Zero
JF-Expert Member
- Mar 8, 2008
- 299
- 17
Wadau,
Hii sijui kama inafit kwenye jukwaa la siasa, lakini naona imekaa kisiasa zaidi na inagusa maslahi ya umma.
Kuna huu utaratibu wa kampuni nyingi za umma kuwauzia wananchi vifaa ambavyo vinahusiana na huduma wanayotoa na vile vile kuwatoza malipo kwa huduma yenyewe.
Nitatumia mfano wa kampuni za simu, shirika la umeme (TANESCO) na upande wa maji ni DAWASCO. Mimi naamini, nikiwa kama mteja wa kampuni fulani ya simu, nisingepaswa kuuziwa simcard, maana hiyo ni nyenzo yao wao ya kuniwezesha mimi kutumia huduma yao na kuilipia kila ninapoitumia. Hapa sioni hoja ya mimi kununua simcard. Maana mwisho siku nikiichoka kampuni yao, sina pa kuipeleka simcard zaidi ya kuitupa.
Vivyo hivyo kwenye upande wa umeme. Ni kwanini mteja alipishwe gharama za nguzo, waya na meter pale anapotaka kuwekewa umeme kwenye jengo lake ilhali mteja huyu atakuwa analipia gharama za umeme kila anapotumia? Hapa pia mimi sioni hoja.
Napongeza upande wa DAWASCO kwa kutoa meter zao bure. Kwa upande wao, kama mteja hudai ankara yoyote ya nyuma, basi unapewa meter ya maji bure pamoja na fundi wa kufanya installation bure. Makampuni mengine yaige mfano huu.
Najua mifano wa huduma za aina hii ni nyingi, na wadau mnaweza kutoa mifano mingi zaidi na zaidi. Hoja hii inagusa maslahi ya watanzania wengi maana bei za huduma hizi ni ghali sana. Kwa upande wa TANESCO, gharama za kufunga umeme ni ghali mno. Wananchi wengi vijijini wanashindwa kupata huduma hii muhimu kutokana na ughali wake. Mimi nadhani TANESCO wangeliangalia hili na kuona kama changamoto kwao ya kuongeza mapato kwa kuwafikishia watanzania wengi huduma hii kwa gharama nafuu.
Hii sijui kama inafit kwenye jukwaa la siasa, lakini naona imekaa kisiasa zaidi na inagusa maslahi ya umma.
Kuna huu utaratibu wa kampuni nyingi za umma kuwauzia wananchi vifaa ambavyo vinahusiana na huduma wanayotoa na vile vile kuwatoza malipo kwa huduma yenyewe.
Nitatumia mfano wa kampuni za simu, shirika la umeme (TANESCO) na upande wa maji ni DAWASCO. Mimi naamini, nikiwa kama mteja wa kampuni fulani ya simu, nisingepaswa kuuziwa simcard, maana hiyo ni nyenzo yao wao ya kuniwezesha mimi kutumia huduma yao na kuilipia kila ninapoitumia. Hapa sioni hoja ya mimi kununua simcard. Maana mwisho siku nikiichoka kampuni yao, sina pa kuipeleka simcard zaidi ya kuitupa.
Vivyo hivyo kwenye upande wa umeme. Ni kwanini mteja alipishwe gharama za nguzo, waya na meter pale anapotaka kuwekewa umeme kwenye jengo lake ilhali mteja huyu atakuwa analipia gharama za umeme kila anapotumia? Hapa pia mimi sioni hoja.
Napongeza upande wa DAWASCO kwa kutoa meter zao bure. Kwa upande wao, kama mteja hudai ankara yoyote ya nyuma, basi unapewa meter ya maji bure pamoja na fundi wa kufanya installation bure. Makampuni mengine yaige mfano huu.
Najua mifano wa huduma za aina hii ni nyingi, na wadau mnaweza kutoa mifano mingi zaidi na zaidi. Hoja hii inagusa maslahi ya watanzania wengi maana bei za huduma hizi ni ghali sana. Kwa upande wa TANESCO, gharama za kufunga umeme ni ghali mno. Wananchi wengi vijijini wanashindwa kupata huduma hii muhimu kutokana na ughali wake. Mimi nadhani TANESCO wangeliangalia hili na kuona kama changamoto kwao ya kuongeza mapato kwa kuwafikishia watanzania wengi huduma hii kwa gharama nafuu.