sky soldier
JF-Expert Member
- Mar 30, 2020
- 5,408
- 19,034
Oh, Ajira ni utumwa
Oh, kuajiriwa ni manyanyaso
Huwa hawanaga utofauti sana na wale waliokulia maisha ya kimasikini ambao ni rahisi sana kuwajua siku hizi, ukisikia mtu anatumia sana msemo maarufu " Tafuta pesa" ni kwamba huyo kuna uwezekano mkubwa sana kakulia maisha ya kimasikini sana.
Basi ndivyo ilivyo kwa wanaoponda sana ajira, mara nyingi ni kwamba wao wamejionea maisha ya ajira kwa wazazi au ndugu walioajiriwa private kwenye malipo madogo na manyanyaso ama ikiwa serikalini basi ni hizi ajira zenye mishahara midogo, fursa chache za kuongezwa vyeo, n.k.
Kuna watumishi wa serikalini wako poa tu wanasomesha watoto shule za private, wana nyumba nzuri, magari hadi watoto wanawanunulia, n.k. na hapo mambo huwa yanakuwa matamu zaidi mtumishi akipiga hybrid yani ana biashara zake pia.
Watu wanakula maisha vizuri tu kwa ajira tusikaririshane kwamba ajira zote ni umasikini,
Mtu ana likizo ya siku 30 kila mwaka, kila jumamosi na jumapili ni off, akiumwa anapewa likizo hadi apone, saa 11 jioni ashatoka kazini anaenda kuspend na familia yake, sioni kigezo cha kumponda kiasi hicho kwamba huyu mtu ni mtumwa .
Offcourse biashara ndio inapesa zaidi lakini pia tukumbuke kwenye biashara kuna upande wa kikatili zaidi ambao wengi huuficha, kuna kufirisika, ushindani mkali, kodi, n.k. so biashara ni tamu lakini nayo tuwe tunaiangazia upande wake wa kikatili, uanweza ukawa unajadiliana na mtu aliejiajiri hata elf 10 kwa siku kuingiza ni shughuli lakini ghafla anajitetea kwamba ajira utumwa kina Mo na Bakhresa (wawekezaji) hawajaajiriwa, hataki kusema yeye kila siku lazima afungue ofisi, kurudi usiku, hana likizo, madeni, n.k.
Oh, kuajiriwa ni manyanyaso
Huwa hawanaga utofauti sana na wale waliokulia maisha ya kimasikini ambao ni rahisi sana kuwajua siku hizi, ukisikia mtu anatumia sana msemo maarufu " Tafuta pesa" ni kwamba huyo kuna uwezekano mkubwa sana kakulia maisha ya kimasikini sana.
Basi ndivyo ilivyo kwa wanaoponda sana ajira, mara nyingi ni kwamba wao wamejionea maisha ya ajira kwa wazazi au ndugu walioajiriwa private kwenye malipo madogo na manyanyaso ama ikiwa serikalini basi ni hizi ajira zenye mishahara midogo, fursa chache za kuongezwa vyeo, n.k.
Kuna watumishi wa serikalini wako poa tu wanasomesha watoto shule za private, wana nyumba nzuri, magari hadi watoto wanawanunulia, n.k. na hapo mambo huwa yanakuwa matamu zaidi mtumishi akipiga hybrid yani ana biashara zake pia.
Watu wanakula maisha vizuri tu kwa ajira tusikaririshane kwamba ajira zote ni umasikini,
Mtu ana likizo ya siku 30 kila mwaka, kila jumamosi na jumapili ni off, akiumwa anapewa likizo hadi apone, saa 11 jioni ashatoka kazini anaenda kuspend na familia yake, sioni kigezo cha kumponda kiasi hicho kwamba huyu mtu ni mtumwa .
Offcourse biashara ndio inapesa zaidi lakini pia tukumbuke kwenye biashara kuna upande wa kikatili zaidi ambao wengi huuficha, kuna kufirisika, ushindani mkali, kodi, n.k. so biashara ni tamu lakini nayo tuwe tunaiangazia upande wake wa kikatili, uanweza ukawa unajadiliana na mtu aliejiajiri hata elf 10 kwa siku kuingiza ni shughuli lakini ghafla anajitetea kwamba ajira utumwa kina Mo na Bakhresa (wawekezaji) hawajaajiriwa, hataki kusema yeye kila siku lazima afungue ofisi, kurudi usiku, hana likizo, madeni, n.k.