Watoto wanakata viuno, Wazazi tunashangilia kwa shangwe, mbinja na vigeregere!

Jumakidogo

R I P
Jul 16, 2009
1,851
417
Inaonekana kwa watanzania hakuna namna yoyote, ama mtindo mbadala wa kucheza muziki, ama kunengua ngoma za asili bila ya kukata MAUNO. Naweza kusema kuwa tumefeli kwa kukosa ubunifu wa kupata namna nyingine ya uchezaji bila ya kukata kiuno. Nilihudhuria sherehe za kumaliza elimu ya msingi katika shule moja mjini Dodoma ambapo wazazi, walezi na watu mbalimbali walialikwa. Ikafika wakati kikundi cha ngoma cha shule hiyo kikaitwa kutumbuiza. Hapo mashindano ya kukata kiuno kwa vitoto hivyo yakaanza. Ikawa ni sawa na kutizama mkanda wa picha chafu. Watu wakalipuka kwa shangwe huku mgeni rasmi naye akiinua mikono juu kama shabiki wa mpira. Hapo nikajiuliza swali, hivi hakuna namna nyingine ya unenguaji mpaka watu wakate mauno? NB: Agharabu kukata kiuno ni tendo linalotumika zaidi wakati mwanamke na mwanaume wanapofanya tendo la ndoa.
 
Jumakdg kimtazamo naungana na ww kulichukia hilo! Bt still yet tutaendelea kulichukia kimyakimya na kikivyovyote vl iwavyo hatutoweza kulikemea, utaniuliza kwa nini? Nitakujibu ndy, kw sababu liko kwenye MTAALA. Mtaala ambao umeathiriwa na globalasation! Wachache sana watakao kuelewa nini unakikemea! Na kundi kubwa la jamii litakuita majina kama vl NATIVE, ILETERATE, LAYMAN, with related matter! Nakumbuka mimi wkt nina age under 15 nyumbani kwetu binti (dada zangu) ilikua ni marufuku kujifunga khanga ya kuzunguka kiuno, khanga ilikua ni inafungwa kishingoshingo! Huo ndy ulikua utaratibu na itifaki ilizingatiwa. Ukichakata kimsingi sababu iliopelekea kwa nini style ya khanga jibu liko wazi, hakuna atakae nipinga kwmb mwili mzima wa mwanamke kw mbele ya mwanaume ni bidhaa tamaniwa tu! Ni mara ngp umewasikia wanaume wakisema "mi nimempendea meno yake tu!" "nimempendea miguu!" "miondoko yake, shingo ya upanga, macho ya panzi, kucha zake bwn!". Hapo ndy sijataja zile sehemu kuu kama matiti, masaburi n.k so far khanga ya kiuno inamfanya binti au mwanamke awe displayed body figure! Hivyo bodymap ya binti iwapo mbele ya mwanaume ambae hormon zake zenu ziko active na isitoshe wanaume nyie ndy wageni waalikwa mabinti zenu ndy wanawakatikia viuno, hata kama ww umeenda pale kw kofia ya mzazi, angalizo hapo mtoto ni yule uliyemzaa! Yatakayofata yako wazi, mwenye macho haambiwi tazama.
 
Inaonekana kwa watanzania hakuna namna yoyote, ama mtindo mbadala wa kucheza muziki, ama kunengua ngoma za asili bila ya kukata MAUNO. Naweza kusema kuwa tumefeli kwa kukosa ubunifu wa kupata namna nyingine ya uchezaji bila ya kukata kiuno. Nilihudhuria sherehe za kumaliza elimu ya msingi katika shule moja mjini Dodoma ambapo wazazi, walezi na watu mbalimbali walialikwa. Ikafika wakati kikundi cha ngoma cha shule hiyo kikaitwa kutumbuiza. Hapo mashindano ya kukata kiuno kwa vitoto hivyo yakaanza. Ikawa ni sawa na kutizama mkanda wa picha chafu. Watu wakalipuka kwa shangwe huku mgeni rasmi naye akiinua mikono juu kama shabiki wa mpira. Hapo nikajiuliza swali, hivi hakuna namna nyingine ya unenguaji mpaka watu wakate mauno? NB: Agharabu kukata kiuno ni tendo linalotumika zaidi wakati mwanamke na mwanaume wanapofanya tendo la ndoa.
Kizazi hiki kimepotoka kuanzia kwa viongozi wetu wa juu!!
Angalia serikali kufadhili mashindano ya Big brother ambapo Uzinzi unafanyika hadharani harafu Rais anashangili ushindi !!
Ulishaona mashindano ya urembo ?? Ni matusi makubwa kwa Watanzania !!!
Hata vingozi wa dini Wanashabikia uchafu huu ni aibu!!!
 
Kuna nyimbo imeibwa na mtoto na wanapenda sana kuicheza kwenye watoto show itv hata jana waliicheza kwakweli WATOTO WANAKATA VIUNO OVER WATU WAZIMA ninaichukia sana hii nyimbo na sijui wazazi wa watoto husika wanajiskiaje kuona watoto wao wanakatika hivyo! Kiukweli namwelimisha mwanangu kuwa kufanya hivyo ni kosa na endapo nitamfuma akikata kiuno NITAMTENGUA KIUNO
 
MACHO HUONA KILE MAWAZO YANACHOFIKIRI! Watu wawili walipotelea pangoni katika harakati za kutafuta hazina ya kale,siku tatu wakitafuta njia ya kutoka pangoni waliona upenyo wa kutokea nje. Maongezi yao baada ya kutoka nje ilikuwa hivi:
Mtu1:naona nuru,kumbe ni mchana!

Mtu2:hapa chini ni matope tu,yaani naona kinyaa!

FUNDISHO:tunaweza kuangalia viuno na kudhani wanatupagawisha kisha tukaweka MIKONO MIFUKONI au kutazama huo ubunifu na kusema: lo! Hapa kuna vipaji zaidi ya Rihana,
 
Inaonekana kwa watanzania hakuna namna yoyote, ama mtindo mbadala wa kucheza muziki, ama kunengua ngoma za asili bila ya kukata MAUNO. Naweza kusema kuwa tumefeli kwa kukosa ubunifu wa kupata namna nyingine ya uchezaji bila ya kukata kiuno. Nilihudhuria sherehe za kumaliza elimu ya msingi katika shule moja mjini Dodoma ambapo wazazi, walezi na watu mbalimbali walialikwa. Ikafika wakati kikundi cha ngoma cha shule hiyo kikaitwa kutumbuiza. Hapo mashindano ya kukata kiuno kwa vitoto hivyo yakaanza. Ikawa ni sawa na kutizama mkanda wa picha chafu. Watu wakalipuka kwa shangwe huku mgeni rasmi naye akiinua mikono juu kama shabiki wa mpira. Hapo nikajiuliza swali, hivi hakuna namna nyingine ya unenguaji mpaka watu wakate mauno? NB: Agharabu kukata kiuno ni tendo linalotumika zaidi wakati mwanamke na mwanaume wanapofanya tendo la ndoa.

Ndio maana wazungu wanaziita ngoma za kishenzi, zinadepict kinachotokea wakati mke na mume wanafanya tendo la ndoa. Sio vizuri kuonyesha vitu hivyo hadharani, ni vitu vinahitaji usiri mkubwa. Sasa watoto wetu wanafanya hadharani, tabia chafu sana. Wazazi tusiruhusu uchafu huu ufundishwe watoto wetu.
 
usipokata kiuno utakata nini?? magoti??
attachment.php
 
Back
Top Bottom