Replica
JF-Expert Member
- Aug 28, 2017
- 1,446
- 7,822
Shabiki wa Arsenal ameaga dunia baada ya kuchomwa na kitu chenye ncha kali na shabiki wa Man U kwenye banda la video.
Wawili hao walianza kwa kurushiana maneno na kufikia ugomvi baada ya VAR kukataa goli la Man U.
Ugomvi huo ukapelekea kifo cha Jackson Aineruhanga eneo la Sheema, kaskazini mwa Uganda.
Mtuhumiwa baada ya tukio alikimbia, yuko mafichoni akitaabika na dunia akiukumbuka kwa vitendo msemo wa waswahili, majuto ni mjukuu. Polisi wa Uganda wanamsaka.
Pamoja na timu za Man na Arsenal kuzaliwa miaka ya 1800's nchini Uingereza na kuwa na mashabiki wanaoishi waliozishabikia kwa zaidi ya miaka 100 hamna mauaji yaliyotokana na mechi ya juzi nchini humo.
Wawili hao walianza kwa kurushiana maneno na kufikia ugomvi baada ya VAR kukataa goli la Man U.
Ugomvi huo ukapelekea kifo cha Jackson Aineruhanga eneo la Sheema, kaskazini mwa Uganda.
Mtuhumiwa baada ya tukio alikimbia, yuko mafichoni akitaabika na dunia akiukumbuka kwa vitendo msemo wa waswahili, majuto ni mjukuu. Polisi wa Uganda wanamsaka.
Pamoja na timu za Man na Arsenal kuzaliwa miaka ya 1800's nchini Uingereza na kuwa na mashabiki wanaoishi waliozishabikia kwa zaidi ya miaka 100 hamna mauaji yaliyotokana na mechi ya juzi nchini humo.