Waziri Bashe hakutakiwa kuukataa msaada wa mchele kutoka Marekani na kama alikuwa na mashaka yoyote angewatumia TBS

Sio kwamba alikua hajui sema ni kwakua lime bumbuluka ivyo kaona apite na upepo wa siasa ... na sio kwamba mchele auta letwa .mchele uta kuja kama kawaidaaa na hamna kitu mta fanya
 
Ukiambiwa wananunua mchele kilo 200 mtauza? Maana inawezekana kwao wananunua kilo shs 200
Kilo miambili, mifuko kuprint, kuinunua, kusafirisha mpaka kwa mlengwa hata tz unafikiri ni gharama ndogo?

Vya bure vyaua , hivi huo mchele wa kuuziwa kilo mia 200, huo ni mchele au makapi
 
Bashe yupo sahihi kwamba,badala ya kuleta Michele,walete hizo pesa wanunue Kwa wakulima watanzania hizo shule zipewe,mm nashangaa,kwanini wasitupe teknolojia na ujuzi wa kuzalisha huo Michele maana ardhi tunayo kama kweli Wana ni ya kutusaidia?,je,hao wamarekani watatulisha hafi lini?
Yani unahitaji mafunzo ya kulima mchele wakati tayari ushapigwa na njaa hiyo ni ngumu ukweli ni kwamba Tanzania tunajisifia tu kwamba tunachakula cha kutosha ila hakuna wanafunzi wanakunywa uji familia nyingi zinaishi kwa kula mlo mmoja mpaka miwili tena isiyo kamili...
 
Bashe yupo sahihi kwamba,badala ya kuleta Michele,walete hizo pesa wanunue Kwa wakulima watanzania hizo shule zipewe,mm nashangaa,kwanini wasitupe teknolojia na ujuzi wa kuzalisha huo Michele maana ardhi tunayo kama kweli Wana ni ya kutusaidia?,je,hao wamarekani watatulisha hafi lini?
Ninachojiuliza, kwani tz kuna njaa. Nani alieomba huo msaada. Wa Tz kupenda kitonga hawajanbo
 
Yani unahitaji mafunzo ya kulima mchele wakati tayari ushapigwa na njaa hiyo ni ngumu ukweli ni kwamba Tanzania tunajisifia tu kwamba tunachakula cha kutosha ila hakuna wanafunzi wanakunywa uji familia nyingi zinaishi kwa kula mlo mmoja mpaka miwili tena isiyo kamili...
Hawa wazalendo uchwara wanachosha sana na kelele zao.
 
Watanzania hatujui tunataka nini.

Kuna wanaosema bora mchele tukatae wengine wanasema tuukubali.

Ila mimi naishauri marekani WAACHE KUTOA MISAADA AMBAYO HAWAKUOMBWA.

laiti kama tanzania imgekuwa imeomba huu mchele basi Bashe asingeukataa.

Tatizo sio tanzania kukataa msaada hapana bali tatizo ni la wamarekani kutoa msaada ambao hawakuombwa.

Wapeleke mchele katika nchi zenye njaa na migogoro ambayo inawaletea uhaba wa chakula.
Wamarekani ni binadamu wenye utu na uchungu na raia wa nchii hii. Wao wanajua kwamba raia wana shida na njaa na viongozi hawajali. Wao wanajua kuwa viongozi wanaishi kwenye maisha ya kifahari ila raia wanakufa kwa njaa. Wanafanya haya kwa sababu wanajali maisha ya watanzania na siyo kama kina Bashe. Bashe hata wafe raia elfu hana uchungu wowote. Unakumbuka kipindi cha Magufuli ilikuwa marufuku kusema sehemu fulani inakabiliwa na njaa hata kama ilikuwa ni kweli?
 
Hawa wazalendo uchwara wanachosha sana na kelele zao.
Ndomana hatuendelei mana siasa kwenye kila kitu kama umepewa kitu si unajiridhisha kitaalamu si mnao wakemia na maabara kwann msifanye vipimo kujua usalama wa hicho chakula kabla ya kuanza kutafuta kiki kwa raiya wenye njaa.
 
Unataka Wamarekani wakulishie shule zako zote juu ya kukujengea matundu ya vyoo pia??
Una evidence ya write up ya Serikali ya Tanzania kuomba msaada wa chakula kulisha hizo shule au ni janjajanja ya NGOs kushirikiana na US Dept of Agriculture kwa maslahi yao?! Wakitumia loopholes ya viongozi crooks hapa nchini? Watoto wetu wasitumike kama objects za kutajirisha wenye NGOs na wakulima wa marekani.
Bwashe yupo sahihi.
 
Mada hii ni kuelezea mashaka makubwa niliyonayo kwa Waziri wetu wa kilimo namna maamuzi yake yanavyoweza kuharibu mahusiano ya kimataifa kama asipojirekebisha.

Kwanza kabisa nianze Kwa 'declare interest' ,Sina mahusiano ya aina yoyote na NGO iliyoleta mchele wa msaada wenye virutubisho kutoka nchini Marekani chini ya kampeni ya wizara ya kilimo ya Marekani inayoitwa "Pamoja tuwalishe" na 'interest' pekee niliyonayo ni Kwa maslahi mapana ya nchi yangu .

