Waziri ang’ang’ania Muungano wa Mkataba.

Gumzo

JF-Expert Member
Jan 2, 2012
211
7
[h=3][/h] WAZIRI wa Nchi Ofisi ya Rais Asiye na Wizara Maalumu, Mansour Yussuf Himid amesema CCM haijazuia wanachama wake wakiwamo wajumbe wa Baraza la Wawakilishi, kutoa maoni yao kuhusu mchakato wa Katiba unaoendelea sasa.
Akizungumza katika mahojiano na Sauti ya Ujerumani (DW) katika ukumbi wa Baraza Chukwani jana, Mansour alisema kila mwanachama wakiwamo viongozi, wako huru kutoa maoni kuhusu Katiba na chama hakijazuia mtu kutumia haki hiyo.
“Katiba ya CCM iko wazi haikatazi mwanachama wake kutoa maoni tofauti kuhusu mchakato wa Katiba ambao uko wazi pia,” alisema Mansour.
lisema CCM mkoa wa Mjini Magharibi haina uwezo wa kikatiba kunyamazisha wanachama wake kutoa maoni ya Katiba katika zama hizi za uwazi na demokrasia.
CCM Mjini Magharibi hivi karibuni ilitoa onyo kali kwa baadhi ya viongozi wa chama hicho wakiwamo wajumbe wa Baraza la Wawakilishi wanaotaka kuwapo muundo wa Muungano wa Mkataba ambao unakwenda kinyume na sera za chama hicho na kusema kitawanyang’anya kadi zake.

KWA HABARI KAMILI BOFYA HAPA GUMZO LA JIJI
 
Aisee muungano ukivunjika sijui itabidi wazenji muanzishe jamii forum yenu maana hii ni ya watanganyika...au moderator wa humu ndani waanzishe ki sub forum cha zenji na maswala ya kwao ka mlivofanya kwa wakenya maana wazenji washasema sio watanzania wao
 
Kwanza napenda kutanguliza shukrani kwa Allah S.W kwa kuniwezesha na kuwawezesha wasomaji wa mtandao huu afya njema na busara na hekima.

Mh. M. Y. Himidi nasema na nitamuita jamadari mwenye kuipigania Zanzibar huru yenye mamlaka kamili asiyeogopa vitisho na mwenye msimamo wa kijanadume. Huyu ndio mfano wa kiongozi na mzanzibar kindaki ndaki mwenye msimamo. Hana tafauti na hayati A.A.Karume,
Mh.Mansour sisi tuliokuwa nje na ndani ya Zanzibar tunakuunga mkono na tuko pamoja na wewe, na hao wanaokutisha kwamba urejeshe kadi ya chama, sasa sio wakati wa kuzungumzia chama ni wakati wa kuzungumzia Zanzibar huru yenye mamlaka kamili.

Suala la kudai Zanzibar yenye mamlka kamili haikuanzia na Mansour labda tujikumbushe kidogo. Muasisi wa Taifa la Zanzibar, jemedari wa Mapinduzi matukufu ya 1964, Hayati Mzee Abeid Amani Karume alipokwenda kwa Nyerere mwaka 1970 na kikosi chake cha Baraza la Mapinduzi alifanya kama anavyofanya Mansour leo. Karume akiungwa mkono na baraza zima la Mapinduzi aliwasilisha kwa Nyerere hati ya kudai mambo 4 ambayo ni ulinzi, uraia, sarafu na mambo ya nje, Nyerere akamjibu Karume wakati ukifika nitakwita rudini kwnza mzee. Baada ya hapo hawakuzungumza hata neno moja baina yao kila mmoja alikuwa mkali kwa upande wake na hana hamu na mwenzake. Kilichofuatia ni kifo cha Nyerere ambapo wazanzibari wengi wanaamini aliuwawa kwa mipango ya Nerere.
Mzee Aboud Jumbe aliyekewa Rais wa Pili wa Zanzibar alitaka mabadiliko makubwa ya muundo wa muungano ili yakubaliane ya mfumo wa mamlaka tatu zilizotajwa katika makubaliano ya muungano lakini pamoja na Urais wake wa Zanzibar na umakamo mwenyekiti wa CCM, Nyerere alitumia kauli ndogo ya kumwambia Jumbe ajiuzulu. Kosa hili ni la kutaka kuipatia Zanzibar mamlaka yake kamili katika muungano. Wengine wengi yamewakuta kama hayo na zaidi ya hayo tena katika CCM sio upinzani.
Unajua kwa nini jitihada hizi hazikuzaa matunda? Wazanzibari walikuwa wamegawanyika makundi kila kundi linamhofu mwenzake kuwa anaweza kupata mwanya wa kutimiza uadui wake. Sasa niwadokeze wasiojua......yaleeeeeeeee maridhiano ya wazanzibari na kuundwa serikali ya umoja wa kitaifa ndio lilikuwa lengo lake. Wanaovutana wakae pamoja, wafanye kazi pamoja, waaminiane, wadai Zanzibar yao yenye mamlaka kamili. Yametimia. Hiyo ya muungano wa MKATABA wasiojua wafahamu si msimamo wa Mansour ni msimamo wa SMZ. Kwani uko wazi hebu wasikilizeni mawaziri, hebu msikilizeni mwanasheria mkuu wa SMZ. Wenzetu wakitaka tutakuwa na muungano utakaozipa nchi zetu mamlaka kamiliwamekataa kila mtu kwake.

