Waziri Katambi: No Research no right to speak. Hayo ndo majibu ya Waziri kwa wastaafu

Kididimo

JF-Expert Member
Sep 20, 2016
3,795
3,361
Hayo ndo majibu ya Naibu Waziri wa Kazi na Ajira kuhusu hatima ya kikokotoo kipya kwa wastaafu. Kuwa kafanya utafiti unaoonesha ni kikokotoo bora kuliko cha zamani. Hivyo, wastaafu wafanye utafiti ndo waulize wasilalamike tuu.

Mawaziri kama hawa hawatufai katika nchi inayotambua haki na maslahi kwa makundi maalumu kama wazee wastaafu.

Wastaafu wengi wameonesha kitoridhika na kikokotoo kipya cha mafao yao. Wanadai walipwe kwa kutumia mfumo wa kikokotoo cha zamani. Ni haki yao, na ingefaa kuweka hata option au kura ya maoni ukweli upatikane.

Serikali isishinikize jambo lisilo na afya kwa walengwa wa mifuko hiyo. Ni jambo la aibu kwa Waziri kumwambia mstaafu mwenye miaka 80 akafanye utafiti ili agundue ubora wa vikokotoo hivyo viwili.

Mama yetu, na Rais wetu wanaokuangusha siyo wengine ni hao wateule wako.
 
Natarajia maaskofu kutoa waraka kuhusu kikokotoo. maana tafti zinaonesha wafanyakazi wote hawakitaki. kama ndani ya waraka wamewagusia wamasai kwani wasiwagusie wafanyakazi katika hili?
 
Haya ma@ccm yanaleta jeuri na dharau kwa Watanzania, sababu yanatambua fika hata yasipopigiwa kura bado yatashinda tu kwenye uchaguzi kupitia ile tume yao mbovu, na pia policcm.
 
Kikokotoo kipya hakiwahusu wanasiasa wakiwemo mawaziri na wale wagonga meza wazee wa ndiooooo ndo maana huyo chitambi anaongea pumba yoyote inayomwijia kinywani.
 
Mimi nilivyomuelewa hakuwa anawajibu wastaafu. Alikuwa anamjibu mbunge ambaye ameuliza swali bila kufanya utafiti kwanza na baadaye alimwambia kama analotatizo afike ofisini kwake atamuelimisha. Kwa hiyo sio wastaafu.
 
Hayo ndo majibu ya Naibu Waziri wa Kazi na Ajira kuhusu hatima ya kikokotoo kipya kwa wastaafu. Kuwa kafanya utafiti unaoonesha ni kikokotoo bora kuliko cha zamani. Hivyo, wastaafu wafanye utafiti ndo waulize wasialamike tuu.
wengine ni hao wateule wako.
Watu wana njia nyingi za kusingizia ili wanayoyafanya watu wengine wasiwakosoe au wasiwe na maoni tofauti. Hebu fikiria ukitaka kutoa maoni mpaka ufanye research sasa sijui ni nani ataisimamia na yeye huyo waziri mstaafu anajuaje kwamba hao wastaafu hawajafanya hiyo research anayoisema?
 
Serikali isishinikize jambo lisilo na afya kwa walengwa wa mifuko hiyo. Ni jambo la aibu kwa Waziri kumwambia mstaafu mwenye miaka 80 akafanye utafiti ili agundue ubora wa vikokotoo hivyo viwili.
Tuna viongozi wa ajabu sana wenye dharau na walivimbiwa madaraka!
Mama SSH angalia hawa ndio mawaziri wako wenye majibu mabovu kabisa!
 
Udhalimu ni kitu kibaya sana hawa wana siasa watambue hilo!
Wastaafu wanapunjwa sana stahiki zao walizofanyia kazi kwa miaka mingi!
Wangekuwa wao (wanasiasa) ndio wanalipwa kwa kikokotoo hiki ungekuta walishabadilisha!
 
Mimi nilivyomuelewa hakuwa anawajibu wastaafu. Alikuwa anamjibu mbunge ambaye ameuliza swali bila kufanya utafiti kwanza na baadaye alimwambia kama analotatizo afike ofisini kwake atamuelimisha. Kwa hiyo sio wastaafu.
Ndugu,unaishi Tanzania ipi. Wabunge ni wawakilishi wa wananchi wakiwemo wastaafu. Mbunge aliuliza swali ambalo ama ametumwa na wawakilishi au ameuliza kwa niaba ya wananchi wake.
Majibu yoyote ya serikali kwa mbunge kama hayo, ni logical kusema anayejibiwa ni mwananchi( mstaafu). Mbunge hatafikisha majibu mengine kwa waliomtuma isipokuwa ni yale aliyojibiwa Mbunge.
Waziri awaombe radhi wastaafu wote nchini kwa kejeli hiyo.
Ni jambo la ajabu serikali kungangania fedha za wastaafu. Ni laana kubwa. Baadhi ya wastaafu wamepoteza maisha kwa mshtuko wa kupokea ambacho hawakutarajia.
Ni kwa nini kama ni kweli kikokotoo kipya ni kizuri , mstaafu asipewe option ya kuamua ni kipi atataka kutumia kwa sababu pesa ni zake?
Serikali imengangania tafiti zisizo za uwazi. Ni kwa nini isipitishwe kura ya maoni kwa wastaafu ili ukweli upatikane?
Mh. Waziri ni kijana mdogo,yawezekana kwake suala hili halimgusi moja kwz moja,ndiyo maana zinamtoka kejeli za aina hiyo.
 
Hayo ndo majibu ya Naibu Waziri wa Kazi na Ajira kuhusu hatima ya kikokotoo kipya kwa wastaafu. Kuwa kafanya utafiti unaoonesha ni kikokotoo bora kuliko cha zamani. Hivyo, wastaafu wafanye utafiti ndo waulize wasialamike tuu.

Mawaziri kama hawa hawatufai katika nchi inayotambua haki na maslahi kwa makundi maalumu kama wazee wastaafu.

Wastaafu wengi wameonesha kitoridhika na kikokotoo kipya cha mafao yao. Wanadai walipwe kwa kutumia mfumo wa kikokotoo cha zamani. Ni haki yao, na ingefaa kuweka hata option au kura ya maoni ukweli upatikane.

Serikali isishinikize jambo lisilo na afya kwa walengwa wa mifuko hiyo. Ni jambo la aibu kwa Waziri kumwambia mstaafu mwenye miaka 80 akafanye utafiti ili agundue ubora wa vikokotoo hivyo viwili.

Mama yetu, na Rais wetu wanaokuangusha siyo wengine ni hao wateule wako.
sio jibu la kiungwana, anazidisha laumu za wanaoathirika na hicho kikokotoo. Huyu akishuka chini kupanda tena juu itakua tabu sana.
 
Tuna viongozi wa ajabu sana wenye dharau na walivimbiwa madaraka!
Mama SSH angalia hawa ndio mawaziri wako wenye majibu mabovu kabisa!
Huyu waziri uwa ananichekesha, anapendaga vijimisemo vya kishule shule Ha ha ha! Inaonesha alishiriki sana debate nyakati zake.

Hii misemo ya kukariri ya wazungu haiendani na maisha halisi ya watanzania. Right ya kuongea ipo kikatiba uhitaji utafiti ili uongee. Nyingi za tafiti ni probability!
 
Back
Top Bottom