Wazo Yakanifu: Thamani ya Lowassa Upinzani imeshuka mno, ni wakati wa Kustaafu tu!

Mzee Mwanakijiji

Platinum Member
Mar 10, 2006
33,478
40,000
lowassa1.jpg

Tangu jina lake likatwe na chama chake - kama baadhi yetu tulivyotamani - thamani ya kisiasa (political value) ya uamuzi wowote wa Lowassa sasa imeshuka kupita kiasi. Kwa vile imechukua muda sana kwake kufanya uamuzi wenye maana wenye kuendana na thamani yake ni wazi sasa hata akichukua uamuzi wowote ule hautakuwa na matokeo yale makubwa ambayo wengine tuliyategemea na ambayo yangesaidia katika jitihada ya kuing'oa CCM kutoka madarakani. Kuna mambo kadhaa ya kusema hapa:

1. Lowassa baada ya kukatwa jina lake alitakiwa kujitoa wakati ule ule kabla ya kura za NEC na Mkutano Mkuu. Sijui ni nani walikuwa washauri wake lakini kipindi cha yeye kukatwa na kabla ya mkutano wa NEC thamani yake kisiasa kwa CCM na hata nje ya CCM ilikuwa haishikiki wala kukamatika; iliendana kabisa na idadi ya watu waliokuwa wanamuunga mkono kwenye udhamini. KUshindwa kwake kufanya uamuzi wa lazima ambao rafiki zake walimtengenezea daraja la kupitia kumethibitisha kile ambacho wengine tumekuwa tukikisema kuwa si mtu wa maamuzi sahihi au ya lazima. Aliamua kufanya uamuzi mgumu; kubakia ndani ya CCM.

2. Lowassa amewaangusha watu waliomtengenezea daraja la kupitia kwenda chama kingine (isipokuwa Chadema - rejea mada yangu nyingine kwa hili). Emmanuel Nchimbi, Adam Kimbisa na Sofia Simba waliamua kumtengenezea daraja na nadhani ilikuwa ni sehemu ya makubaliano ya awali ili yeye afuatie na kusema kuwa na yeye hakubaliani na maamuzi ya kamati kuu na hivyo ameamua kurudisha kadi ya CCM na kujitoa akifikiria hatua inavyofuatia. Uamuzi huu ungetosha kabisa kuipasua CCM na vikao vilivyokuwa vimebakia.

3. Bahati mbaya Lowassa alijikuta anaburudishwa na ule wimbo wa "tuna imani na Lowassa" lakini alishindwa kutumia clout (ujiko) ule ipasavyo. Alisimama kama swala aliyepigwa na mwanga wa gari barabarani. Hakujua afanye nini.

4. Hata baada ya kura za NEC - chombo ambacho kingeweza kusahihisha maamuzi ya Kamati Kuu (NEC ni chombo cha juu ya CC) Lowassa hakuoneakana kutaka kupigania nafasi yake na badala yake akala 'kobisi' na kuvumilia hadi Mkutano Mkuu ambako nako akaburudishwa na kushangiliwa jina lake lilipotajwa na Da' Amina Ali. Alishindwa kufanya uamuzi wa lazima na uamuzi sahihi. Aliamua kufanya uamuzi mgumu wa kubakia na watu waliomsaliti, kumtupa na kumgeuka.

5. Sasa hivi hata baada ya Mkutano Mkuu watu wengine walitarajia angefanya ule uamuzi japo thamani ilikuwa inazidi kushuka lakini hakufanya hivyo. Matokeo yake hata kina "Msukuma" ambao waliapa ati wanaenda naye nchi ya ahadhi liwalo na liwe wote wakageuka na kuanza kuimba nyimbo za Magufuli. Hata Nchimbi ambaye alisimama kupinga maamuzi ya Kamati Kuu - hili sikumbuki kutokea tangu CCM ianzishwe - naye amegeuka na kusema ati Magufuli ndiye mgombea sahihi - kana kwamba alikuwa hajui kabla. KUshindwa kwake kufanya uamuzi huu wakati muafaka na sasa ati anajadiliana na familia na wadau wengine inashangaza na kuchekesha. Hivi hawa watu walikuwa hawajakaa na kufikiria "the worst case scenario"? Unaweza vipi kupanga harakati au jambo lolote lile muhimu bila kufikiria mambo yakienda vibaya kabisa utafanya nini?

