Josephine03
JF-Expert Member
- Feb 7, 2012
- 752
- 302
Hivi wewe kila kitu ni lazima uchangie?****.
Wagonjwa wa akili humu ndani pia wamo msamehe bure M4C hiyo ndo dalili za dozi yake kufanya kazi
Hivi wewe kila kitu ni lazima uchangie?****.
tarehe 26/04/2012 kupitia forum hii nilitangaza mkutano wa kusimika mabalozi wa chadema kijiji cha nkwini kata ya makanya wilaya ya same na niliomba kusaidiwa kadi 500 na bendera 50 za cdm kutoka uongozi wa taifa. Ninafuraha kuwajuza kuwa mkutano ulifanyika kama ulivyopangwa tar 29/04 na nilipata kadi na bendera . Katika hali ya kustaabisha wazee wakitongoji cha nkwini kata ya makanya wilayani same wameng'ang'ania kadi chache za chadema na kulaani ccm kwa kuwapotezea matumaini yao na vizazi vyao kwa muda wa miaka 50. Wamesema jimbo la same magharibi limekuwa wazi tangu uchaguzi upite 2010. Hii nikutokana na mbunge wao david matayo kutofanya chochote tangu wa mchague, huku akiacha udongo aina ya boxite ukisafirishwa toka chome kwenda kenya bila wananchi kunufaika. Wameelezea kero zao kuwa ni pamoja na migogoro ya ardhi, shule kukosa choo, kukosa dispensar, maji, na ujira mdogo wanaolipwa kama vibarua katika shamba la mkonge. Wazee hao wamewataka viongozi wa chadema kujipanga vizuri ili kuchukua jimbo la same magharibi ambao kwao wanaona kama liko wazi. Hapa nime attach picha ya mzee wa miaka 80 akipokea kadi ya chadema baada ya kurudisha ya ccm. Mkutano ulifanywa na mwanaharakat godson mbaga (0752225501)
Mtoa mada heshima yako kamanda(kama ni kweli ulivyojitambulisha) nina maswali mawili ambayo yananifanya mimi niamue kutokukubaliana na habari yako uliyoitoa hapa zaidi ukikilaumu chama kwa kukutumia vifaa vichache vya uenezi tofauti nan maombi yako.
Kwanza,kama ulijishughulisha namna hiyo mpaka kuomba makao makuu wakutumie bendera na kadi ni dhahiri kuwa wewe ni kiongozi kwenye level flani ndani ya chama,hivyo unaielewa vizuri katiba,sheria na utaratibu wa kufanya mambo ndani ya chama.kwamba suala la chama kutokukutumia bendera na kadi kiasi ambacho ulikuwa unahitaji halikuwa suala la kuliongelea hapa JF.hayo mambo ulitakiwa uyafikishe kwa wahusika ndani ya chama chako.Hapa wanaJF hakuna aliyekuwepo au aliyesikia maombi yako wakati unahitaji hivyo vifaa,na wala hukutumia JF kupeleka maombi yako ya kuhitaji bendera na kadi.sasa sioni kama ni hekima ukijidai kuongelea issues ambazo hazituhusu sisi members wa JF.wananchi wanataka kusikia habari za ukuaji wa chama na sio habari za kushutumiana ndani ya uongozi wa chama.peleka shutuma zako panapo husika kwa muujibu wa sheria na utaratibu mnaoufuata manake ukiongelea hapa hutakaa upate solution yake.
Pili,kwamba kama kweli ulikuwa na uhakika ungeweza pata watu wengi namna hiyo wa kuwapa kadi na kutumia bendera zote hizo kijijini kwako hapo,lazima pia ulitakiwa uwe na vidhibitisho vya kufanya makao makuu wakuelewe zaidi.suala la kuhisi au kufikiria unaweza kugenerate watu wengi namna hiyo halina msingi wowote.uelewe kwamba kwa jinsi chama kinapanuka kwa kasi ya ajabu sio wewe tu unayehitaji vifaa vya uenezi vya bure.ni kila sehemu Tanzania nzima.
Ukisema wewe ni kamanda wa kweli lakini ushaanza kutoa shutuma sehemu ambazo hutakiwi kuzitoa,basi jua yatakupata yaliyowapata jamaa wale wa CUF na NCCR Mageuzi.Be blessed!
Uongozi Jimbo na mkoa wanafuatilia kadi! Ivyo tunasubiri toka juu
Tarehe 26/04/2012 kupitia forum hii nilitangaza mkutano wa kusimika mabalozi wa CHADEMA kijiji cha Nkwini Kata ya Makanya Wilaya ya Same na niliomba kusaidiwa kadi 500 na bendera 50 za CDM kutoka uongozi wa Taifa. Ninafuraha kuwajuza kuwa mkutano ulifanyika kama ulivyopangwa tar 29/04 Na nilipata kadi na bendera . Katika hali ya kustaabisha wazee wakitongoji cha Nkwini Kata ya Makanya wilayani Same wameng'ang'ania Kadi Chache za CHADEMA na kulaani CCM Kwa kuwapotezea matumaini yao na vizazi vyao kwa muda wa miaka 50. wamesema Jimbo la Same Magharibi Limekuwa wazi tangu uchaguzi upite 2010. Hii nikutokana na Mbunge wao David Matayo kutofanya chochote tangu wa mchague, huku akiacha udongo aina ya boxite ukisafirishwa toka Chome kwenda Kenya bila wananchi kunufaika. wameelezea kero zao kuwa ni pamoja na migogoro ya Ardhi, Shule kukosa Choo, kukosa Dispensar, Maji, na ujira mdogo wanaolipwa kama vibarua katika shamba la Mkonge. Wazee hao wamewataka Viongozi wa CHADEMA Kujipanga vizuri ili kuchukua Jimbo La Same Magharibi ambao kwao wanaona kama liko wazi. Hapa nime attach picha ya mzee wa miaka 80 akipokea kadi ya CHADEMA baada ya kurudisha ya CCM. Mkutano ulifanywa na mwanaharakat Godson Mbaga (0752225501)
nimeipenda juhudi yako kaka, hata mwenyekiti wa bavicha katika kufungua tawi la CDM chuo cha st. john dar alitudokezea kuwa sisi vijana tunakiwa kukisaidia chama maake vijiji vya tanzania ni vingi mno vyapata kama 20,000. Let's keep on creating awareness on the issue