Waziri Bashe hakutakiwa kuukataa msaada wa mchele kutoka Marekani na kama alikuwa na mashaka yoyote angewatumia TBS

Bashe atasababisha watoto wakatae kula chakula shuleni, yale yale ya anti-vaxxers tu kupinga watoto wao wasipewe chanjo.
Kauli ya Bashe ni mbaya sana, inapaswa kulaaniwa na watu wote wenye akili.
Bashe is right!
 
Kuhusu Msaaada Wa USAID Wa Chakula Lishe.

📌Ni kweli kuna ukosefu mkubwa wa chakula lishe chenye virutubisho kwa wanafunzi wengi maana vyakula vingi wanavyokula ni kuzuia njaa tu na sio kuleta afya ya mwili na akili hivyo udumavu unaongezeka.

📌USAID kwa mahaba makubwa kama ambavyo wanawajengea vyoo vya kujisaidia wameamua kuwaletea msaada wa vyakula vyenye virutubisho vizuri zaidi maana wahusika si mmejisahau ngoja wao wawakumbushe vizuri

📌Sisi tuko bize sana na mambo ya umbeya na umepigwa mwingi ila kuwa makini sana kuhusu afya za watoto wetu kwa mwili na akili wengi bado wako nyuma sana ila inapotokea mambo kama haya ndo tunaanza kupaza sauti ya kushituka eti huenda wana nia mbaya .

📌Nendeni mashuleni huko muone kuanzia asubuhi mpaka saa tisa watoto wenu wanakula vyakula vya aina gani je vina ongeza tija katika afya ya mwili na akil ? kisha muanze Kulalamika.

📌Huwa nasema wazazi na walezi wengi ni wabinafsi sana kwa watoto wao licha ya kujifanya wanapenda watoto wao mfano wakisikia semina za mizagamuo hata 50k Wanaenda ila semina zinazohusu watoto wao hata bure hawaendi huo ni UNAFIKI

Kitabu changu cha MZAZI ACHA UZEMBE; MAMBO 10 YA MSINGI KUZINGATIA KUHUSU ELIMU YA MTOTO WAKO.kingekuwa kinaongelea kuifinyia kwa ndani au kusimamia muda mrefu ungeona sharing zake kuwa nyingi na maswali kibao ila kwa vile ni kuhusu elimu ya watoto wao huwaoni sababu ya UNAFIKI wa kujifanya wanawapenda watoto wao kumbe hawawapendi kiuhalisia .

NB ; Msiache Kuweka Oda Kwa Namba 0718821168.
Ndugu yenu Magoda Jr 📌
Ujamaa Ni Imani

Haya Maoni ni mazuri sana
 
Mada hii ni kuelezea mashaka makubwa niliyonayo kwa Waziri wetu wa kilimo namna maamuzi yake yanavyoweza kuharibu mahusiano ya kimataifa kama asipojirekebisha.

Kwanza kabisa nianze Kwa 'declare interest' ,Sina mahusiano ya aina yoyote na NGO iliyoleta mchele wa msaada wenye virutubisho kutoka nchini Marekani chini ya kampeni ya wizara ya kilimo ya Marekani inayoitwa "Pamoja tuwalishe" na 'interest' pekee niliyonayo ni Kwa maslahi mapana ya nchi yangu .

Siku zote mjumbe hauawi na hiyo NGO inabaki kuwa ni mjumbe tu wa wizara ya kilimo ya Marekani ,kitendo Cha Waziri kuonesha kukasirishwa na kitendo Cha mjumbe kinaleta picha isiyopendeza.

Kwa mtazamo wangu badala ya Waziri Bashe kuonesha kukasirishwa na kuletwa Kwa mchele na hiyo NGO angetumia nafasi hiyo kufanya "formal communication" na wizara ya kilimo ya Marekani juu ya mambo tunayohitaji.

