Waziri mkuu Mizengo Pinda akana serikali haijamfunga mikono Dr.Hosea

Breki sina

Member
Jun 3, 2013
96
31
Bungeni Dodoma kupitia maswali ya papo kwa papo kutoka kwa Mh Ally mohamed ameuliza kuwa hivi karibuni viongozi wa kitaifa wameonekana wakilalamika kuwa Ufisadi ni tatizo kubwa,huku waziri mkuu akisema kuwa sio kulalamika kwa viongozi bali ni kuwakumbusha wananchi kuhusu tatizo hilo,huku akisema kuwa serikali haijamfunga mikono Dr.Hosea, hakika serikali hii haiwezi kupambana na ufisadi nchini nchi hii.

Soma sheria ya kitu
husika ndipo utoa hoja.Kwa
kukusaidia, Katika sheria namba
11 ya 2007 ya PCCB , Kifungu
cha 5 (2) sheria inatambulisha
kuwa PCCB ni chombo huru. Ukisoma kifungu cha 15 (1), (a)
& (b) utakuta panaelezewa
makosa madogo madogo ya
rushwa yasiyo ya maandishi au
mikataba ambapa Mkurugenzi
PCCB anaruhusiwa kupeleka mahakaman moja kwa moja na
kifungu cha 15 (2) ni Adhabu -
faini kati ya tshs 500,000/- na
1,000,000/- AU kifungo jela kati
ya miaka 3 na 5. AU vyote
kifungo na faini. Ukisoma kifungu cha 16 (1) (a)&
(b) na vifungu vingine vingi
siweza andika vyote, kinaelezea
makosa ambayo Mkurugenzi
hana mamlaka kupeleka kesi za
makosa hayo Mahakamani moja kwa moja isipokuwa mpaka
DPP atoe kibali chake, tena kwa
maandishi.
Kifungu cha 57 (1) & (2)
Kinamfunga mikono
mkurugenzi wa PCCB kutopeleka mafisadi papa
mahakamani moja kwa moja,
na ndicho anacholalamika
Dk.Hosea.
Hebu angalia sheria hii ilivyo ya
kibabaishaji. Katika kifungu cha 16 (3) adhabu yake ni kati ya
Tshs 1,000,000/- na 3,000,000/-
au kifungo jela kati ya miaka 3
hadi 5 AU vyote.
My take:-
*Dk. HOSEA yuko sahihi kuhusu kufungwa kwake mikono
kisheria.
* Sheria za adhabu kwa upande
wa faini haziangalii mpokea
rushwa amepiga bingo la kiasi
gani hata kama ni trilioni kadhaa, hakimu au jaji
atamtoza adhabu ya faini
isozidi Mill. 3
* Wanaotunga sheria ipo haja
kuifanyia marekebisho
*@ breki sina, Tusifanye ushabiki wa siasa ktk masuala
muhimu kama haya
 
Sasa anakana nini wakti Dr. Hosea mwenyewe kasema serikali imemfunga mkono?

Mh Pinda hakuna kitu na si lolote huyu nimeamini ni sawa na shok up kwenye gari huwezi amini anadai kuwa takukuru haiwezi kuchunguza na kupeleka kesi mahakamani hivyo wameweka utaratibu wa kupeleka kwa Dpp ili yeye ndio ahusike kupeleka hizo kesi mahakamani kuwa ni kutenda haki kwa watuhumiwa anachoficha Pinda na alichosema Hosea ni kuwa kesi zinazohusu mapapa na Nyangumi Takukuru hairuhusiwi kizipeleka mahakamani ila hizi za wezi wa kuku wanaruhusiwa kuzipeleka bila kupita kwa Dpp unaweza kuona jinsi ambavyo anawalinda mafisadi watanzania tusiwe wasahaulifu ni hivi karibuni kulitokea malumbano kati ya Dr.Hosea na Dpp kuhusu faili la Chenge kila mmoja akidai lipo ofisini kwake kuhusu pesa za Rada haya ndio mambo yanayowachikuza wananchi hata mkitupinga mkongoto,mioyo ya watu ikisha ingiwa na kiu ya kutaka mabadiliko hakuna Risasi ya kuizuia kamwe.
 
Basi akabidhiwe yale mafaili 60 ya vigogo ili ayafanyie kazi kisheria pasipo kuingiliwa. Hizi kauli kauli za danganya toto tumeshazichoka.
 
Ni kweli kajifunga mwenyewe na unafiki wake na ubinafsi wake.
 
Pinda ndani kabisa ya dhamira yake anajua anasema uongo na yuko pale kutumikia mabosi zake ili kuvimbisha tumbo lake. Hivyo kumsikiliza huyu bwana ni kujibumbaza au kujipotezea muda wa kufanya mambo ya msingi
 
Huyu mfalme wa nyuki hana lolote. Ni msanii sana na siasa ndo nyingi kuliko utekelezaji. Kwa hiyo anasema Dr. Hosea anaonhopa?
 
Tatizo la WM anakataa vitu ambavyo viko
bayana kabisa tena havihitaji pesa ya kigeni
Kwani Dr Hosea ni mjinga mbona kwenye
mkutano na wabunge Dodoma alisema na
Wabunge wakasema wazi.