Wanazungumza sera ambazo zimepitwa na wakati, mawazo yao na fikra zao ni za miaka ile ya kumezwa na Nyerere sio za mwaka 2012/13. Ni watu wa kupuunzwa, kwanza wapo wachache hapa Zanzibar, ni watu wenye chuki dhidi ya CUF na wapemba, ni watu wenye kupigania maslahi binafsi, ni watu wenye kupendelea dhulma, ni watu wenye fikra ambazo haziendani na wakati, ni watu wenye kufikiria kuwa DIVIDE AND RULE ndio silaha.


Mh. Mansour kuna vikwazo na vitisho vingi vitajitokeza lakini tunakuhakikishia ni wachache mno, wazanzibari tulio wengi tunakuunga mkono, tuko pamoja na wewe na wengine wote wenye msimamo kama wako wa kutetea maslahi ya Zanzibar na watu wake.


Huu sio wakati wa kutishana na kuoneana haya, kama ulivyozungumza msimamo katika msimamo wako humuogopi mtu na uko na REASON ndio maana unasema hivyo ambavyo unaendelea na utaendelea kusema ukiwa ndani ya chama au hata nje ya chama. Na watafukuza wangapi maana huu ni msimamo wa serikali nzima wengi hawajatamka tu na karibuni watatamka.


Nitawapa ushahidi kuwa Muungano wa MKATABA ni msimamo wa serikali ya SMZ. Utowaji wa maoni umekamilika Mkoa wa kusini Unguja ambapo CUF haina kiti hata cha boksi. Moa huu ndio uliongoza katika kupiga kura ya hapana wakati ule Amani Karume hajaeleweka na kura ya NDIO ikapata zaidi ya asilimia 70 katika mkoa huu. Nawaomba wasomaji waangali matokeo ya utowaju maoni yalivyokuwa katika tume ya warioba ndani ya mkoa huo wataamini kuwa MKATABA ni msimamo wa SMZ na ushafanyiwa kazi.

UTOLEWAJI WA MAONI MKOA WA KUSINI UNGUJA, TUME YA MABADILIKO YA KATIBA
s/n
tarehe
shehia
ser2
ser3
Mkataba
NoMuungano
wasofahamika
1.
2/7
mzuri/maku-nduchi
20
0
50
0
0
2.
2/7
mtende
40
0
25
0
0
3.
3/7
kibuteni
2
1
3
0
0
4.
3/7
Mich-amvi
17
0
15
0
3
5.
4/7
kizimkazi mkunguni
5
1
27
0
0
6.
4/7
kizimkazi dimbani
24
0
23
0
0
7.
5/7
kitogani
38
0
11
0
0
8.
5/7
muyuni
16
0
47
0
0
9.
6/7
jambiani
55
0
44
0
0
10.
6/7
paje/bwejuu
25
0
46
0
8
11.
7/7
Maku-nduchi/kijini
78
0
39
2
2
12.
7/7
Kajengwa
69
0
48
2
2
13.
8/7
mwera/koani
142
0
26
1
0
14.
8/7
kiboje/ndagaa
136
0
11
0
1
15.
9/7
ndijani/dunga
59
0
108
0
2
16.
9/7
Ukon-Goroni
47
0
57
0
1
17.
10/7
bambi/mpapa
66
0
18
0
3
18.
10/7
pagali
34
0
3
0
3
19.
11/7
uzini
136
5
40
0
0
20.
11/7
Mcha-Ngani
57
0
20
0
0
21
12/7
Chwaka
77
0
279
3
2
22
12/7
uroa/marumbi
82
0
22
0
1
23
13/7
bungi/tunguu
113
0
143
0
0
24
13/7
u/ukuu/kaebona
63
0
50
7
3
25
14/7
u/ukuu/kaepwani
61
3
48
0
6
26
14/7
uzi
51
0
208
0
0
total
1513
10
1421
15
37
%
50.5
0.3
47.4
0.5
1.2


