KXY
JF-Expert Member
- Dec 31, 2011
- 880
- 327
- Thread starter
- #21
Katikati ya Afrika ya Zamani na Afrika Mpya kuna daraja la mauti. Watu wa Afrika hawana budi kufa ili kuzaliwa upya katika nuru na 'mwongozo mpya' kutoka ndani na ndani ya nafsi zao na ili kumalizana na ulimwengu hadaa wa leo wa ufikirifu pofu wa kimakundi. Sehemu ya jitihada ya kushiriki haya yote ni katika kule kuchochea mawezekano ya fikra za mtu mmoja mmoja katika kule kujaribu kunasua mtu na ukundiko wake wa kiimani ama dini--hakuna jinsi, kila mtu hana budi kubeba mzigo wake katika wakati hu muhimu. Yeyote anayeona 'hajiwezi' ila kubakia na makundi yake ya usadikifu hata kwa mambo ambayo ingelimpasa sana kujimulika mwangaza--kwake huyo hakuna jinsi ila Wakati kuwa muamuzi wa mavuno ya ustahili wa wale wenye kufaulu kujinasibu katika kule kuzaliwa upya ajili ya fahari mpya.
Ni mtu mmoja mmoja aliyejikwamua kiakili ataungana na mwenzake katika shauri lenye kheri zaidi na kuzaa ushirika na taasisi zenye Nguvu Mpya, Ari Mpya na Hadhi Mpya. Mtu wa zamani ni kimeo taslim na wala hata nusa wala kuonja harafu ya marashi ya ustawi mpya wenye mawezekano; lake itakuwa ni kusakamwa na maradhi na kule kutokomea katika migogoro isiyo na suluhu na pia maangamizi ya taasisi na mifumo isiyofaa tena.
huuuu...hoi
Kipengele hicho hapo juu ndio nilichokielewa zaidi, kwa kuwa haya ni maono yako nafikiri itanichukua mda mrefu kidogo kuona kwa macho yako. Nategemea kujifunza kutoka kwako kwasababu siwezi kukataa wala kukubali kitu nisichokielewa, nakuomba utumie lugha nyepesi kwa siku zijazo.