Kwa kuwa mchele huo ni msaada sikuona ulazima wowote wa Waziri kusema kwamba mchele tunao ,Kwa kuwa lengo la kampeni hiyo ni zuri ,tunatakiwa kuupokea msaada huo na kushukuru na wizara ingetumia TBS kuchunguza ubora wa mchele huo kimya kimya kabla haujaanza kutumika na kama kungekuwa na mashaka yoyote Serikali ingekataa baada ya kufanyika Kwa uchunguzi na ubora na sio Kwa hoja za Waziri.

Mashaka niliyonayo kwa Waziri Bashe ni kuwa:

Kama Waziri hajui athari za kimahusiano zinazoweza kuibuka kutokana na kauli tu. Kitendo Cha Waziri Bashe kudai Kwa nini wasingeleta virutubisho wachanganye tukiwaona ,sio rafiki Kwa afya ya diplomasia. Kitendo hicho kinaweza kufikirika kama tuhuma ya usalama. Kabla ya kauli hiyo alitakiwa kuwatumia TBS kuuchunguza mchele.

Marekani ni Moja ya nchi zinazozalisha nataka ( mchele na mahindi) Kwa wingi duniani na kutokana na mabadiliko ya hali ya hewa ,nchi yetu inaweza kukumbwa na baa la njaa na tukahitaji msaada wa Chakula kutoka nje. Je, tutapata wapi nguvu za kuomba msaada kutoka Marekani kama tumeamua kukataa msaada Sasa ?

Pengine kulikuwa na Cha zaidi ambacho hatukijui lakini kama ni hiki kilichopo ,ni vema Waziri Bashe angeliendea suala Hilo Kwa busara, angejiridhisha kwanza na angejua hatua Kwa busara ili tuendelee kuimarisha mahusiano na nchi nyingine.

Kila siku Rais anasisitiza mifumo kusomana ili kuepusha migogoro , na kama mifumo ingekuwa inasomana kusingekuwa na kauli za namna Ile kutoka Kwa Waziri.

Ahsante
Ni vizuri msaada ukatolewa kipindi cha uhitaji. Je, tuna upungufu wa chakula mpaka tuletewe msaada wa chakula? Au wamarekani wanatafuta soko la chakula chao kilazima na kuua soko la wazalishaji wa ndani?
 
Nani kakwambia hizo shule zinahitaji huo mchele na maharage!?
Sijaambiwa, nimesoma shule ambayo siku mchele au nyama vikipikwa inakuwa shangwe kama sikukuu na ukizembea unaweza kushinda njaa siku hiyo jinsi watu wanavyogombania ubwabwa au nyama.
 
Bashe yupo sahihi kwamba,badala ya kuleta Michele,walete hizo pesa wanunue Kwa wakulima watanzania hizo shule zipewe,mm nashangaa,kwanini wasitupe teknolojia na ujuzi wa kuzalisha huo Michele maana ardhi tunayo kama kweli Wana ni ya kutusaidia?,je,hao wamarekani watatulisha hafi lini?
Serikali ya Marekani inawasaidia wakulima wake kupata soko. Nawe unafaidika kwa kupata msaada. A win-win situation. Hawawezi kukuletea fedha.
 
Huo mchele umeshapigwa vita nchi kibao, ni wa maabara na si rafiki kwa afya ya mtumiaji. Huko kwao wenyewe wanaupiga vita ila waswahili wenzangu wa kingugi wanautetea! Tuna chakula fresh from shamba, hebu tuache kujitia ufukara uliopitiliza kwa kupokea hata misaada tusiyohitaji. Kama kweli hao wamarekani wana huruma na sisi basi watoe hizo hela mchele ununuliwe hapa nchini na kusambazwa mashuleni. Zingatia kuwa huo mchele umeongezwa "virutubisho"
Huelewei maana ya kuongezwa virutubisho, hata hapa Tanzania kuna vyakula vingi viko fortified, hata mafuta ya kula yanaoingizwa kutoka nje lazima yaongozewe virutubisho, chumvi inayochimbwa nchini lazima iongozwe virutubisho kabla ya kuuzwa.
 