ZANZIBAR HURU YENYE MAMLAKA KAMILI KWANZO VYAMA BAADAE.
Nawashukuru wote wasomaji wa hii mada.
 
Leteni hoja bungeni ya kuvunja muungano!! hata sisi wamlima tumechoshwa nanyi!!

Assalaam Aleykum wana JF,Mi nashangazwa sana na hawa jamaa zetu wa znzb,wao kila siku wanasema wamechoka na muungano,mbona siye watanganyika ndo tumechoka kabisa,sisi hatutaki hata huo muungano wa mkataba si tunataka kila m2 kivyake wa bara wote ambao hata 200 hawafiki wanaoishi znzb warudi kwao na wazenji wote waliokwetu bara warudi kwao znzb hata kama walizaliwa huku warudi kwao,hatuwataki.insikitisha sana kuona waznzb wanalalamika wakati serikali yao sasa ni kama nchi ina kila ki2 hadi inapata misaada separately toka marafiki zao wa nje kama sisi tunavyopata lkni bado wanasema tunawanyonya kivipi sasa?ukiona hawendelei ujue hata wakitengana hawataaendelea sababu sasa ni kama nchi kamili,halaf inashangaza kuona kwamba wanaolalamika wote ukiangalia wanaishi bara wamesoma bara,na wameomba kazi na wameajiriwa na taasisi za bara pia inasikitisha sana,kama unachukia ki2 kwanini usikiache kazi mwache mrudi kwenu mkaijenge nchi yenu jamani inashangaza kuona wapemba wote wamejenga bara hawajajenga kwao,halaf wanang'ang'ania kuvunja muungano,mi nasema hvi znzb nchi nzima wakiandamana kukataa muungano,dunia itasikia na tutatengana sasa kwanini hamfanyi hivyo jamani?,msiogpe kupigwa risasi kwani hakuna kiongozi mjinga kuweza kuamuru mauaji ya halaiki sababu wanajua kabisa wakifanya hivyo THE HAGUE inawaita,dunia ya sasa tofauti na ile ya 2001,hawawezi kuua zaidi ya wa2 kumi wanaoandamana kwa amani kudai uhuru wao wa haki halafu wakaachwa hvi hvi,ni lazima watawajibishwa tu.sasa msiongee sana waznzbr sisi watanganyika tunataka vitendo tu,tunataka kutumia haya maoni ya kikatiba iitishwe referendum mupate nchi yenu manung'uniko yaishe.
mana sasa huu muungano hautufai tena kwani sasa tumekuwa hatuaminiani kabisa,na hata kwenye ndoa unapoona wewe na mke wako hamwaminiani hata kuogopa kula chakula basi hakuna budi kuvunja ndoa mana hamna usalama hapo.
siku hizi wanasema karume alikuwa mwanaume wa shoka hivi ni kweli hayo jamani au ni kwasababu wanaosema hvyo ni watoto wa juzi tu hajakuwepo wakati huyu bwana anatawala?wakati znzb was run as a police state.hawakumbuki kwamba ni karume huyu huyu mwaka 1966 alitangaza anatawala znzbr kwa miaka 50 bila kufanya uchaguzi?kama angekuwa hai angemaliza uchaguzi mwaka 2014,hawakumbuki ni karume huyu huyu alikataza waznzbr kusoma vyuo vikuu ktk utawala wake? mpaka alipokuja maalim sefu ndo alianza kuleta sera za waznzbr kusoma hasa udsm wakati anatawala huyu bwana ilikuwa marufuku kupata skolaship kwenda kusoma nje,hasa hasa wapemba.hawakumbuki kuwa n karume huyuhuyu ndiye aliyewacharaza viboko wapemba kwa kumwifazi sultani mpaka wapemba wakakimbilia bara kutafuta salama yao nyerere akawapokea nasasa wanahozi ardhi bara na wamekufanya nymbani hawataki kurudi kwao.
ni karume na kamanda wake seu bakari ndo waliokuwa wanakugongea usiku kama saa tatu kama wana wasiwasi na wewe na ukishaondoka tu basi ndugu zako ndo hawakuoni tenaaa.jikumbusheni historia kabla hamjazungumza,karume alikataa hadi msaada wa wanasheria toka bara kwa kusema ni waongo kwa kumtetea m2 wanayedhani kabisa kakosa,alianzisha mahakama za zake za kangaroo ambazo sifa ya wewe ili uwe hakimu inabidi usiwe na ujuzi wa sheria yeyote na ikiwezekana kabisa usiwe unajua kusoma kabisa na karibia wote walikuwa hawawezi hata kuandika kabisa.

