JanguKamaJangu
JF-Expert Member
- Feb 7, 2022
- 2,308
- 5,460
Kamanda wa Polisi mkoani humo Pius Lutumo amethibitisha kutokea kwa tukio hilo na kueleza kuwa amepata taarifa ya tukio hilo na kwa wakati huo alikuwa njiani kuelekea eneo la tukio, hivyo kuahidi kutoa taarifa zaidi wakati unaofuata.
"Nimesikia hivyo nipo njiani naelekea huko kwenye tukio,”- Kamanda Lutumo.
Diwani wa kata ya Mbwewe Omary Msonde amesema kuwa ajali hiyo imetokea saa kumi na mbili alfajiri ya leo, Alhamisi Desemba 28.2023.
Katika hatua nyingine, Mkuu wa Wilaya ya Handeni, Mkoani Tanga, Albert Msando kupitia mitandao yake binafsi ya kijamii amesema kuwa waliofariki ni familia ya Diwani wa Kata ya Kabuku, Halmashauri ya Wilaya Handeni mkoani Tanga, Nurudin Semnangwa ambapo amepoteza mke, mtoto na dada wa kazi.
Chanzo: JamboTV