Kuna maneno yanasemwa sana humu JF kwamba watu wanamuonea wivu Januari Makamba ndio maana wanamkosoa juu ya utendaji wake wa kazi ni kwa sababu tu ametoka kwenye familia bora ya uongozi
Watoto wa Mwalimu JK Nyerere kina Makongoro Nyerere RC wa Manyara mbona hawana kesi na umma na hawasemwi kwa lolote
Kwanini Hussein Ali Mwinyi- Rais wa Zanzibar hajawahi kusemwa kwa ubaya wowote licha ya kuwa Mtoto wa Rais Mstaafu wa Zanzibar na baadaye Rais wa JMT na tunaona mageuzi anayoyafanya Zanzibar.
Watoto wa Benjamini Mkapa ambaye nadhani mmoja ni Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Ardhi kama sikosei mbona licha ya Baba yake kuwa Rais wa JMT hasemwi kwa lolote
Watoto wa Mstaafu Rais Jakaya Kikwete, Ridhiwani Kikwete mbona yeye anaonekana ni mtu mwenye kuongelewa vizuri na watu sio mtu wa kujikweza na hata majukumu haya mapya aliyopewa ya Naibu Waziri wa Ardhi anaonekana ameanza vizuri na hakuna anayelalamikia utendaji wake.
Watoto wa Dk. John Pombe Joseph Magufuli ndio hawakusika kabisa enzi baba yao akiwa Rais wanaonekana siku ya mazishi ya Baba yao
Hii dhana kwamba Januari Makamba anaonewa wivu kwa sababu ni mtoto wa Mkubwa sasa yeye ambaye Baba yake aliishia kwenye Katibu Mkuu wa CCM na hao ambao baba zao wameishia kwenye Urais kabisa wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania nani wazazi wao walikuwa watu wakubwa kwenye nchi hii.
Alafu tunaletewa maneno kwamba Januari amelelewa vizuri na Mzee Mkapa na Kikwete sasa yeye atakuwa amepata malezi bora zaidi ya akina Ridhiwani au Nicholas?
Swali la kujiuliza kwanini Jakaya Kikwete hakuwahi kumpa Uwaziri kamili kama alimuamini uwezo wake kwanini aliishia kumpa Unaibu Waziri tu tena wa Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia Mei Mwaka 2012 akahudumu kwa miaka mitatu tu kufikia 2015 mwisho wa utawala wa JK.
Tutatafakari kwa pamoja kama kuna mahali nimekosea mnaweza kunisahihisha.
Watoto wa Mwalimu JK Nyerere kina Makongoro Nyerere RC wa Manyara mbona hawana kesi na umma na hawasemwi kwa lolote
Kwanini Hussein Ali Mwinyi- Rais wa Zanzibar hajawahi kusemwa kwa ubaya wowote licha ya kuwa Mtoto wa Rais Mstaafu wa Zanzibar na baadaye Rais wa JMT na tunaona mageuzi anayoyafanya Zanzibar.
Watoto wa Benjamini Mkapa ambaye nadhani mmoja ni Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Ardhi kama sikosei mbona licha ya Baba yake kuwa Rais wa JMT hasemwi kwa lolote
Watoto wa Mstaafu Rais Jakaya Kikwete, Ridhiwani Kikwete mbona yeye anaonekana ni mtu mwenye kuongelewa vizuri na watu sio mtu wa kujikweza na hata majukumu haya mapya aliyopewa ya Naibu Waziri wa Ardhi anaonekana ameanza vizuri na hakuna anayelalamikia utendaji wake.
Watoto wa Dk. John Pombe Joseph Magufuli ndio hawakusika kabisa enzi baba yao akiwa Rais wanaonekana siku ya mazishi ya Baba yao
Hii dhana kwamba Januari Makamba anaonewa wivu kwa sababu ni mtoto wa Mkubwa sasa yeye ambaye Baba yake aliishia kwenye Katibu Mkuu wa CCM na hao ambao baba zao wameishia kwenye Urais kabisa wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania nani wazazi wao walikuwa watu wakubwa kwenye nchi hii.
Alafu tunaletewa maneno kwamba Januari amelelewa vizuri na Mzee Mkapa na Kikwete sasa yeye atakuwa amepata malezi bora zaidi ya akina Ridhiwani au Nicholas?
Swali la kujiuliza kwanini Jakaya Kikwete hakuwahi kumpa Uwaziri kamili kama alimuamini uwezo wake kwanini aliishia kumpa Unaibu Waziri tu tena wa Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia Mei Mwaka 2012 akahudumu kwa miaka mitatu tu kufikia 2015 mwisho wa utawala wa JK.
Tutatafakari kwa pamoja kama kuna mahali nimekosea mnaweza kunisahihisha.