 
Aisee muungano ukivunjika sijui itabidi wazenji muanzishe jamii forum yenu maana hii ni ya watanganyika...au moderator wa humu ndani waanzishe ki sub forum cha zenji na maswala ya kwao ka mlivofanya kwa wakenya maana wazenji washasema sio watanzania wao

siyo waanzishe yao tu bali tunataka waudi kwao na sisi hatuwatakiii.mbona sisi haturuhusiwi kujenga znzb wala kuishi jamani?wameanzisha kitambulisho cha utaifa wao wanakiita kitambulisho cha ukaadhi spesho kuwazuia wabara wasiiingie kwao sasa wao mbona wanakuona kwe2 kutamu kwao wanakatazia jamani? Wapembaa wote mnaoishi bara tunawaomba jamani anzeni kuuza viwanja vyenu murudi kwenu hatuwataki tumewachoka na kelele zenu.
 
Maoni ya muundo ya Muungano ya Wanzanzibari

Serikali 2 = 50.5%
Serikali 3 = 0.3%
Mkataba 47.4%
No Muunagano = 0.5%
Wasiofahamu = 1.2%


I can't BELIEVE hivi SERIKALI 2 Bado ndiyo changuo la wazanzibari? Kumbe kelele zote za UAMUSHO ni bure?

BTW, ungetuwekea pia wanaotaka SERIKALI MOJA hata kama ni 0% It is a data.
 
Maoni ya muundo ya Muungano ya Wanzanzibari

Serikali 2 = 50.5%
Serikali 3 = 0.3%
Mkataba 47.4%
No Muunagano = 0.5%
Wasiofahamu = 1.2%


I can't BELIEVE hivi SERIKALI 2 Bado ndiyo changuo la wazanzibari? Kumbe kelele zote za UAMUSHO ni bure?

BTW, ungetuwekea pia wanaotaka SERIKALI MOJA hata kama ni 0% It is a data.


sisi wabara tunasikitika sana kuona hvi sisi tunaona muungano hautufaidishi zaidi ya manung'uniko tu,sasa wa2sikilize na sisi wabara tusiotaka muungano,uvunjeni muungano nanyi mrudi kwenu muanze kuuza kabisa viwanja na nyumba zenu mrudi home chake chake mkakujenge jamani.
kama znzb inarudishwa nyuma na bara basi huu ndo wakati mwafaka kuandamana hadi tutengane znzb nzima ikiandamana mtapata tu uhuru wenu labda muwe hamtaki wenyewe huo uhuru hakuna anayeweza kutawala asipokubalika siku moja.hamna haja enyi wapemba kujenga kwa m2 ambaye mnamchukia kwa uafrika wake,kwa maana hyo rudini kwenu mtakapokuwa wenyewe wapemba na waunguja watupu na m'bara akijipendekeza kwenu mkateni hata mapanga akija chakechake hiyo itakuwa ni ruksa.

