Wasomi wa PhD kulilia teuzi za utendaji/kisiasa ni tusi kwa wasomi

blessings

JF-Expert Member
Jul 9, 2012
6,983
6,237
Ni ukweli usiopingika kuwa PhD (ya kusomea, si ya kupewa) ndio shahada ya juu kabisa katika mfululizo wa elimu hapa duniani. Tena ukiipata unaheshimika na dunia ina matarajio makubwa sana kwako kwa kuzalisha maarifa, tafiti na huduma kwa jamii (inayokuzunguka na duniani kwa ujumla) inashangaza Afrika na hususani Tanzania wasomi hapa "hulilia" kuteuliwa katika nafasi za utendaji (kimsingi huitaji kuwa na PhD kupitia mafaili/kusaini ya watumishi) kwa vyeo vya wakuu wa wilaya, mkoa, kamishna, mkurugenzi, naibu/ katibu mkuu. Hili tusi kwa wasomi na wanetu/wadogo zetu kuonyesha kuwa hakuna thamani ya kuwa msomi kama utafanya kazi za watu wa kawaida. Narudia tena kazi za PhD holder si katika utendaji (kusaini barua) bali ni kufundisha, kufanya tafiti na huduma za kitaalam kwa jamii. Siasa na utendaji si kazi za hadhi yenu.
** Mawaziri & Manaibu (PhD) - 11
*** Makatibu Wakuu & Manaibu - 21
 
Ni ukweli usiopingika kuwa PhD (ya kusomea, si ya kupewa) ndio shahada ya juu kabisa katika mfululizo wa elimu hapa duniani. Tena ukiipata unaheshimika na dunia ina matarajio makubwa sana kwako kwa kuzalisha maarifa, tafiti na huduma kwa jamii (inayokuzunguka na duniani kwa ujumla) inashangaza Afrika na hususani Tanzania wasomi hapa "hulilia" kuteuliwa katika nafasi za utendaji (kimsingi huitaji kuwa na PhD kupitia mafaili/kusaini ya watumishi) kwa vyeo vya wakuu wa wilaya, mkoa, kamishna, mkurugenzi, naibu/ katibu mkuu. Hili tusi kwa wasomi na wanetu/wadogo zetu kuonyesha kuwa hakuna thamani ya kuwa msomi kama utafanya kazi za watu wa kawaida. Narudia tena kazi za PhD holder si katika utendaji (kusaini barua) bali ni kufundisha, kufanya tafiti na huduma za kitaalam kwa jamii. Siasa na utendaji si kazi za hadhi yenu.
** Mawaziri & Manaibu (PhD) - 11
*** Makatibu Wakuu & Manaibu - 21

Mfumo wa mishahara ndio uloharibu kila kitu.
Wenzetu walo kua wasomi wanapata mishara mikubwa na hawakimbiilii kutaka vyeo vya siasa.

Kwetu tanzania ukitaka kua tajiri haraka kuwa mbunge
 
Kwa level yetu ya elimu ukiacha waliosoma na kukulia elimu zao zote nje nchi, mtu mwenye phd anaweza kuwa sawa na mtu mwenye masters kwa kusoma na kuishi nchi za dunia ya kwanza. Nachosema ukimkuta mechanic engineer mwenye shahada ya kwanza yuko kampun ya tuseme mercedez benz, au GM motors hawez kulingana na hata engineer mweny masters hapa hata awe na experience. Kuna material mengi yana evaporate kutokea kwenye vitabu mpaka kwenye application, yakiingia kwenye atmosphrere ya Tanzania tu 15% inapungua, lugha 15% delivery, learning tools, boom na factor nyingine nyingi unajikuta ili uweze kuwa na weledi wa kawaida inabid uwe na phd.
 
halafu la kufurahisha eti PhD holder (Prof. ama Dr.) ni naibu katibu mkuu wakati waziri kamili ana Cheti (Wizara ya "VIWANJA") hapo lazima kuzugia katika fukuza fukuza tu maana ofisin hakukaliki. LUGHA GONGANA (upeo)
 
