Wasomi wetu wanaisaliti nchi au CCM inawatumia wasomi wetu kuifilisi nchi?

Allen Kilewella

JF-Expert Member
Sep 30, 2011
18,330
33,958
Tangu enzi za wizi wa Tangold na Meremeta, wizi wa fedha za Tegeta - Escrow na hata sasa wizi unaonekana kwenye Ripoti ya CAG, kila hatu ya wizi huo wahusika wakuu huwa ni wasomi wabobevu wa fani mbali mbali.

Swali linaloibuka ni kwamba wasomi wetu wanaisaliti nchi kwa kushindwa kutumia elimu waliyo nayo kwa maslahi ya nchi, au CCM ambao ndiyo wako madarakani wanawatumia wasomi wetu kuifilisi nchi?

Kuna kisa kimoja cha kweli cha mwanasiasa mmoja wa CCM mpenda kunyoa upara, kuwa wakati wa Kampeni za uchaguzi za Mwaka 2015 alikwenda kwenye chuo Kikuu kimojawapo cha Serikali na KUTAKA apewe shilingi milioni 60 kwa ajili ya Kampeni za CCM. Makamu wa Mkuu wa Chuo wakati huo aliomba apewe siku mbili awasiliane na wenzake, lakini bwana mkubwa huyo alitoa saa moja tu apewe hizo fedha.

Busar wa chuo alimwambia Makamu Mkuu wa chuo atoe hizo hela kwani akikataa hao jamaa wanao uwezo wa kumtoa yeye na kumteua mwingine ambaye atakuja kuwapa hizo hela. Mnyoa upara yule alipewa zile milioni 60 na kutokomea nazo. Mtaka hela msomi, mtoa hela msomi,lakini wote hawakufuata taratibu za fedha za chuo husika. Tatizo ni nini?
 
Wanafanya kazi Kwa kuogopa hao wasomi wameajiriwa lakini maelekezo Wanapata kutoka Kwa wakubwa.Ukigoma kufanya wanachotaka wanakutoa.Sasa nani anataka kukosa kazi wanaona Bora wakubali tu.

Nchi ilishakuwa fisadi tangia muda kilichobaki ni mazoea.
 
Hiyo story yako bila Ushahidi inakosa nguvu ya kujadiliwa hapa ndugu yangu, maana Inabaki kama hadithi tu ya ndotoni,kikubwa lazima ufahamu ya kuwa chini ya uongozi shupavu na madhubuti wa Rais Samia na serikali yake Hakuna mtu atakayebakia salama akibainika kugusa pesa za umma.
 
Hiyo story yako bila Ushahidi inakosa nguvu ya kujadiliwa hapa ndugu yangu ,maana Inabaki Kama hadithi tu ya ndotoni,kikubwa lazima ufahamu ya kuwa chini ya uongozi shupavu na madhubuti wa Rais Samia na serikali yake Hakuna mtu atakayebakia salama akibainika kugusa pesa za umma.
Unataka ushahidi ili kiwe nini? CAG huwa anaweka ushahidi na wala huwa hakuna kinachofanyika. Halafu huwa hamuezi kujenga hoja mpaka mtie na marapurapu ya kusifia aliyeko madarakani?
 
Unataka ushahidi ili kiwe nini? CAG huwa anaweka ushahidi na wala huwa hakuna kinachofanyika. Halafu huwa hamuezi kujenga hoja mpaka mtie na marapurapu ya kusifia aliyeko madarakani??
Nataka ushahidi wa hiyo stori yako ya kiongozi wa CCM kwenda chuoni kuhitaji million 60 na kupewa haraka,maana nyie kazi yenu siku hizi mmebakia kutunga tu mahabari Kama mtani wangu Erythrocyte
 
Nataka ushahidi wa hiyo stori yako ya kiongozi wa CCM kwenda chuoni kuhitaji million 60 na kupewa haraka,maana nyie kazi yenu siku hizi mmebakia kutunga tu mahabari Kama mtani wangu Erythrocyte
Ili iweje? Maana nikupe ushahidi ili ufanye nini??
 