 
Nafikiri ni wakati wa kuvunja muungano. Huo wa mkataba hatuutaki sisi watanganganyika. Wazenji rudini kwenu kabla na sisi hatujaanza kuwaletea fujo
 
Ninyi watanganyika wacheni unyonge mbona tunakuwa hivi? Tuelezeni ukweli ni ipi faida ya muungano kwetu wa bara?Mbona hakuna mtu hata mmoja anayenieleza faida ya muungano kwetu sisi wa bara.Naomba saana watu wa bara kabla hatuja walaumu wenzetu wa znz hebu tuziainishe kwanza faida za muungano kwa sisi wa bara na hapo tuone tunafanyeje.Ninaamini kabisa kuwa hata hao mawaziri hawajui kabisa sisi wa bara tunafaidika nini na huu muungano.Jamani ee,muda wa kumuiga nyerere umepita sasa inatakiwa tuanze upya ninyi wa bara,nyerere ndiye mtu pekee ambaye anajua siri kuu ya muungano huu.Faida za muungano kama zipo zimepitwa na wakati kwani zilikuwa muhimu enzi za vita baridi na sio sasa,hivyo kumuezi nyerere kwa sababu za kijinga hakuna maana yoyote kwa mtanganyika wa wakati huu. Watu wa bara tuamke sasa na tusiwe mazezeta na tuhoji wazi wazi faida za muungano kwa viongozi wetu na kama hawatuambii kweli kweli hizo faida za muungano basi kweli sisi wa bara tunawazurumu wa znz hivyo wa znz wanayohaki ya kulilia nchi yao.Nawaomba wana jf kama kuna mtu yoyote anayojua faida za muungano kwa watanganyika basi azilete na tuzione uzito wake.
 
Assalaam Aleykum wana JF,Mi nashangazwa sana na hawa jamaa zetu wa znzb,wao kila siku wanasema wamechoka na muungano,mbona siye watanganyika ndo tumechoka kabisa,sisi hatutaki hata huo muungano wa mkataba si tunataka kila m2 kivyake wa bara wote ambao hata 200 hawafiki wanaoishi znzb warudi kwao na wazenji wote waliokwetu bara warudi kwao znzb hata kama walizaliwa huku warudi kwao,hatuwataki.insikitisha sana kuona waznzb wanalalamika wakati serikali yao sasa ni kama nchi ina kila ki2 hadi inapata misaada separately toka marafiki zao wa nje kama sisi tunavyopata lkni bado wanasema tunawanyonya kivipi sasa?ukiona hawendelei ujue hata wakitengana hawataaendelea sababu sasa ni kama nchi kamili,halaf inashangaza kuona kwamba wanaolalamika wote ukiangalia wanaishi bara wamesoma bara,na wameomba kazi na wameajiriwa na taasisi za bara pia inasikitisha sana,kama unachukia ki2 kwanini usikiache kazi mwache mrudi kwenu mkaijenge nchi yenu jamani inashangaza kuona wapemba wote wamejenga bara hawajajenga kwao,halaf wanang'ang'ania kuvunja muungano,mi nasema hvi znzb nchi nzima wakiandamana kukataa muungano,dunia itasikia na tutatengana sasa kwanini hamfanyi hivyo jamani?,msiogpe kupigwa risasi kwani hakuna kiongozi mjinga kuweza kuamuru mauaji ya halaiki sababu wanajua kabisa wakifanya hivyo THE HAGUE inawaita,dunia ya sasa tofauti na ile ya 2001,hawawezi kuua zaidi ya wa2 kumi wanaoandamana kwa amani kudai uhuru wao wa haki halafu wakaachwa hvi hvi,ni lazima watawajibishwa tu.sasa msiongee sana waznzbr sisi watanganyika tunataka vitendo tu,tunataka kutumia haya maoni ya kikatiba iitishwe referendum mupate nchi yenu manung'uniko yaishe.
mana sasa huu muungano hautufai tena kwani sasa tumekuwa hatuaminiani kabisa,na hata kwenye ndoa unapoona wewe na mke wako hamwaminiani hata kuogopa kula chakula basi hakuna budi kuvunja ndoa mana hamna usalama hapo.
siku hizi wanasema karume alikuwa mwanaume wa shoka hivi ni kweli hayo jamani au ni kwasababu wanaosema hvyo ni watoto wa juzi tu hajakuwepo wakati huyu bwana anatawala?wakati znzb was run as a police state.hawakumbuki kwamba ni karume huyu huyu mwaka 1966 alitangaza anatawala znzbr kwa miaka 50 bila kufanya uchaguzi?kama angekuwa hai angemaliza uchaguzi mwaka 2014,hawakumbuki ni karume huyu huyu alikataza waznzbr kusoma vyuo vikuu ktk utawala wake? mpaka alipokuja maalim sefu ndo alianza kuleta sera za waznzbr kusoma hasa udsm wakati anatawala huyu bwana ilikuwa marufuku kupata skolaship kwenda kusoma nje,hasa hasa wapemba.hawakumbuki kuwa n karume huyuhuyu ndiye aliyewacharaza viboko wapemba kwa kumwifazi sultani mpaka wapemba wakakimbilia bara kutafuta salama yao nyerere akawapokea nasasa wanahozi ardhi bara na wamekufanya nymbani hawataki kurudi kwao.
ni karume na kamanda wake seu bakari ndo waliokuwa wanakugongea usiku kama saa tatu kama wana wasiwasi na wewe na ukishaondoka tu basi ndugu zako ndo hawakuoni tenaaa.jikumbusheni historia kabla hamjazungumza,karume alikataa hadi msaada wa wanasheria toka bara kwa kusema ni waongo kwa kumtetea m2 wanayedhani kabisa kakosa,alianzisha mahakama za zake za kangaroo ambazo sifa ya wewe ili uwe hakimu inabidi usiwe na ujuzi wa sheria yeyote na ikiwezekana kabisa usiwe unajua kusoma kabisa na karibia wote walikuwa hawawezi hata kuandika kabisa.

