Wazazi tuchukue tahadhari, Tusomeshe watoto sambamba na kuwaandaa waweze kujiajiri ama kufanya biashara, degree/masters zinawaaibisha watu mitaani

sky soldier

JF-Expert Member
Mar 30, 2020
5,408
19,033
Ni wazi kabisa bila kupepesa macho lengo kuu la wazazi wa Tanzania ni kusomesha mtoto ili aje kupata ajira serikalini.

Ajira zinazidi kuwa adimu sana, wanafunzi wengi wanahitimu vyuo na vyuo vipo vingi sio kama zamani, wahitimu wamekuwa wengi sana lakini ajira haziongezeki.

Wanaoajiriwa ni wachache sana, wanaobaki mitaani baada ya kuona hakuna matumani ya ajira mwisho wa siku wanakubaliana na matokeo na wengi wao huishia kujiajiri ama wafanye biashara, wengi huanza kufanya shughuli hizi bila uzoefu kwasababu walitumia muda mwingi shuleni, matokeo yake ugeni wao unaweza kuchangia shughuli zao ziwe na changamoto na hata kufilisika kwa kukosa uzoefu.

Wengine wana degree zao wanaamua kufanya kazi za elf 80 kwasababu hawajui kitu kingine zaidi ya elimu ya darasani, hawana skills zozote walizowahi kujifunza nje ya darasa na hawana uzoefu wowote wa kufanya biashqra, hapa ndio wengi hudhalilika "fulani ana degree lakini anafanya kazi ya laki 1"

Nitoe rai kwa wazazi wenye biashara ama waliojoajiri kwa skills wawe bega kwa bega na watoto wao waweze kuwamegea uzoefu wao kwenye shughuli zao, mfundishe mtoto kusimamia biashara, mfundishe kodi zinalipwa wakati gani, supplier yupo wapi, jinsi ya kufungua biashara, jinsi ya kukwepa changamoto za ugeni wa biashara, n.k. itamsaidia sana kwasababu wewe mzazi ulishapitia changamoto kibao unamtafunia asizirudie, hapo mbele akikosa ajira aweze kufanya biashara.

Wale ambao, Lipia mtoto wako apprenticeship, Tafuta watu walau wa karibu unaowaamini wanaoendesha maisha yao kwa kuwa wakulima, wafugaji, vinyozi, wapishi, seremala, n.k. uwe unawalipa wamfundishe kazi mtoto. yani kila likizo awe anatumia muda wake huko kujinoa zaidi, azijue abcd za kuingiza hela, hata akimaliza chuo ukimpa mtaji anafungua ofisi yake huku anajua anachofanya na jinsi ya kukabiliana nachangamoto sio kuanza upya.
 
Ndio maana nawaambia kila siku acheni kulipa mamilioni kwenye shule za kiingereza ni kupoteza hela bure. Pelekeni watoto wenu Kayumba
 
Ndio maana nawaambia kila siku acheni kulipa mamilioni kwenye shule za kiingereza ni kupoteza hela bure. Pelekeni watoto wenu Kayumba
Japo elimu yetu ya kimagumashi lakini ni bora mtoto aende shule ya kiingereza kuliko kiswahili kwasababu sekondari mpaka chuo watoto wanaenda kufundishwa kwa kiingereza, ni bora waanze kujifunza kwa kiingereza tangu utotoni.

Halafu si kila shule za kiingereza ni milioni, zipo za msingi za msingi za serikali ada laki 2 na nusu zinafanya vizuri tu
 
Ndio maana nawaambia kila siku acheni kulipa mamilioni kwenye shule za kiingereza ni kupoteza hela bure. Pelekeni watoto wenu Kayumba
Unasema hivyo kwa sababu shule za Tanzania siyo shule bali ni majengo ya kwenda kukariri majibu ya maswali ya mitihani. Ulaya kwa mfano kuna uhitaji mkubwa wa wafanyazi wataalam lakini huwezi kumchukuwa graduate wa masters hata PhD akafanye kazi huko kwa sababu elimu yao ni duni.
 
