A
Anonymous
Guest
Mzazi wangu ni mmoja wa Wazee ambao wamestaafu utumishi katika Mamlaka ya Reli ya Tanzania na Zambia (TAZARA), mzee wangu na wenzake wengi waliostaafu Mwaka 2004, 2005 na 2006 hawajalipwa stahiki zao licha ya kufanya jitihada kubwa ya kushughulikia.
Naandika andiko hili kwa maelekezo ya Mzee wangu ambapo anachokisema ndicho nakiandika...
Mimi na Wazee wenzangu tupo zaidi ya 180 tumefanya jitihada kubwa tangu wakati huo hadi leo ikiwa ni takribani miaka 20 bila mafanikio huku Serikali ikituzungusha.
Wazee wachache ambao wana ndugu kwenye nafasi za juu Serikalini wao walifanikiwa kupata msaada na wakalipwa.
Waliolipwa walikuwa na ndugu au jamaa katika nafasi za Uwaziri na nyinginezo lakini sisi huku ambao naweza kusema ‘hatujuani na Wakubwa’ tumeambulia patupu bado tunateseka kufuatilia.
Kuna wenzangu kadhaa wameshapoteza maisha bila kupata stahiki zao, familia zao zimepambana nazo hazijafanikiwa.
Uhakiki wa madai yetu ulishafanyika na Serikali ikathibitisha tangu kipindi cha Rais Jakaya Kikwete hadi cha hayati Magufuli, ambapo tulionana hadi na Mwanasheria Mkuu wa Serikali ikathibitishwa kuwa tunatakiwa kulipwa lakini hilo halijatekelezeka.
Suala letu lilifika hadi Mahakamani tukashinda shauri, baada ya hapo tukaonana na Waziri Mkuu kuwasilisha malalamiko yetu, akatusikiliza na akatukabidhi kwa maafisa wake washughulikie lakini tangu wakati huo danadana zimekuwa nyingi.
Wengi wetu wanaendelea kuteseka, wengine wanaumwa, jasho letu tulilolitoa kwa ajili ya Taifa linapotea, tunamasononeko, familia zetu zinamasononeko dhidi ya Serikali yetu kwa hiki kinachoendelea.
Mara kadhaa nimewashawishi wenzangu twenden kwenye Vyombo vya Habari kueleza changamoto zetu, hawataki kwa kuwa wengi wetu ni Wazee wa CCM na wakereketwa hasa, wenzangu wanaamini tukisema kwa Waandishi tunaweza kukiharibia chama, jambo ambalo mimi napingana nalo kwa kuwa ukimya wetu ndio anguko letu hadi tunakufa.
Taarifa zilizopo ni kuwa fedha tunazotakiwa kulipwa zipo Hazina na kuna wakati inadaiwa zimekuwa zikitoka na kurejea, kwa maana zinaingia katika matumizi mengine kisha zinarejeshwa.
Tumejuaje hilo? Harakati hizi za kwenda huku na huku zimetuwezesha kukutana na baadhi ya watu wa karibu na Mamlaka za juu wa Serikali ambao wanajua sakata hilo na wamekuwa wakitudokeza kuhusu hilo, kama ni kweli au la hilo sina uhakika.
Sisi Wastaafu wengi tuna hali mbaya sana kiuchumi, wengi tupo Dar na wengine wapo mikoa tofauti, tumeenda huku na huku bila mafanikio, yaani kwa ufupi tunatapatapa na imekuwa kawaida kuombaomba nauli kwa watu tofauti, ni aibu lakini hatuna jinsi.
Inaniuma sana kuona Watanzania tuliopambana kwa nguvu zetu zote kwa ajili ya Taifahiki haya ndio matunda.
Tumaini letu pekee limebaki kwa Rais Samia Suluhu Hassan kwani kauli yake inaweza kuwa na nguvu ya kuweza kutusaidia kupata haki yetu.
Naandika andiko hili kwa maelekezo ya Mzee wangu ambapo anachokisema ndicho nakiandika...
Mimi na Wazee wenzangu tupo zaidi ya 180 tumefanya jitihada kubwa tangu wakati huo hadi leo ikiwa ni takribani miaka 20 bila mafanikio huku Serikali ikituzungusha.
Wazee wachache ambao wana ndugu kwenye nafasi za juu Serikalini wao walifanikiwa kupata msaada na wakalipwa.
Waliolipwa walikuwa na ndugu au jamaa katika nafasi za Uwaziri na nyinginezo lakini sisi huku ambao naweza kusema ‘hatujuani na Wakubwa’ tumeambulia patupu bado tunateseka kufuatilia.
Kuna wenzangu kadhaa wameshapoteza maisha bila kupata stahiki zao, familia zao zimepambana nazo hazijafanikiwa.
Uhakiki wa madai yetu ulishafanyika na Serikali ikathibitisha tangu kipindi cha Rais Jakaya Kikwete hadi cha hayati Magufuli, ambapo tulionana hadi na Mwanasheria Mkuu wa Serikali ikathibitishwa kuwa tunatakiwa kulipwa lakini hilo halijatekelezeka.
Suala letu lilifika hadi Mahakamani tukashinda shauri, baada ya hapo tukaonana na Waziri Mkuu kuwasilisha malalamiko yetu, akatusikiliza na akatukabidhi kwa maafisa wake washughulikie lakini tangu wakati huo danadana zimekuwa nyingi.
Wengi wetu wanaendelea kuteseka, wengine wanaumwa, jasho letu tulilolitoa kwa ajili ya Taifa linapotea, tunamasononeko, familia zetu zinamasononeko dhidi ya Serikali yetu kwa hiki kinachoendelea.
Mara kadhaa nimewashawishi wenzangu twenden kwenye Vyombo vya Habari kueleza changamoto zetu, hawataki kwa kuwa wengi wetu ni Wazee wa CCM na wakereketwa hasa, wenzangu wanaamini tukisema kwa Waandishi tunaweza kukiharibia chama, jambo ambalo mimi napingana nalo kwa kuwa ukimya wetu ndio anguko letu hadi tunakufa.
Taarifa zilizopo ni kuwa fedha tunazotakiwa kulipwa zipo Hazina na kuna wakati inadaiwa zimekuwa zikitoka na kurejea, kwa maana zinaingia katika matumizi mengine kisha zinarejeshwa.
Tumejuaje hilo? Harakati hizi za kwenda huku na huku zimetuwezesha kukutana na baadhi ya watu wa karibu na Mamlaka za juu wa Serikali ambao wanajua sakata hilo na wamekuwa wakitudokeza kuhusu hilo, kama ni kweli au la hilo sina uhakika.
Sisi Wastaafu wengi tuna hali mbaya sana kiuchumi, wengi tupo Dar na wengine wapo mikoa tofauti, tumeenda huku na huku bila mafanikio, yaani kwa ufupi tunatapatapa na imekuwa kawaida kuombaomba nauli kwa watu tofauti, ni aibu lakini hatuna jinsi.
Inaniuma sana kuona Watanzania tuliopambana kwa nguvu zetu zote kwa ajili ya Taifahiki haya ndio matunda.
Tumaini letu pekee limebaki kwa Rais Samia Suluhu Hassan kwani kauli yake inaweza kuwa na nguvu ya kuweza kutusaidia kupata haki yetu.