Ni kwa sababu hiyo hata kumfikiria ati kuna watu wanataka aende upinzani sasa sijui kama itakuwa na matokeo kama angeamua kwenda kabla ya Kura za NEC na Mkutano Mkuu. Sijui kama thamani yake kisiasa bado ipo kivile tena na sidhani hata wale wadhamini karibu milioni wanamtaka sasa hasa kama anataka kupambanishwa na Magufuli. Kama kuna kiongozi yeyote wa upinzani au chama kinamfikiria kuwa anathamani ile aliyokuwa nayo kabla naomba niwape taarifa mbaya - hana tena. Ni sawasawa na kutaka kununua tiketi ya Mayweather na Pacquiao baada ya pambano; ni sawasawa na kutaka uende mpirani kuangalia mechi ya MaNU dhidi ya Chelsea wakati watu wanatoka uwanjani kipenga cha mwisho kishalia. Sidhani wale wana CCM wapenda madaraka na wafuata upepo leo watakuwa tayari kumfuata "kokote atakakokwenda". Hata wale Wachungaji waliomba "Pamoja na wewe" sidhani kama akiwaita leo nyumbani wataimba tena vile; labda wataimba "Tulimwambia Lowassa Bai Bai"!

Ushauri wangu wa kiutu tu ni kuwa uamuzi sahihi sasa kwa Lowassa ni kustaafu siasa kabisa na kwenda kupumzika. Mihemko ambayo ameipata miaka hii tangu kujiuzulu inamtosha kabisa katika maisha na sidhani ana sababu nyingine yoyote - iwe ya kisasi au vinginevyo - ya kujiingiza siasa za Tanzania. Kama akitaka zaidi kuonesha kutofurahishwa na CCM yake anaweza kujiunga na chama kimoja cha upinzani kama mwanachama wa kawaida tu na kuwasaidia kukiondoa chama kilicho mlea. Kwani CCM siyo mamake! Ingekuwa mamake au hata umbu yake kisingemgeuka hivyo.

Nimpe pole tu kuwa hizi nazo ni 'ajali za kisiasa' hata kama nyingine zinasababishwa na watu kwa makusudi. UKAWA - iwe mtu mmoja au timu nzima - wakifiria kuwa Lowassa ana thamani aliyokuwa nayo baada ya jina kukatwa na kabla ya vikao vya NEC na Mkutano Mkuu watakuwa wanajidanganya. Wamuache mzee wa watu apumzike. Ila kama kuna chama cha upinzani kinafikiria kinaweza kumtumia Lowassa vizuri kama mgombea wake wajaribu; sidhani kama kuna kundi kubwa CCM litamfuata kama nilivyofikiria mwanzoni. Wale wote waliokuwa wanamuunga mkono tangu ajiuzulu wengi walikuwa wamepigia mahesabu yeye kuwa mgombea wa Urais kwa CCM. Hili halitatokea sasa hivi isipokuwa kwa njia nje ya za kibinadamu.

MMM
 
Point..mkuu...mie pia HOFU yangu ilikua siku ile Nchimbi anapinga yale maamuzi..nikajua anafuata yy..kisha wanaondoka dodoma..angefanya hivyo saa hz tunaongea mengine
 
Lowasa amewaangusha watu wengi sana waliompata imani na itamgharim sana kuelleweka kwa watu wake kwamba kwanin haonyeshi ushirikiano wakati wao wanampa support.
 
Kwa mtizamo wangu hata kabla Lowasa hakuwa na hiyo thamani, wengi tuliowaona ni waliomuunga mkono tena kwa kupewa pesa, wale wanaompinga muda wao wa kumpinga ulikuwa haujafika na ndo mngeona hali halisi ya wanaomuunga mkono na wanaompinga. Lowasa hakuwa na sifa hata kabla bali yalikuwa ni maigizo tu kama ya kina James Bond.
 
walijipanga ki ela hawakujipanga kimkakati na walidanganywa na tafiti za magazeti na taasisi mbalimbali kuwa lowassa anakubalika ndani na nje ya ccm wakatumia nguvu nyingi kumtoa membe badala ya kufikilia kuwingiza lowassa kwa kupingana na maamuzi ya Cc kwani nchimbi na sophia walikuwa wamesha tengeneza njia wakati kikwete anaingia kwenye mkutano wangeimba tu mkutano ungevunjika na wakapata nafasi ya kujipanga kwa plan B kwani walikuwa na plan A tu lowassa straight to state house bt awakujua kuwa mpaka lowassa afike ikulu kuna mchakato mkubwa na kama wakashindwa plan A plan B ni nini? lowassa ni kama gari sasa kila mda zinavyokwenda linashuka thamani unaweza kulinunia million 100 ukaja ukaliuza million 1 wafwasi wake now wako busy kujipendeza kwa magufuli now sasa kumeshapambazuka aitaji taa kuwaona walikuwa na yeye kwa mapenzi ya kweli au kwa kumchuna pesa zake
 
Kweli Mm Lowasa amekuwa ni wa maamuzi mepesi na si magumu tena kama alivyokuwa akijitanabaisha! Yeye na kundi lake hawajui kucheza kwa timing!
 