Ni wazi kabisa bila kupepesa macho lengo kuu la wazazi wa Tanzania ni kusomesha mtoto ili aje kupata ajira serikalini.

Ajira zinazidi kuwa adimu sana, wanafunzi wengi wanahitimu vyuo na vyuo vipo vingi sio kama zamani, wahitimu wamekuwa wengi sana lakini ajira haziongezeki.

Wanaoajiriwa ni wachache sana, wanaobaki mitaani baada ya kuona hakuna matumani ya ajira mwisho wa siku wanakubaliana na matokeo na wengi wao huishia kujiajiri ama wafanye biashara, wengi huanza kufanya shughuli hizi bila uzoefu kwasababu walitumia muda mwingi shuleni, matokeo yake ugeni wao unaweza kuchangia shughuli zao ziwe na changamoto na hata kufilisika kwa kukosa uzoefu.

Wengine wana degree zao wanaamua kufanya kazi za elf 80 kwasababu hawajui kitu kingine zaidi ya elimu ya darasani, hawana skills zozote walizowahi kujifunza nje ya darasa na hawana uzoefu wowote wa kufanya biashqra, hapa ndio wengi hudhalilika "fulani ana degree lakini anafanya kazi ya laki 1"

Nitoe rai kwa wazazi wenye biashara ama waliojoajiri kwa skills wawe bega kwa bega na watoto wao waweze kuwamegea uzoefu wao kwenye shughuli zao, mfundishe mtoto kusimamia biashara, mfundishe kodi zinalipwa wakati gani, supplier yupo wapi, jinsi ya kufungua biashara, jinsi ya kukwepa changamoto za ugeni wa biashara, n.k. itamsaidia sana kwasababu wewe mzazi ulishapitia changamoto kibao unamtafunia asizirudie, hapo mbele akikosa ajira aweze kufanya biashara.

Wale ambao, Lipia mtoto wako apprenticeship, Tafuta watu walau wa karibu unaowaamini wanaoendesha maisha yao kwa kuwa wakulima, wafugaji, vinyozi, wapishi, seremala, n.k. uwe unawalipa wamfundishe kazi mtoto. yani kila likizo awe anatumia muda wake huko kujinoa zaidi, azijue abcd za kuingiza hela, hata akimaliza chuo ukimpa mtaji anafungua ofisi yake huku anajua anachofanya na jinsi ya kukabiliana nachangamoto sio kuanza upya.
Una akili kubwa broo,ubarikiwe sana
 
Ngumu kumeza lakini huo ndio ukweli elimu ya Sasa Haina tija mzazi unatumia garama kubwa kumsomesha mtoto mwisho wa siku mtoto anamaliza anarudi mtaani na wale waliosomeshwa English medium asilimia kubwa ushoga ndio anaanzia mtoto huko wengine tunawaona mtaani wanakula ngada na wengine wanauza utelezi kwa maelewano maisha ya Sasa hayaitaji degree au PhD maisha ni juhudi zako na kumtanguliza mungu
 
unataka kusema biashara za ambao sio graduate hazipati changamoto?
Zinapata changamoto lakini tayari huyu wa darasa la Saba unakuta ana uzoefu mkubwa Sana na ameshakutana na changamoto nyingi Sasa huyu wa degree kwanza hajui lolote zaidi ya gpa ya kwanza
 
Japo elimu yetu ya kimagumashi lakini ni bora mtoto aende shule ya kiingereza kuliko kiswahili kwasababu sekondari mpaka chuo watoto wanaenda kufundishwa kwa kiingereza, ni bora waanze kujifunza kwa kiingereza tangu utotoni.

Halafu si kila shule za kiingereza ni milioni, zipo za msingi za msingi za serikali ada laki 2 na nusu zinafanya vizuri tu
Haina tija ndio maana wazungu wanaangalia mtoto ana talent gani anayo na anamkazania hio na mwisho wa siku mtoto anaenda vizur na maisha yake na kwa Sasa tekilogia zimekuwa Pana Sana huko ulaya marobo yameanza kufanya kazi maofisini na sehemu nyeti idadi kubwa ya watu wanakuwa hawana kazi mkuu
 
Back
Top Bottom