Bashe yupo sahihi kwamba,badala ya kuleta Michele,walete hizo pesa wanunue Kwa wakulima watanzania hizo shule zipewe,mm nashangaa,kwanini wasitupe teknolojia na ujuzi wa kuzalisha huo Michele maana ardhi tunayo kama kweli Wana ni ya kutusaidia?,je,hao wamarekani watatulisha hafi lini?
Huna akili

Msaada umetolewa na wakulima wa Marekani means sehemu ya mavuno yao ndio yameletwa huku, sasa wewe unataka wauze huko halafu walete hela wanunue mchele wa huku nani atakubali upuuzi huo, yaani mfano mnataka kupewa msaada na kampuni ya magari halafu tuwaambie hatutaki magari yenu uzeni huko halafu mlete hela tukanunue magari mengine.
 
Lengo la msaada likiwa zuri hakuna sababu ya kukataa msaada, dunia nzima wanaishi hivyo
Hivi mtu mweupe ana lengo zuri na nyani kweli,hivi hujasoma history Kama vipi nenda kwao kaishi nao ndio utaona Kama wanakupenda.
Unajua wale wale black Americans wanachowafanya lakini
 
Mada hii ni kuelezea mashaka makubwa niliyonayo kwa Waziri wetu wa kilimo namna maamuzi yake yanavyoweza kuharibu mahusiano ya kimataifa kama asipojirekebisha.

Kwanza kabisa nianze Kwa 'declare interest' ,Sina mahusiano ya aina yoyote na NGO iliyoleta mchele wa msaada wenye virutubisho kutoka nchini Marekani chini ya kampeni ya wizara ya kilimo ya Marekani inayoitwa "Pamoja tuwalishe" na 'interest' pekee niliyonayo ni Kwa maslahi mapana ya nchi yangu .

Siku zote mjumbe hauawi na hiyo NGO inabaki kuwa ni mjumbe tu wa wizara ya kilimo ya Marekani ,kitendo Cha Waziri kuonesha kukasirishwa na kitendo Cha mjumbe kinaleta picha isiyopendeza.

Kwa mtazamo wangu badala ya Waziri Bashe kuonesha kukasirishwa na kuletwa Kwa mchele na hiyo NGO angetumia nafasi hiyo kufanya "formal communication" na wizara ya kilimo ya Marekani juu ya mambo tunayohitaji.

Kwa kuwa mchele huo ni msaada sikuona ulazima wowote wa Waziri kusema kwamba mchele tunao ,Kwa kuwa lengo la kampeni hiyo ni zuri ,tunatakiwa kuupokea msaada huo na kushukuru na wizara ingetumia TBS kuchunguza ubora wa mchele huo kimya kimya kabla haujaanza kutumika na kama kungekuwa na mashaka yoyote Serikali ingekataa baada ya kufanyika Kwa uchunguzi na ubora na sio Kwa hoja za Waziri.

Mashaka niliyonayo kwa Waziri Bashe ni kuwa:

Kama Waziri hajui athari za kimahusiano zinazoweza kuibuka kutokana na kauli tu. Kitendo Cha Waziri Bashe kudai Kwa nini wasingeleta virutubisho wachanganye tukiwaona ,sio rafiki Kwa afya ya diplomasia. Kitendo hicho kinaweza kufikirika kama tuhuma ya usalama. Kabla ya kauli hiyo alitakiwa kuwatumia TBS kuuchunguza mchele.

Marekani ni Moja ya nchi zinazozalisha nataka ( mchele na mahindi) Kwa wingi duniani na kutokana na mabadiliko ya hali ya hewa ,nchi yetu inaweza kukumbwa na baa la njaa na tukahitaji msaada wa Chakula kutoka nje. Je, tutapata wapi nguvu za kuomba msaada kutoka Marekani kama tumeamua kukataa msaada Sasa ?

