Wazabuni na biashara serikalini inatisha

The Listener

JF-Expert Member
Feb 5, 2012
993
213
Serikali imekuwa (kama inavyotakiwa na sheria ya manunuzi) ikiingia tenda na wafanyabiashara ili shughuli zake ziende kama inavyotakiwa yaani kutekeleza malengo yaliyopangwa kwa mwaka husika wa fedha. Mimi kinachonisikitisha ni namna serikali inavyokubali kuliwa kirahisirahisi (ingawa nahisi ni makusudi kwa kamisheni ya ten percent). Lita moja ya mafuta ya dizeli ya bei ya shilingi 2000 mtaani, serikali wananunua kwa tenda kwa shilingi 2500. Vifaa vikubwa na vya gharama zaidi mtaani bei yake kwa serikali ni balaa tupu. Hii ndo Serikali yetu na nashindwa elewa kwani hakuna hata kiongozi mmoja mwenye uthubutu wa kufanya mabadiliko makubwa ya kuondoa haya mawaa?
 
Hii ni biashara mkuu,kama serikali itahitaji kwa bei hiyo wanayochukulia watu wengine na wenyewe waje na cash on hand kununua product,,hivi can u imagine mkuu unapata tender ya serikali na baada ya kutoa huduma hesabu miezi hadi mitatu na kuendelea kwa ajili ya kulipwa,sasa kwa vimtaji vyakudunduliza uwauzie kwa bei hiyo?lazima nipande juu hata peni ya mia 2 mi ntawachaji 1000
 
Back
Top Bottom