Kitimoto
JF-Expert Member
- Aug 25, 2012
- 5,017
- 4,675
Jeshi la Polisi limewakamata watuhumiwa watatu waliofanya mauaji ya mfanyakazi mmoja wa Mgodi wa GGM kwa jina la Milembe Selemani katika mtaa wa Matulole, Kata ya Buhalahala mkoani Geita.
Aidha Mtuhumiwa wa nne (Pastory Lugodisha), baada ya kupata taarifa ya kukamatwa kwa wahalifu wenzake aliamua kujinyonga kwa kutumia mkanda wa suruali katika pori la hifadhi ya Buhindi Wilayani Sengerema.
"Kutokana na Uchunguzi makini wa askari wanaochunguza matukio ya mauaji wamefanikiwa kukamata watuhumiwa watatu kuhusiana na mauaji ya mfanyakazi mmoja wa Mgodi wa GGM Milembe Selemani aliyekua maarufu kwa jina la Hungwa siku ya Aprili 26, 2023 katika mtaa wa Matulole kata ya Buhalahala Mkoani Geita."
SACP- Misime Amesema watuhumiwa hao wameonyesha vielelezo walivyotumia katika Mauaji hayo ikiwa ni pamoja na baadhi ya mali za marehemu, na watafikishwa mahakani wakati wowote.
"Mtuhumiwa wa nne katika tukio hili baada ya kupata taarifa ya kukamatwa kwa wahalifu wenzake na kwamba askari wamefika nyumbani kwake, aliamua kujihukumu mwenyewe kwa kujinyonga, Mtuhumiwa huyo amejulikana kwa majina ya Pastory Lugodisha @ Buchuchu na alijinyonga mei 06, 2023 kwa kutumia mkanda wa suruali katika pori la hifadhi ya Buhindi Wilayani Sengerema".Ameeleza SACP- Misime
Pia, Soma: TANZIA - Afisa Ugavi wa mgodi wa Geita, Milembe Suleiman auawa na viganja vyake kukatwa
Aidha Mtuhumiwa wa nne (Pastory Lugodisha), baada ya kupata taarifa ya kukamatwa kwa wahalifu wenzake aliamua kujinyonga kwa kutumia mkanda wa suruali katika pori la hifadhi ya Buhindi Wilayani Sengerema.
"Kutokana na Uchunguzi makini wa askari wanaochunguza matukio ya mauaji wamefanikiwa kukamata watuhumiwa watatu kuhusiana na mauaji ya mfanyakazi mmoja wa Mgodi wa GGM Milembe Selemani aliyekua maarufu kwa jina la Hungwa siku ya Aprili 26, 2023 katika mtaa wa Matulole kata ya Buhalahala Mkoani Geita."
SACP- Misime Amesema watuhumiwa hao wameonyesha vielelezo walivyotumia katika Mauaji hayo ikiwa ni pamoja na baadhi ya mali za marehemu, na watafikishwa mahakani wakati wowote.
"Mtuhumiwa wa nne katika tukio hili baada ya kupata taarifa ya kukamatwa kwa wahalifu wenzake na kwamba askari wamefika nyumbani kwake, aliamua kujihukumu mwenyewe kwa kujinyonga, Mtuhumiwa huyo amejulikana kwa majina ya Pastory Lugodisha @ Buchuchu na alijinyonga mei 06, 2023 kwa kutumia mkanda wa suruali katika pori la hifadhi ya Buhindi Wilayani Sengerema".Ameeleza SACP- Misime
Pia, Soma: TANZIA - Afisa Ugavi wa mgodi wa Geita, Milembe Suleiman auawa na viganja vyake kukatwa