Waziri wa Mambo ya Ndani, Mwigulu Nchemba: Naagiza aliyemtolea bastola Nape Nnauye, achukuliwe hatua

Nchemba hapo kama unajiosha tu.

Isiishie kwa kuwaagiza polisi, inatakiwa uwape masaa wakuletee ripoti, huyo ni nani na kwanini alifanya vile na kama ni askari nani alimpa amri ile, chain of command iliyofanya yale ijulikane, tuone hiyo chain ya command kama ilianzia tokea kwako au ilianzia kati kati.

Bila kufanya hivyo basi wewe ni Waziri husika wa usalama wetu na inabidi ufanye wajibu wako ili tuelewe kuwa na wewe huhusiki kwa Nape kuwa harassed namna ile.

Nnawaza tu, ikiwa mtu kama Nape anafanyiwa vile, sisi wenzangu na mie si tupo mashakani.

Mbwa wa polisi hakamati mtu bila ya kupewa amri, hali kadhalika kwa polisi mwenyewe kama ni polisi.

Tunataka mizizi ya huo ujinga ing'oke.

You can do much better than that kama hautaki nafsi yako ikusute. Otherwise utakuwa ni mnafik tu.
Umenena yaliyo ya haki, Yeye kama Waziri anapaswa kwenda mbali zaidi hayo maagizo aliyoyatoa. Haiwezekani mtu unaulizwa kitambulisho unatoa bastola unarudi nyuma kulenga shabaha!! Hili limetuhuzunisha wengi maana kama Nape ambaye karibu kila mtanzania anamfahamu anatendewe vile, je wananchi wa kawaida wana hali gani kutoka kwa vyombo hivi vya usalama?? Kimsingi, Yule mtu anatakiwa kupekekwa mahakamani kwa kutishia kuua. Najiuliza, hivi tangu lini bastola ikawa ni kitambulisho cha askari au mwana usalama??? Kwa nijuavyo mimi hata majambazi wana bastola, sasa sijui Yule bwana tumuweke kundi lipi kati ya ujambazi na uaskari!!?
Kwa ujumla ni tukio lililoleta udhia kwa watu wengi, na tumejeruhiwa nyoyo zetu
 
Kazi waliyoifanya Mwigulu, January, Nape na Kinana kuhakikisha Magufuli anashinda Urais, hata Magufuli mwenyewe asingeiweza.

Kiserikali Nape keshaenda na maji, bado watatu, atakaefuatia ni Mwigulu (endapo atang'ang'ania kufanya kazi kwa uadilifu kama Nape) Kama wale wahuni wa bastola walitumwa na RC (very probable) basi uadilifu na uwajibikaji wa Mwigulu (The potential future President) utamfukuzisha kazi. January mjanja sana, utadhania hayupo vile.

Finally Kinana will go down the drain, in a way. Hiyo ndio characteristic ya madikteta wote duniani, hawawaamini waliowasaidia kuingia madarakani, wanawaona ni threat kwao.

Wanawaamini zaidi puppets wao kama vile Makonda ambaye wakati wa uchaguzi mkuu akiwa DC wa Kinondoni alikuwa dhaifu mno kiasi cha kupoteza majimbo yote ya wilaya yake!
 
Utawala wa sheria umewekwa kapuni.....huyo askari alikua anacheza tu muziki unaopigwa na utawala wetu....
Kuna matukio mengi tu yanaashiria sheria kutofuatwa:
  1. Mkuu wa mkoa kuvamia studio, na Mh. Rais kutokemea, in fact ni kama alimpongeza
  2. Mhe. Rais aliamuru kufunguliwa matairi kwa vyombo vya moto vikiukavyo sheria ya usalama barabarani
  3. Dhamana ya Mhe. Lema
  4. Kufutwa mikutano ya hadhara kwa vyama vya siasa...nk
 
Mnataka kumtumbua Askari mtu mdogo kabisa mnaacha aliyesababisha yote haya yaani Bashite!.
Mwigulu you can't have it both ways, either umwagize IGP amkamate Bashite kwa kuvamia clouds hapo ndiyo umkamate na huyu Askari, otherwise jiuzulu tu mheshimiwa kwa sababu utakuwa unatenda kwa kubagua
 
...leo umelitolea tamko hili la Nape...je lile la bashite kuvamia clouds mbona ulikaa kimya?hizi double standards Mwigulu zitawamaliza na kuwarudi nyie wenyewe...

....btw ....mnamtafuta aliyetoa bastola mnasahau aliyemtuma why?.....anzeni na aliyemtuma.....na muache unafiki na double standards kwenye kazi zenu....hii inawageuka hata nyie wenyewe.....
 
