Ashampoo burning
JF-Expert Member
- May 12, 2023
- 420
- 1,583
Jamaa alikuwa na nyumba nzuri tu Tabata lakini kamwe alikataa kukaa nje ya mji hata mimi ashampoo ni moja ya wadau ambao napenda kukaa Posta
Jamaaa alikuwa na marafiki wengi wenye vipato hasa hela chafu nikisema hela chafu naamanisha chafu hela za deal za kimafia lakini hakushawishisika kuingia huko aliendelea kuishi na kipato chake cha kawaida na kile kigari chake mimi nimemuona nacho miaka mingi kinomahhivi hakuwa na tamaa ovyo.
Alipenda sana starehe alifanya kazi jioni unamkuta kwenye starehe zake na mabebez watu wanalalamika ila hela alikuwa anajitafutia mwenyewe so matumiz yake
Kwenye siasa yeye huko ndo alikuwa ana marafiki wa kila aina alijaribu ila siasa sio za wote..... japo za chini wana sema jamaaa usalaama(TISS) we huoni kesho anaagwa pale karimjee pale huwa haagwi kajamba nani
Mzee wake malecela kapoteza kijana wake RIP POLE MZEEE
Hapa mwishoni le mutuz alikuwa kama gari la mkaa safari moja kijijini safari nyingine gereji.... mwishoni afya ya lemutuz ilianza kumsumbua hasa moyo alikuwa analazwa sana pale Muhimbili kitengo cha jakaya mambo ya moyo
Baaada ya kuona hali hiyo alijua mwisho wake hauko mbali miaka ya nyuma aligombana na mke wake na watoto sasa aliwatumia meseji kuwaomba msahamaha pia kuwaambia anaumwa hivyo anaomba msamaha.
Yale matoto yana roho ngumu yakamtumia zile meseji Mange Kimambi akapost kwenye ile app yake na Mange alifurahi maana watu hawa ni maadui akalipua hewani zile meseji.
Ila nadhani Le Mutuz alikuwa anaomba msamaha akijua tu huu mwisho wake umefika mara nyingi watu hupenda kuomba msamaha kabla ya mauti.
Watoto wa Lemutuz kama mnasoma ujumbe huu msameheni baba yenu aande kwa amani aliwakimbia marekani labda maisha yalikuwa magumu ....ASHAMPOO hapa.