sasa kama na wewe muungano umekuchosha kama ulivyowachosha wao, BUNGE SI LIPO HAPO DODOMA, SI Uungane nao kwenda BUNGENI kuuvunja? Haya masuala unayoyapublicise ya kangaroo korti, na viboko vya karume (aliyekufa) and blah blah and blah blah yanaonesha ulivyo mnafiki.

Kwa sababu karume alipiga viboko wapemba (lakini hata waunguja walipata joto ya jiwe wakati wa karume) ndio sababu ya kutosha kuwa muungano uendelee hadi kiama hata kama ulishapoteza maana ya kuwepo kwake?

Makala ndefu hii uliyoiandika na upuzi unaouongea inaonesha ni kiasi gani bado mtanganyika ulivyo kuwa na ndozo za kuendelea kuitawala zanzibar. TUMEAMSHWA, TUMEAMKA
 
Maoni ya muundo ya Muungano ya Wanzanzibari

Serikali 2 = 50.5%
Serikali 3 = 0.3%
Mkataba 47.4%
No Muunagano = 0.5%
Wasiofahamu = 1.2%


I can't BELIEVE hivi SERIKALI 2 Bado ndiyo changuo la wazanzibari? Kumbe kelele zote za UAMUSHO ni bure?

BTW, ungetuwekea pia wanaotaka SERIKALI MOJA hata kama ni 0% It is a data.

"believe it! hayo ni maoni ya mkoa wa kusini unguja tu, mkoa mmoja kati ya mikoa mitano ya zanzibar, sikiliza maoni toka mikoa mengine, infact hata sisi wenyewe tumeshangazwa na matokea hayo kuwapo 47.4% ya wanaotaka muungano wa mkataba!?"

 
Aisee muungano ukivunjika sijui itabidi wazenji muanzishe jamii forum yenu maana hii ni ya watanganyika...au moderator wa humu ndani waanzishe ki sub forum cha zenji na maswala ya kwao ka mlivofanya kwa wakenya maana wazenji washasema sio watanzania wao

"kumbe watanganyika mpo? mi nilifikiri ni watanzania ati, kwa maana hadi sasa nasi ni watanzania upande mmoja (hadi hapo tutakapouvunja muungano) ila tunajivunia kwanza kwa uzanzibari wetu, na kwa vile nyinyi hamna utanganyika tutaendelea kubanana humu humu, kwa taarifa tu sisi tunyo mikumbi mingi tu ya kijamii, special for zanzibaris, wewe huruhusiwi kuingia/kujiunga, yaani hivi tunavyozungumza"
 
Back
Top Bottom