Strategy aliyoitumia ya kununua watu ili aonekane anapendwa ilikuwa ya kitoto. Siamini alipendwa kiasi hicho cha watu kuweka future yao kwake kufa na kupona. Alizungukwa na wachumia tumbo ambao kwa makusudi walijidanganya au kumdanganya yeye kuwa bila yeye hakuna CCM.
 
Mikakati yake ya kuusaka urais ilitosha kumtisha kila mwenye kufikiri. Ukiacha wale waliopofushwa na uchu wa kutafuta madaraka, hakuna mtu aliyetumaini kama Lowassa angekuwa rais Tanzania ingekuwa na neema. wengi tunashukuru hili limetokea
 
Afya na umri pia vinaweza kuongezea katika sababu muhimu za kumfanya apumzike kisiasa, lakini bado tunahitaji michango yake kwenye vikundi vya kijamii, kanisani, kwenye kwaya, misikitini, vikundi vya bodaboda nk, tunamuomba sana aendelee na moyo huo huo wa kujitolea
 
Bado LOWASSA na wenzie na hasa kina Nchimbi na wenzie, Tanzania isingempata huyu mgombea ambaye kikweli tunasatahili kumpata kama Rais wetu!

Kilichopo kwa sasa tuachane na habari hizi za Lowasa, kwakuwa haziisaidii sana nchi kwa sasa, na tujielekeze tujadili changamoto zinazoikumba nchi yetu, vipaumbele vyake na njia za kuzitatua!
 
Ni wakati sahihi kabisa wa lowassa kutundika daruga for good....watu wake wamekosa matumaini kutokana na boss wao kukosa uelekeo...kondoo wake wamemkimbia na sasa wamerudi kumsapoti Magufuli wakiamini ndio mbadala sahihi wa Lowasa.
Kinachonishangaza tu ni watu wa Lowassa kufurahia uteuzi wa Magufuli na kukosa kwa Membe.
Kwa hili nampongeza sana Rais Kikwete kwani kafanya siasa ya hali ya juu.
 
Kaka uko sahihi kabisa huo ni ukweli,huyu mtu apumzike tu hawezi kurudisha status yake ya awali,hao wakina nchimbi walikuwa kimaslahi na chuki ya kuwajibika ktk nafasi zao za uwaziri,ndiyo maana walionekana tibaijuka,karamagi,na baadhi ambao walihusishwa na kashfa na wasio na subira wakiegemea kwa lowasa wakiamini atapita tu,siku zote mwenyekiti wa taifa kwa chama tawala ana nguvu kubwa,maana ana kura yake,ikumbukwe ni mwenyekiti na ni rais,sijui vikao vya majungu au vya kumzunguka utavifanyia wapi asikubane,ndiyo maana mzee mwandosya aliomba kabla ya kufanya uchaguzi wa nafasi ya urais,wafanye uchaguzi wa mwenyekiti taifa,ili atleast watu wajue mwelekeo wake
 
Mamvi kwisha habari yake...wafuasi wake wamemkimbia mchana kweupee tena wanasema magufuli ni chaguo sahihi so inamaana walijua Edo hafai but wakakomaa na pesa yake...
Nakumbuka maandishi ya Pasco wa jf alikuwa anasema mwaka huu ni mwaka wa mavuno..nakweli wafuasi wa edo na mtama mmezivuna kama hamjajenga hata vibanda vya kuishi basi hamjakosa za kusomeshea watoto st accademia school hongereni kwakweli..
 
Uvumi huu wa EL kuhamia CHADEMA, UKAWA au ACT umeshika kasi na sasa unaelekea kuaminika. Sina hakika kama wenye vyama hivi wako comfortable na wazo hili au vinginevyo. Nashauri secretariats za vyama hivi kwa pamoja au kipekee waite press conference watoe msimamo. Kama EL anawafaa kweli hebu semeni basi,come out real ili msiendelee kumtesa kisaikolojia mzee wa watu. Kwani kuna wanaoamini kuwa EL kayakubali matokeo ya CHAMA KUBWA na anajiaanda kutoa tamko kupitia Press conference ku-declare support yake kwa Pombe Magufuli na CCM, jambo ambalo mimi naamini ndio la busara zaidi. Urais unatoka kwa Mungu na wala sio CCM, UKAWA wala ACT. Hey! Viongozi upinzani semeni neno juu ya jambo hili na kama ni kweli mtampokea, mtusaidie kuelewa ni kwa namna gani uwepo wake kwenye vyama vyenu hakuta athiri "Brand" yenu ya Uadidilifu mnayoilinda kwa nguvu zote.
 
Lowasa ni kweli ni tishio kwa CCM, kama hajitaki afanye kosa la kuhamia upinzani kama CCM hawatamkolimba ndani ya wiki moja...
 
Lowassa sio super natural. Guys ongeeni mambo ya msingi ya nchi, nchi ina watu milioni 45! . Huyo aliechaguliwa is even better 10 times thst that old man, so why waste your times guys!
 
Back
Top Bottom