Ukisoma kitabu cha Mario puzo cha godfather utajifunza kitu kwamba taasisi za serikal pamoja na wanaozoziongoza wamewekwa mfukoni na makundi machache nadiriki kuziita cartels kwa ajili ya maslahi ya wachache.wakati mwingine ukiona sera zinapitishwa na bunge usidhani ni kwa ajili ya maslahi ya wengi...kuwa vigilant
 
Tangu enzi za wizi wa Tangold na Meremeta, wizi wa fedha za Tegeta - Escrow na hata sasa wizi unaonekana kwenye Ripoti ya CAG, kila hatu ya wizi huo wahusika wakuu huwa ni wasomi wabobevu wa fani mbali mbali.

Swali linaloibuka ni kwamba wasomi wetu wanaisaliti nchi kwa kushindwa kutumia elimu waliyo nayo kwa maslahi ya nchi, au CCM ambao ndiyo wako madarakani wanawatumia wasomi wetu kuifilisi nchi?

Kuna kisa kimoja cha kweli cha mwanasiasa mmoja wa CCM mpenda kunyoa upara, kuwa wakati wa Kampeni za uchaguzi za Mwaka 2015 alikwenda kwenye chuo Kikuu kimojawapo cha Serikali na KUTAKA apewe shilingi milioni 60 kwa ajili ya Kampeni za CCM. Makamu wa Mkuu wa Chuo wakati huo aliomba apewe siku mbili awasiliane na wenzake, lakini bwana mkubwa huyo alitoa saa moja tu apewe hizo fedha.

Busar wa chuo alimwambia Makamu Mkuu wa chuo atoe hizo hela kwani akikataa hao jamaa wanao uwezo wa kumtoa yeye na kumteua mwingine ambaye atakuja kuwapa hizo hela. Mnyoa upara yule alipewa zile milioni 60 na kutokomea nazo. Mtaka hela msomi, mtoa hela msomi,lakini wote hawakufuata taratibu za fedha za chuo husika. Tatizo ni nini?
Baadhi ya matatizo ni haya hapa.
1) hatuna mfumo imara ambao unamuwezesha mtu kusimamia taasisi au ofisi ya imma kwa mujibu wa sheria na akawa huru kusema ndiyo au hapana kwa kuongozwa na sheria na taratibu husika.
2) Sheria nyingi pia zinatungwa zikiwa na matobo kwa hiyo kama msomi anakuwa mwepesi kuona matobo na kupitia hapo.
3)Uhalali wa watu wanaweza kuwajibisha yule aliyetumia mali ya umma ovyo.
Mfano:1: PAc na LAAc inasimamiwa na wabunge fulani, wanatakiwa wasiwe na doa lakini wao pia ndio hivyo unavyoona na kufahamu, maana yake na wao wananyooshewa vidole , sasa nani ni nani?
2: umesikia uamuzi wa mahakama kuu kwamba wabunge waliopata ubunge kwa kupita bila kupingwa ni kuvunja katiba.
Sasa huyu anakuwa na nguvu ipi ya kumsimamia yule ambaye angalau anafanya kazi kwa nafasi ya elimu yake? Na yote haya kama msomi anatambua.
Kwa hayo hapo
USHAURi wangu
1) Tunaowatuma kuhoji haya kwanza wanatakiwa kwanza wawe watu safi wasiotiliwa mashaka yoyote ya nafasi yake.
2)Sheria zetu zirekebishwe siyo kuegemea sana kwa mwenye mamlaka ya uteuzi.
3)Tujenge utamaduni wa kuwajibika na kuwajibishana
Na mengine mengi sana
Dawa ya yote haya ni msaafu wa nchi tu.
 
Busar wa chuo alimwambia Makamu Mkuu wa chuo atoe hizo hela kwani akikataa hao jamaa wanao uwezo wa kumtoa yeye na kumteua mwingine ambaye atakuja kuwapa hizo hela. Mnyoa upara yule alipewa zile milioni 60 na kutokomea nazo. Mtaka hela msomi, mtoa hela msomi,lakini wote hawakufuata taratibu za fedha za chuo husika. Tatizo ni nini?
Tatizo ni lile lile, uzao wa panya!
1681394576347.png
 
antimatter ina maana watanzania wote ni ukoo wa panya? Kwa ivo badala ya kuona tunakula visivyo vyetu basi tunatafuta nani wa kumfunga paka Kengele??
 
Back
Top Bottom