The Listener
JF-Expert Member
- Feb 5, 2012
- 993
- 213
Serikali imekuwa (kama inavyotakiwa na sheria ya manunuzi) ikiingia tenda na wafanyabiashara ili shughuli zake ziende kama inavyotakiwa yaani kutekeleza malengo yaliyopangwa kwa mwaka husika wa fedha. Mimi kinachonisikitisha ni namna serikali inavyokubali kuliwa kirahisirahisi (ingawa nahisi ni makusudi kwa kamisheni ya ten percent). Lita moja ya mafuta ya dizeli ya bei ya shilingi 2000 mtaani, serikali wananunua kwa tenda kwa shilingi 2500. Vifaa vikubwa na vya gharama zaidi mtaani bei yake kwa serikali ni balaa tupu. Hii ndo Serikali yetu na nashindwa elewa kwani hakuna hata kiongozi mmoja mwenye uthubutu wa kufanya mabadiliko makubwa ya kuondoa haya mawaa?