Jumakidogo
R I P
- Jul 16, 2009
- 1,851
- 417
Inaonekana kwa watanzania hakuna namna yoyote, ama mtindo mbadala wa kucheza muziki, ama kunengua ngoma za asili bila ya kukata MAUNO. Naweza kusema kuwa tumefeli kwa kukosa ubunifu wa kupata namna nyingine ya uchezaji bila ya kukata kiuno. Nilihudhuria sherehe za kumaliza elimu ya msingi katika shule moja mjini Dodoma ambapo wazazi, walezi na watu mbalimbali walialikwa. Ikafika wakati kikundi cha ngoma cha shule hiyo kikaitwa kutumbuiza. Hapo mashindano ya kukata kiuno kwa vitoto hivyo yakaanza. Ikawa ni sawa na kutizama mkanda wa picha chafu. Watu wakalipuka kwa shangwe huku mgeni rasmi naye akiinua mikono juu kama shabiki wa mpira. Hapo nikajiuliza swali, hivi hakuna namna nyingine ya unenguaji mpaka watu wakate mauno? NB: Agharabu kukata kiuno ni tendo linalotumika zaidi wakati mwanamke na mwanaume wanapofanya tendo la ndoa.