Nimesikitishwa na vitendo vya watoto wa Nyerere kutumia jina la baba yako na kudai viwanja vingi msasani ambavyo si vyao. Kuna watu wengi wana viwanja karibu na nyerere na wameshutushwa kwa kuambiwa baada ya miaka mingi kwamba watoto wa Nyerere wanadai ni mali ya baba yao. Raisi kwasababu ya uwoga wa siasa ame revoke hati za kihalali za viwanja vyote pembeni mwa nyerere kwani watoto wanadai ni vya kwao na kesi ziko mahakamani!. Kwa kuwa hawa watoto hawafanyi vizuri kibiashara na kimaisha wameona kitu pekee wanachoweza kufanya ni kudai viwanja kwani viwanja vimepanda thamani sana hivyo hawakudai wakati baba yao yupo sasa miaka mingi imepita na mama yako haelewi haya maovu basi wameona ni wakati wa kutumia jina na baba yao ambaye alipewa nyumba na watanzania kwa manufaa binafsi. Hali hii imemfanya raisi ku revoke viwanja na itabidi serikali ilipe fidia kwa viwanja ambao havikuwa vya nyerere. Raisi ame revoke vibali hivyo kwani kihalali hawawezi kushinda. Siamini kama nyere angekuwepo leo angeachia watoto wake waanze kupagania viwanja ambavyo siyo vyao.