Pengine kulikuwa na Cha zaidi ambacho hatukijui lakini kama ni hiki kilichopo ,ni vema Waziri Bashe angeliendea suala Hilo Kwa busara, angejiridhisha kwanza na angejua hatua Kwa busara ili tuendelee kuimarisha mahusiano na nchi nyingine.

Kila siku Rais anasisitiza mifumo kusomana ili kuepusha migogoro , na kama mifumo ingekuwa inasomana kusingekuwa na kauli za namna Ile kutoka Kwa Waziri.

Ahsante
Bashe kafanya the right thing,I support him 100%.It seems sio agent wa the CIA.TBS sio trustworthy kabisa,ni already captured by the American government.Keep it up Bashe,unawafaa Watanzania.
 
Tanzania Ina shule zaidi ya 300, nani anazilisha hizo zingine nje ya hizo 300?
Kama Kuna shule 10 na kati ya hizo shule Moja ina uhitaji mkubwa sana wa walimu na vifaa vya kufundishia kuliko zingine, ukitaka kupeleka walimu utaanza na zipi?
 
Kama Kuna shule 10 na kati ya hizo shule Moja ina uhitaji mkubwa sana wa walimu na vifaa vya kufundishia kuliko zingine, ukitaka kupeleka walimu utaanza na zipi?
Hakuna popote Tanzania imewahi kutangaza crisis ya chakula kwa shule zake. Tulifikaje hapa?
 
Huna akili

Msaada umetolewa na wakulima wa Marekani means sehemu ya mavuno yao ndio yameletwa huku, sasa wewe unataka wauze huko halafu walete hela wanunue mchele wa huku nani atakubali upuuzi huo, yaani mfano mnataka kupewa msaada na kampuni ya magari halafu tuwaambie hatutaki magari yenu uzeni huko halafu mlete hela tukanunue magari mengine.
Kwa hiyo NGO imekuwa wakulima wa Marekani? Ng'ombe ww!
 
Kwa hiyo misaada wa mchele utashusha bei? Na sio kuwezesha wakulima Kwa dhana,na ujuzi wa kisasa Ili uzalishaji uongezeke bei ipungue,!?
Hapa suala kwa sasa kwanza ni watoto mashuleni wasishinde njaa au kuona ubwabwa ni anasa, pia kutegemea na ukubwa wa msaada bei inaweza kushuka.
Pia Marekani na mataifa mengine ya Magharibi yanasaidia sana bajeti ya nchi yetu, wanatoa misaada na scholarships.
Tatizo pesa zetu za bajeti zinaenda kununulia maV8 na pia hao wataalamu wanaosomeshwa wakija hawapewi mazingira mazuri na wezeshi ya kufanya kazi husika za kilimo.
 
Hapa suala kwa sasa kwanza ni watoto mashuleni wasishinde njaa au kuona ubwabwa ni anasa, pia kutegemea na ukubwa wa msaada bei inaweza kushuka.
Pia Marekani na mataifa mengine ya Magharibi yanasaidia sana bajeti ya nchi yetu, wanatoa misaada na scholarships.
Tatizo pesa zetu za bajeti zinaenda kununulia maV8 na pia hao wataalamu wanaosomeshwa wakija hawapewi mazingira mazuri na wezeshi ya kufanya kazi husika za kilimo.
Kwani Dodoma ndio watoto wanashinda njaa tu?
 
Hivi mtu mweupe ana lengo zuri na nyani kweli,hivi hujasoma history Kama vipi nenda kwao kaishi nao ndio utaona Kama wanakupenda.
Unajua wale wale black Americans wanachowafanya lakini
Waziri wa Ulinzi wa Marekani ni Black
Mkuu wa majeshi wa Marekani ni Black
Balozi wa Marekani nchini ni Black.
 
Back
Top Bottom