgumu hadi sasa? Yaliyotokea huko Mbeya kwake yanaweza kuwa ni changamoto ya kujua hali halisi na kuuona ukweli wa mambo, zaidi ya kuwa ni wakati mgumu!

Kumbuka kuwa hata mara moja hakuwakimbia wananchi hao, zaidi ya kuongea nao pasipo jazba ya aina yoyote... Huo wakati mgumu unaosema wewe ni upi hasa?

Anyway vipi Mbeya wanasemaje huko? Au wikiendi hii upo Dom?

Kibunango niko hapa Dear Mama Hotel mjini Dodoma na nimeleta issue ya Mbeya sikusema niko Mbeya bali nimeandika we flash back maana maisha ni historia .Wakati mgumu niusemao ni ule wa yeye kushindwa kusimama jukwaani na kusema na watendaji na viongozi indoors badala ya kuwa majukwaani kama ilivyo kuwa inapangwa ama kuhamishwa kwa majukwaa ya mara kwa mara kwenda mbali zaidi wakidai ni sababu za usalama .Sasa unataka kubisha lipi hapa ? Huu si wakati mgumu ?Lakini anywa CCM bwana mna mambo ya ajabu maana hata Tarime Makamba alimwambia Kingunge kwamba ushindi ulikuwa asilimia 100 lakini kwa kuwa Kingunge hakumwamini aliamua kumpigia simu Wasira kuujua ukweli na Wasira alimpa LIVE kwamba Tarime CCM ilikuwa inashindwa kwa mbaaali na kwamba kama wangalishinda basi walipaswa kuua watu wote Tarime.No wonder unakataa na ukweli huu maana CCM wanaweza kushindana hata na jiwe walidhani wanaweza kupigana vichwa na jiwe .
 
Back
Top Bottom