Date::1/31/2009
Chadiel Mgonja afariki
Fredy Azzah
ALIYEKUWA Waziri katika serikali ya awamu ya kwanza, Chediel Mgonja, atazikwa siku ya Jumanne Kijijini kwake Vudee, Wilaya ya Same, Mkoa wa Kilimanjaro.
Watu mbalimbali watapata fursa ya kutoa heshima zao za mwisho kesho kuanzia saa 6 mpaka saa 8 mchana, nyumbani kwa shemeji wa marehemu Ibrahim Kaduma, Makongo Juu.
Akizungumza na gazeti hili jana, Ibrahim Kaduma ambaye ni shemeji wa marehemu, alisema shughuli zote za mazishi ya Mgonja zitafanyika nyumbani kwake, na kwamba, marehemu Chediel Mgonja ameacha mjane mmoja na watoto 10 na wajukuu 13.
Alisema kuwa marehemu ambaye alizaliwa Desemba 31, mwaka 1934, alikuwa akisumbuliwa kwa muda mrefu na ugonjwa wa kisukari, lakini hali ilikuwa mbaya zaidi ilipofika Desemba 13 mwaka jana.
"Marehemu alikuwa akisumbuliwa na presha pamoja na kisukari toka siku nyingi. Lakini hali ilikuwa mbaya zaidi tarehe 13, Desemba na tulimpeleka katika Hospitali ya Lugalo, alipolazwa hadi mauti ilipomfika jana (juzi) saa 10 alasiri," alisema Kaduma.
Alisema mjane Liliani Mgonja yuko Same, kijijini Vudee ambapo marehemu alikuwa akiishi na familia yake, na kwamba watoto wawili wa marehemu wako nje ya nchi, lakini wametoa ridhaa shughuli za mazishi ziendelee.
Marehemu Mgonja aliongoza wizara mbalimbali katika serikali ya awamu ya kwanza, ambapo pia kwa nyakati tofauti aliwahi kuwa Mkuu wa Mkoa wa Mtwara na Mkoa wa Tabora. Aliingia kwenye siasa mwaka 1965, akiwa Mbunge wa Same na mwaka huo huo akateuliwa kuwa Waziri wa Utamaduni, Siasa na Michezo.
Mwaka 1966 alikuwa Waziri katika Ofisi ya Rais na Mambo ya Nje na pia mwaka 1968 alikuwa Waziri wa Elimu. Mgonja alikuwa kwenye Siasa mpaka mwaka 1995, ambapo kwa wakati wote alikuwa akiliwakilisha Jimbo la Same.
Source: Mwananchi
Chadiel Mgonja afariki
Fredy Azzah
ALIYEKUWA Waziri katika serikali ya awamu ya kwanza, Chediel Mgonja, atazikwa siku ya Jumanne Kijijini kwake Vudee, Wilaya ya Same, Mkoa wa Kilimanjaro.
Watu mbalimbali watapata fursa ya kutoa heshima zao za mwisho kesho kuanzia saa 6 mpaka saa 8 mchana, nyumbani kwa shemeji wa marehemu Ibrahim Kaduma, Makongo Juu.
Akizungumza na gazeti hili jana, Ibrahim Kaduma ambaye ni shemeji wa marehemu, alisema shughuli zote za mazishi ya Mgonja zitafanyika nyumbani kwake, na kwamba, marehemu Chediel Mgonja ameacha mjane mmoja na watoto 10 na wajukuu 13.
Alisema kuwa marehemu ambaye alizaliwa Desemba 31, mwaka 1934, alikuwa akisumbuliwa kwa muda mrefu na ugonjwa wa kisukari, lakini hali ilikuwa mbaya zaidi ilipofika Desemba 13 mwaka jana.
"Marehemu alikuwa akisumbuliwa na presha pamoja na kisukari toka siku nyingi. Lakini hali ilikuwa mbaya zaidi tarehe 13, Desemba na tulimpeleka katika Hospitali ya Lugalo, alipolazwa hadi mauti ilipomfika jana (juzi) saa 10 alasiri," alisema Kaduma.
Alisema mjane Liliani Mgonja yuko Same, kijijini Vudee ambapo marehemu alikuwa akiishi na familia yake, na kwamba watoto wawili wa marehemu wako nje ya nchi, lakini wametoa ridhaa shughuli za mazishi ziendelee.
Marehemu Mgonja aliongoza wizara mbalimbali katika serikali ya awamu ya kwanza, ambapo pia kwa nyakati tofauti aliwahi kuwa Mkuu wa Mkoa wa Mtwara na Mkoa wa Tabora. Aliingia kwenye siasa mwaka 1965, akiwa Mbunge wa Same na mwaka huo huo akateuliwa kuwa Waziri wa Utamaduni, Siasa na Michezo.
Mwaka 1966 alikuwa Waziri katika Ofisi ya Rais na Mambo ya Nje na pia mwaka 1968 alikuwa Waziri wa Elimu. Mgonja alikuwa kwenye Siasa mpaka mwaka 1995, ambapo kwa wakati wote alikuwa akiliwakilisha Jimbo la Same.
Source: Mwananchi
Last edited by a moderator: