habari ya hapa
JF-Expert Member
- Dec 20, 2012
- 12,791
- 8,739
binafsi nimeacha siku nyingi kuamini kuhusu dini isipokuwa naamini katika mambo haya:-Sijawahi kuamini kuwa muislamu ni bora zaidi ya mkristo au kinyume chake .....haya mambo ya udini ni mabaya maana hats shuke tumefundishwa Na walimu wa dini zote........
1. Naamini akilini mwangu na moyoni mwangu kuwa Mungu yupo
2. Nihakikishe kuwa ninachukia na kuachana na uovu wote siku zote za maisha yangu
3. Nitende haki, nitetee haki, nisimamie haki maishani mwangu mwote
4. Niwapende binadamu wote bila ya ubaguzi, niwe tayari kuwasaidia katika matatizo yao mahali ninapojiweza
5. Niipende kazi na niifanye kwa bidii, kuhakikisha kuwa naifanya dunia hii kuwa makao ya wanadamu kwani kupitia kazi za mikono yangu Mungu atanibariki, naamini kuwa kwa kufanya haya Mungu atanipenda na watu watafurahia uweppo wangu hapa duniani.