Tatizo la Nchi hii siasa ina nguvu hata kwenye utaalam.
 
MH.HOSEA,,yupo sahihi,,anataka apewe mamlaka kama ya CAG,,,yakutoojiwa katika kazi yake,,,,iweje uchunguzi afanye yeye alafu kesi apelekewe DPP,,,na yeye ndio anayeamua iwapo swala lifike mahakamani au file liweke kapuni,,,,HOSEA YUPO SAHIHI,,,serikali imemfunga mkono,,,hana tofauti na uhuru wa bendera
 
watu wengine sijui ni viumbe gani sote tulimsikiliza hosea na sote tumemsikia mh pinda sasa huyu mleta hoja anajidanganya yeye au anataka kutudanganya na cc.
 
Mnafiki kwa lipi? Ana ubinafsi upi? Labda una chuki binafsi
We uoni unafiki wake?
Anashindwa kufanya kazi yake kakaa kulia lia oh nazuiwa si aseme kashindwa na aache ubinafsi aachie kiti watendaji kazi washike.!
 
Huyu baba kwa uongo kakubuhu mia

"To know the enemy is half the victory"
 
MH.HOSEA,,yupo sahihi,,anataka apewe mamlaka kama ya CAG,,,yakutoojiwa katika kazi yake,,,,iweje uchunguzi afanye yeye alafu kesi apelekewe DPP,,,na yeye ndio anayeamua iwapo swala lifike mahakamani au file liweke kapuni,,,,HOSEA YUPO SAHIHI,,,serikali imemfunga mkono,,,hana tofauti na uhuru wa bendera

haya maoni yake apeleke kwenye katiba mpya ili yafanyiwe kazi.
 
Mnafiki kwa lipi? Ana ubinafsi upi? Labda una chuki binafsi

Diunal jenga hoja ana chuki gani wakati ukweli upo wazi tunajenga hoja kwa mfano wewe unaleta mambo ya kanga humu jamvini kwa mfano wenzetu Kenya wao taasisi yao inayohusika na masuala ya upelelezi ndio inapeleka kesi mahakamani chini ya utaratibu mpya waliojiwekea baada ya kukubwa na kashifa nyingi kama Golden berg,na zingine nyingi ni hivi jana tu kesi iliyokuwa inahusu uhujumu uchumi kuhusu shirika la UDA imefutwa na Dpp who knows nini kipu huko,ni lazima tuwe na taasisi zilizo imara ili kupambana na ufisadi ulio kidhili nchi hii,na viongozi wanaoweza kusimamia sheria zilizopo .
 
Mh Pinda hakuna kitu na si lolote huyu nimeamini ni sawa na shok up kwenye gari huwezi amini anadai kuwa takukuru haiwezi kuchunguza na kupeleka kesi mahakamani hivyo wameweka utaratibu wa kupeleka kwa Dpp ili yeye ndio ahusike kupeleka hizo kesi mahakamani kuwa ni kutenda haki kwa watuhumiwa anachoficha Pinda na alichosema Hosea ni kuwa kesi zinazohusu mapapa na Nyangumi Takukuru hairuhusiwi kizipeleka mahakamani ila hizi za wezi wa kuku wanaruhusiwa kuzipeleka bila kupita kwa Dpp unaweza kuona jinsi ambavyo anawalinda mafisadi watanzania tusiwe wasahaulifu ni hivi karibuni kulitokea malumbano kati ya Dr.Hosea na Dpp kuhusu faili la Chenge kila mmoja akidai lipo ofisini kwake kuhusu pesa za Rada haya ndio mambo yanayowachikuza wananchi hata mkitupinga mkongoto,mioyo ya watu ikisha ingiwa na kiu ya kutaka mabadiliko hakuna Risasi ya kuizuia kamwe.

Utaratibu wa Takukuru kupeleka kesi kwa DPP kabala ya kwenda mahakamani moja kwa moja ndio uchochoro wa kuwa linda mafisadi kwa yeye DPP kutumia powers zale za NOLLE.... Hivi niandikapo DPP ametumia powers hizo hizo kufuta kesi ya kuhujumu uchumi iliyokuwa inamkabili fisadi mwingine waziri wa zamani Idd Simba!!!!
 
Diunal jenga hoja ana chuki gani wakati ukweli upo wazi tunajenga hoja kwa mfano wewe unaleta mambo ya kanga humu jamvini kwa mfano wenzetu Kenya wao taasisi yao inayohusika na masuala ya upelelezi ndio inapeleka kesi mahakamani chini ya utaratibu mpya waliojiwekea baada ya kukubwa na kashifa nyingi kama Golden berg,na zingine nyingi ni hivi jana tu kesi iliyokuwa inahusu uhujumu uchumi kuhusu shirika la UDA imefutwa na Dpp who knows nini kipu huko,ni lazima tuwe na taasisi zilizo imara ili kupambana na ufisadi ulio kidhili nchi hii,na viongozi wanaoweza kusimamia sheria zilizopo .
sina breki,Sorry, labda cjakuelewa kuwa mnafiki ni yupi. Me nimekuelewa unamsema Dk. HOSEA ndo mnafiki. Kama ni Pinda basi nakuunga mguu 1500%
 
Last edited by a moderator:
Back
Top Bottom