Watu 70,000 wazingirwa na matope Marekani,wako hatarini kufa

Webabu

JF-Expert Member
Apr 29, 2010
7,194
10,929
Kundi kubwa la watu wako hatarini kufa huko jimbo la Nevada nchini Marekani baada ya kuzingirwa na matope mazito kwenye eneo walilokwenda kushiriki sherehe za kila mwaka za kumchoma mtu "Burning man".
Eneo kikawaida huwa ni vumbi kali lakini mwaka huu wakati watu wako katikati ya sherehe hizo mvua kubwa zimenyesha na kusababisha matope mazito yaliyowazuia watu hao kutoka kurudi makwao na huku shughuli za sherehe hiyo kusitishwa mara moja.
Mamlaka ya jimbo hilo limewataka watu hao wasijaribu kuondoka na hakuna ruhusu ya mtu yoyote kuingia eneo hilo..Pia wametakiwa wahifadhi chakula na maji walivyobakisha katika hakiba zoa.Katika hali ya taharuki hiyo utabiri wa hali ya hewa unaonesha mvua kubwa inatarajiwa kunyesha katika siku chache zijazo.

View: https://www.youtube.com/watch?v=6UxcX7_QNnU
 
Hawawezi kufa kwanz yatakauka fasta..na misaada watapata helicopter kibao..condition itai mprove ndani ya siku 4
Tuombe iwe hivyo lakini kifo hapo kiko nje nje.Helikopta na vifaru ikiwa vifo vimepangwa vitokee havitafanya kitu. Watu ni wengi sana na misaada ya kuokoa watu ina kikomo.
 
... mtasema laana zinayakumba makafir! Majanga ya asili hayana mwenyewe; uwe kafir au nani hayana kwao. Mungu wa Mbinguni awanusuru.
Uturuki mji ulisawazishwa na tetemeko na ni watu wa diin
 
Tuombe iwe hivyo lakini kifo hapo kiko nje nje.Helikopta na vifaru ikiwa vifo vimepangwa vitokee havitafanya kitu. Watu ni wengi sana na misaada ya kuokoa watu ina kikomo.
Mimi nina imani na mamlaka ya nchi za wenzentu, kule hata mtu mmoja anathaminiwa sana tofauti na hapa kwetu wanaweza wakafa watu 50 ila kama hakijatokea kitu.
 
Hii dunia ina sherehe nyingi sana zenye kuwafanya watu wawe na fantasies za ajabu sana...🤣
Hiyo baningi mani ndio naisikia tudei walahi...😂
 
Mimi nina imani na mamlaka ya nchi za wenzentu, kule hata mtu mmoja anathaminiwa sana tofauti na hapa kwetu wanaweza wakafa watu 50 ila kama hakijatokea kitu.
Hili janga kama linaanza mdogo mdogo.Baada ya siku tatu sijui itakuwaje.Nakumbuka Tsunami ya kule Thailand.hakuna cha mamlaka wala nini.Mwenyezi Mungu akikasirika anaziba njia zote za kujiokoa.
Pale Jangwani nimeona watu wameshaanza kutaharuki sana.Huwezi kwenda na hata gari hazitoki.Ibaki rehma za Mungu tu.
 
Uturuki mji ulisawazishwa na tetemeko na ni watu wa diin
Mfano mzuri sana huo.Watu wa dini hawaangamizwi namna hiyo.Lazima kuna kufri kubwa ilikuwa ikitokea kule.Mji ukiona una kufru sana hama haraka.
 
Chunga sana mdomo wako unapozungumzia mambo ya Mungu.Dini yoyote utakayokuwa au usiwe na dini Mungu (Allah) hataniwi.
Ninyi watu wa dini ndio Mnaomtania huyo mungu wenu, eti anakasirika, ana wivu, ana kisasi, nk... Sasa mbona hayo yote ni mambo ambayo hata binadamu werevu hawafanyi ila tu wapumbavu.

Unayechukia ni wewe unasingizia ni mungu. Pole sana!
 
Hii dunia ina sherehe nyingi sana zenye kuwafanya watu wawe na fantasies za ajabu sana...🤣
Hiyo baningi mani ndio naisikia tudai walahi...😂
Na mimi ndio nimeisoma na kuijua hapa muda huu na kazi yangu ya kwanza nikutafuta uthibitisho kama kweli kuna Sherehe ya aina hiyo.
Nina wasiwasi huenda ikawa si yakumchoma mtu bali yakumchoma mtu "Mweusi" au yakuchoma "Maiti".
 
Back
Top Bottom