Haha kweli hii inchi vituko daah taarifa ya kumsaka huyo jamaa ilipaswa kuwa confidential na ndani ya wizara husika.
Raratu sijui zikoje Siku hizi sasa jamaa si anawezapotea na asikamatwe.

Ilipaswa Waziri aseme tu kwa ujumla wake kwamba wanshughulikia swala hilo kwa umma then mchakato wa siri ndani ya wizara unaendelea....

Ukweli ni kwamba askari yule alikusudia au aliagizwa kuua maana huwezi mtolea MTU bastola kwa asiye na silaha yoyote au ndio uTISS wa siku hizi?!

Kila kitu lazima kiwe mubashara kwa sababu ya hali tuliyonayo. Je wewe unadhani kwa awamu hii "confidentiality" ina tija? Umemwona Rais wako akitumbua watu confidentially? Au umeona mambo mengi yalivyo sasa.....nenda na midundo ya ngoma ubaki kwenye game. The rules of the game has long changed rafiki!
 
Mwigulu kubali mlichelewa kurudisha HESHIMA ya jeshi la polisi.Wakati Sirro akining'inizwa na RC hukufanya effort za kumuonya Sirro nor RC.

Hujafanya effort za kuwaonya ma RPC na ma OCD kufuata sheria na si kila mtu ampe order ya kukamata kamata watu sababu ya itikadi.

Mmelea upumbavu huu ngoja na nyie mfanyiwe ndipo mtajua ukipiga ugali lazima uungue na moto
 
Wewe unaleta urafiki binafsi wa mitaani ktk kazi na maadili ya kitaifa. Wakati Lipumba anatwangwa vibao kule Mbagala na kutupwa kwenye gari la polisi wakiwa na siraha, yeye mwenyewe alikuwa na silaha au rekodi ya uhalifu?

Mwangosi alipotumbuliwa utumbo, alikuwa na silaha? Munarahisisha maisha ya wengine na kuamini ninyi muna hadhi kubwa bila sababu.

Nahisi uwaziri safari hii haulipi kama mulivyotegemea na wengi munatafuta sababu ya kuondoka kwa kushangiliwa.
 
Kwanza mh Nchemba uwe tayari kutumbuliwa maana umebaki wewe na January.Vile vile lazima ujue kua askari wanafanya kazi kibashitebashite hakuna weledi hapo.Huyo askari ametumwa na Daud usimuonee na kama una uchungu sana na upo tayari kutumbuliwa mshughulikie aliyemtuma ndg Daud
Ni kweli kabisa umenena vyema kabisa. Sina cha kuongeza hapo.
 
Mbona kama kizungumkuti?
Si ajabu tukaambiwa yule aliyetoa bastola alikuwa jambazi wala hahusiki na watu wa usalama.
 
Hata anaweza kuondolewa kwenye uwaziri kama ilivyofanyika kwa Nape. Hii nchi Mwenyezi Mungu awape watawala na wasaidizi wao hekima. Mwenye tuhuma za vyeti ameachwa, aliyevamia kituo cha tv ameachwa, aliyewatukana watumishi wa ardhi kinondoni na kujifananisha na Mungu ameachwa, aliyepuuza wito wa mahakama na kamati ya maadili ya bunge ameachwa lakini pia mwenye tuhuma zingine lukuki hatishiwi bastola
Je, kuongea na wanahabari ni uhalifu kuliko haya yaliyofanywa na rc?

Leo umeamka vizuri
 
Hizi double standard zitatupeleka pabaya muheshimiwa... Double standard = kukanyaga haki ya wengine. Mbona umekuwa kimya kama maji ya mtungi kwenye matukio mengine ya aina hii?

Ulishasikia ule wimbo unaimbwa:

"Cheo ni dhadhama hakuna mtu aliyezaliwa naaaacho, ukiingia madarakani yapasa kusimama kwenye haaaki, wala usijidanganye walio chini hawajui kiiiitu, haki ya mnyonnge haipotei bali inacheleweshwaaa... Cheeezeaaa viiiiingine usichezee amaniiii ikitoweeeka...."

Huu wimbo hata kiongozi mkuu bosi wako nimemuona kwenye video anauimba na kucheza. Haya bana, tendeni haki aisee...
 
Taarifa kwa vyombo vya habari

Leo 25/7/2017 Mheshimiwa Rais amefanya Mabadiliko katika baraza la Mawaziri Professor--------------- ameteuliwa kuwa Waziri wa Mambo ya ndani

Uteuzi huu umeanza taangu Jana na wataapishwa Ikulu tarehe 26/7/2017

Imetolewa na Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais Ikulu
Jaruu Musiingwa

Nawaza Tuuuu!!!!!?
 
Back
Top Bottom