Siku zote mjumbe hauawi na hiyo NGO inabaki kuwa ni mjumbe tu wa wizara ya kilimo ya Marekani ,kitendo Cha Waziri kuonesha kukasirishwa na kitendo Cha mjumbe kinaleta picha isiyopendeza.

Kwa mtazamo wangu badala ya Waziri Bashe kuonesha kukasirishwa na kuletwa Kwa mchele na hiyo NGO angetumia nafasi hiyo kufanya "formal communication" na wizara ya kilimo ya Marekani juu ya mambo tunayohitaji.

Kwa kuwa mchele huo ni msaada sikuona ulazima wowote wa Waziri kusema kwamba mchele tunao ,Kwa kuwa lengo la kampeni hiyo ni zuri ,tunatakiwa kuupokea msaada huo na kushukuru na wizara ingetumia TBS kuchunguza ubora wa mchele huo kimya kimya kabla haujaanza kutumika na kama kungekuwa na mashaka yoyote Serikali ingekataa baada ya kufanyika Kwa uchunguzi na ubora na sio Kwa hoja za Waziri.

Mashaka niliyonayo kwa Waziri Bashe ni kuwa:

Kama Waziri hajui athari za kimahusiano zinazoweza kuibuka kutokana na kauli tu. Kitendo Cha Waziri Bashe kudai Kwa nini wasingeleta virutubisho wachanganye tukiwaona ,sio rafiki Kwa afya ya diplomasia. Kitendo hicho kinaweza kufikirika kama tuhuma ya usalama. Kabla ya kauli hiyo alitakiwa kuwatumia TBS kuuchunguza mchele.

Marekani ni Moja ya nchi zinazozalisha nataka ( mchele na mahindi) Kwa wingi duniani na kutokana na mabadiliko ya hali ya hewa ,nchi yetu inaweza kukumbwa na baa la njaa na tukahitaji msaada wa Chakula kutoka nje. Je, tutapata wapi nguvu za kuomba msaada kutoka Marekani kama tumeamua kukataa msaada Sasa ?

Pengine kulikuwa na Cha zaidi ambacho hatukijui lakini kama ni hiki kilichopo ,ni vema Waziri Bashe angeliendea suala Hilo Kwa busara, angejiridhisha kwanza na angejua hatua Kwa busara ili tuendelee kuimarisha mahusiano na nchi nyingine.

Kila siku Rais anasisitiza mifumo kusomana ili kuepusha migogoro , na kama mifumo ingekuwa inasomana kusingekuwa na kauli za namna Ile kutoka Kwa Waziri.

Ahsante

Hana ubavu wa kuzuia lolote 🤣🤣🤣🤣🤣
 
Kwani huo misaada ni wa serikali ya Marekani,au NGO kutoka Marekani? Acheni kubabaisha watu bhana,na hata kama tutapata Janga,sio Marekani tu itatusaidia,nyinyi kama mlikuwa na lengo la upigaji mmeliwa mtulie tu🤣🤣🤣
Kweli mnahitaji msaada au mnataka mpewe mkauze Burundi?
Nyie ndio wapiga dili mnapambana mpate magunia kadhaa mkayauze
Tunajua hata maturubali ya shirika la ukimbizi yalikuwa yanaibiwa Ulyankulu na kuuzwa kwa kuanikia mahindi badala ya tent au ulikuwa hujazaliwa?

Hamuhitaji misaada bali akili ya kujikomboa kutoka kwenye umasikini
Umasikini ni Laana
 
Una evidence ya write up ya Serikali ya Tanzania kuomba msaada wa chakula kulisha hizo shule au ni janjajanja ya NGOs kushirikiana na US Dept of Agriculture kwa maslahi yao?! Wakitumia loopholes ya viongozi crooks hapa nchini? Watoto wetu wasitumike kama objects za kutajirisha wenye NGOs na wakulima wa marekani.
Bwashe yupo sahihi.
Watoto wenu wapeni ubwabwa mashuleni, acheni porojo za kwamba mchele mnao mwingi huku wao wakisoma na njaa na hata huo ubwabwa wa maharage bado ni anasa kwao.
 
Lengo la msaada likiwa zuri hakuna sababu ya kukataa msaada, dunia nzima wanaishi hivyo
"Virutubisho" kwenye huo mchele na maharage husika ndo vinatiliwa mashaka mkuu. Bora kuzuia kuliko kutibu.
Hao watoto wakila wakageuka "mabwabwa" tiba itapatikana?!
 
Watoto wenu wapeni ubwabwa mashuleni, acheni porojo za kwamba mchele mnao mwingi huku wao wakisoma na njaa na hata huo ubwabwa wa maharage bado ni anasa kwao.
😅😅😅😅😅........Wacha fujo chifu. Ubwabwa siyo tatizo kwenye shule zetu hapa nchini. Atleast mara 2 kwa wiki.
 
Ndomana hatuendelei mana siasa kwenye kila kitu kama umepewa kitu si unajiridhisha kitaalamu si mnao wakemia na maabara kwann msifanye vipimo kujua usalama wa hicho chakula kabla ya kuanza kutafuta kiki kwa raiya wenye njaa.
Hii ndio hoja yangu. Kuna TBS na mengine mengi ila hayatumiki
 
Back
Top Bottom