Waziri Lazaro Nyalandu ajibu tuhuma za Mbunge Joshua Nassari

calist91

Member
Jan 23, 2012
43
22

Jana wakati akichangia bungeni Mheshimiwa Nassari aliichana chana serikali ya CCM kwa kusema "imechoka" huku akimtaja moja kwa moja Nyalandu kuwa amekuwa bingwa wa kupiga picha na mbwa wa wazungu, ameshika bunduki, kupiga picha na mamiss na akiwa amemmbeba askari wa wanyapori.

Inaonekana Waziri Nyalandu hakuifurahia hotuba ya Mheshimiwa Joshua Nassari na ametoa tamko:

Nimesikitishwa sana na kauli ya Mhe. NASSARI ambayo ameongea kwa kudhalilisha utendaji wangu serikalini. Naomba Mh Nassari afahamu kuwa kunikashifu pasipo kueleza masuala ya kisera au ya kiutendaji ni kupungukiwa na busara ya kawaida kwa kiongozi aliyepaswa kuwawakilisha wapiga kura wake kwa hoja.

Itakumbukwa kuwa hivi karibuni MH Nassari aliniita Jimboni kwake Armeru Mashariki akiniomba nitatue tatizo lililohusu wananchi wa Jimboni kwake waliokuwa wanahitaji matibabu katika hospitali ambayo ilikuwa sharti upitie ndani ya hifadhi ili ufike kutibiwa. Nilikwenda kuwaona wagonjwa na kuitembelea hospitali hiyo na kulitatua tatizo hilo siku hiyo hiyo. Kwangu kama Waziri, halikuwa suala la kufanyia siasa suala la afya za watanzania, pamoja na yeye kuwa Mbunge wa upinzani.


Nilimheshimu na kukubali wito wake kwa niaba ya wananchi. Nimewatembelea na kuwatia moyo maaskari wetu nchi nzima na kuwapelekea vitendea kazi. Nimefurahi pamoja nao na kulia pamoja nao.

Nimeenda kuwafariji Familia za wapiganaji wetu waliopoteza maisha kwa kuuawa wakilinda raslimali za Taifa, watu ambao Mh Nassari anawabeza. Tumepambana na ujangili na tunaendelea kuushinda. Tumeleta magari, silaha, ndege, helicopters, na raslimali nyingi ili kulinda raslimali za Taifa.

Busara haisomewi ila ni kumshukuru Mungu akusaidie kujua matumizi ya ulimi. Nimesikitishwa sana na kauli za uongo na kuzusha za Mh Nassari.
Source: Wavuti
 
Niliisikiliza ile hotuba na binafsi sikupenda alivyomshambulia Nyalandu. Najua kama upinzani wana kazi ya kuikosoa serikali lakini ukishaingiza personal attack kwa mtu na familia yake unakuwa umevuka mpaka.

Hao wamechanganyikiwa hawana sera pale unatakiwa kutoa hoja za msing ciyo kukashfu.
 
Kiongozi ni kioo cha jamii,kwa hiyo matendo yako yanamulikwa na wanajamii kwa hiyo unatakiwa use mfano wa kuigwa,kujificha katika Sera haitoshi. Kiongozi wa kisiasa unambeba askari wa like,umeoa tena una familia unaiweka katika kundi gani familia yako? Kwa ni ni asimbebe askari wa kiume? Hana haja ya kulalamika ajichunguze
 
Nassari ana ugonjwa wa kusahau hebu tumkumbushe hii

View attachment 196321
Waziri wa Maliasili na Utalii, Lazaro Nyalandu

Wabunge wa Kanda ya Kaskazini wamemtaka Waziri wa Maliasili na Utalii, Lazaro Nyalandu, kutovunjika moyo kutokana na kauli za baadhi ya watu wanaoushutumu utendaji wake.

Wakizungumza katika mkutano wa viongozi wa mikoa ya Arusha na Kilimanajaro, wabunge hao wamesema wanaomuandama wana kinyongo na utendaji wake.

Wabunge hao ni Aggrey Mwanri wa Siha na Joshua Nassari wa Arumeru Mashariki, ambao walimpongeza kwa hatua anazochukua kwa kulinda maliasili na kupambana na ujangili na kumtaka aongeze bidiii. “Usife moyo kwa kuwa tunajua unafanya kazi zako vizuri kwa manufaa ya taifa, ukiona wanakurushia mawe, usifadhaike.Ndiyo wanakuongezea nguvu za kuweza kuongoza,” alisema Mwanri.

Alimpongeza kwa kuja na wazo la kuundwa kwa mfuko wa Uhifadhi wa Milima Kilimanjaro na Meru na kusema kuwa hiyo itasaidia wananchi kwani utalii utaongezeka na uhifadhi wa mazingira utakuwa bora zaidi.

“Nazungumza hivi sio kwamba nataka kujipendekeza kwako, kwani hapa nilipo ninahitaji nini zaidi? Lazima kusema ukweli na sio kuzushiana,” alisema.

Mbunge wa Arumeru Mashariki, Nassari alisema amekuwa akifuatilia utendaji wa waziri huyo na kupata faraja jinsi anavyoshughulikia masuala ya maliasili.

“Naomba kukutia moyo kwani anayefanya kazi ya Mungu atapata nguvu, nikisikia mtu bungeni anasema wewe ni waziri mzigo, mimi nitaruka juu na kumwangukia vibaya,” alisema.

Alisema kwa waziri kuchukua uzito wa kuanzisha mfuko wa kuhifadhi milima hiyo ni hatua muhimu kwa wananchi wa mikoa ya Arusha na Kilimanjaro ambao wamekuwa wakitegemea milima hiyo kwa ajili ya utalii.

Kwa upande wake Nyalandu alisema kwa kasi iliyopo sasa watu kutumia vibaya bidhaa zitokanazo na misitu, baada ya miaka 15 kuna wasiwasi nchi ikawa jangwa kama hatua za haraka hazijachukuliwa.

“Milima hii ndio imekuwa chanzo cha maji kwa wananchi wa mikoa ya Arusha na Kilimanjaro lakini kwa kasi ya ukataji miti kwa matumizi ya nyumbani imekuwa trishio kwani hadi sasa hivi barafu katika mlima Kilimanjaro imepungua kwa kiasi kikubwa” alisema Nyalandu.

Nyalandu alisema kasi ya ukataji miti nchini imekuwa kubwa kwa sasa kutokana na kuongezeka kwa idadi ya watu na kuwa kwa mwaka mmoja pekee hekta 350,000 hukatwa huku kikiwa hakuna jitihada za kurejesha iliyoondolewa.



Source: Nipashe

Home
 
Ile.picha aliyopiga na askri gemu akiweka kambeba kimahaba kweli inaenda sawa na heshima aliyopewa na rais
Saa ingine tuache ushabiki wa kisiasa tuongee ukweli
Wengine hiyo picha imetupita
Hebu iwekeni hapa tuione basii
Namshukuruni.
 
Nassary si ndio anataka nchi ya Kaskazini, Lema awe Rais ,halafu yeye awe Waziri Mkuu
 
Nassary alishampiga marufuku JK asikanyage kwenye nchi ya Chadema ya Kaskazini
 
Back
Top Bottom