Ni ukweli usiopingika kuwa PhD (ya kusomea, si ya kupewa) ndio shahada ya juu kabisa katika mfululizo wa elimu hapa duniani. Tena ukiipata unaheshimika na dunia ina matarajio makubwa sana kwako kwa kuzalisha maarifa, tafiti na huduma kwa jamii (inayokuzunguka na duniani kwa ujumla) inashangaza Afrika na hususani Tanzania wasomi hapa "hulilia" kuteuliwa katika nafasi za utendaji (kimsingi huitaji kuwa na PhD kupitia mafaili/kusaini ya watumishi) kwa vyeo vya wakuu wa wilaya, mkoa, kamishna, mkurugenzi, naibu/ katibu mkuu. Hili tusi kwa wasomi na wanetu/wadogo zetu kuonyesha kuwa hakuna thamani ya kuwa msomi kama utafanya kazi za watu wa kawaida. Narudia tena kazi za PhD holder si katika utendaji (kusaini barua) bali ni kufundisha, kufanya tafiti na huduma za kitaalam kwa jamii. Siasa na utendaji si kazi za hadhi yenu.
** Mawaziri & Manaibu (PhD) - 11
*** Makatibu Wakuu & Manaibu - 21
Mkuu ukisema p
PhD ya kupewa una maana gani labda tupe mfano
 
  • Thanks
Reactions: SDG
halafu la kufurahisha eti PhD holder (Prof. ama Dr.) ni naibu katibu mkuu wakati waziri kamili ana Cheti (Wizara ya "VIWANJA") hapo lazima kuzugia katika fukuza fukuza tu maana ofisin hakukaliki. LUGHA GONGANA (upeo)
Teeeeeeeeh teeeeeeeeh teeeeeeeeeh teeeeeh wizara ya viwanjaaaa
 
Acha wivu wa zamani. Zamani ukiajiriwa ulikuwa hurusiwi kwanda kusoma eti kwa vile wao walifanya miaka 15 kwanza na dip ndo akaenda digrii ya kwanza.

Samahani kwa kuanza na hilo.

Angalia profiles za Mawaziri wote wa Marekani utajua wana zaidi ya PhD. Hawa ni watafiti wakubwa sana katika maeneo wanayofanyia kazi. Na pia wanaendelea kufundisha katika vyuo na taasisi mbalimbali.

Sinda yetu inaweza kuwa tu ubora wa PhD zetu. Ambazo naona shida kwetu ni vitendea kazi. Mtu baada ya kumaliza na kuajiriwa anashindwa hata kurudia kitu alichofanya au anaishia kwenye theories.
 
  • Thanks
Reactions: SDG
Waziri wa "VIWANJA" nomaaa. Watendaji jiandaeni kufukuzwa sana aisee maana mkulu kiti cha moto so lazima kuzugia humo humo leo kafukuzwa huyu kesho yule basi vurugu mechi tu. Kutokuwa na elimu mbele ya msomi wa PhD kunatiaga ubaridi/unyonge sana kama hamjui ndo muelewe.
 
  • Thanks
Reactions: SDG
Siasa inalipa sana Tanzania, ndio maana wanatumia hela nyingi sana wakati wa kampen na wanapokosa ubunge au ukuu wa mkoa wanakuwa maskini. Siasasio ajira permanent kama ilivyo watumishi wa umma. Its only 5years term, then ukishindwa unarudi kuendelea na shughuli zako nyingine. Kwa mfano Ndesamburo, Dr Slaa tunategemea kwasasa anaandika vitabu au tafiti mbalimbali au kufundisha. Hebu mwangalie Lawrence Masha kwasasa anafanya nini? Wasira yuko mahakamani anahangaika arudi kwa hawajui nini cha kufanya. Wako wengi, have something before you engage in politics! Then after that you go back na hapo hakutakuwa na kunyenyekeana.
 
Siasa inalipa sana Tanzania, ndio maana wanatumia hela nyingi sana wakati wa kampen na wanapokosa ubunge au ukuu wa mkoa wanakuwa maskini. Siasasio ajira permanent kama ilivyo watumishi wa umma. Its only 5years term, then ukishindwa unarudi kuendelea na shughuli zako nyingine. Kwa mfano Ndesamburo, Dr Slaa tunategemea kwasasa anaandika vitabu au tafiti mbalimbali au kufundisha. Hebu mwangalie Lawrence Masha kwasasa anafanya nini? Wasira yuko mahakamani anahangaika arudi kwa hawajui nini cha kufanya. Wako wengi, have something before you engage in politics! Then after that you go back na hapo hakutakuwa na kunyenyekeana.
umeongea point ya msingi sana nchi nyingi zilizoendelea watu wanaanza kwy prof.zao kwanza halafu wakishakuwa succesful ndio wanakwenda kwy politics kwa jili ya payback to the community kwa muda maalum kabla hajarejea kwy kazi yake ya msingi. hapa Tanzania mtu kama Nape has never held a really job in his entire life when he got booted out from gov paycheck he has nothing to go back to. anabaki mahakamani kama Wasira kujaribu kurudia mizoga aliyoiacha nyuma.
 
  • Thanks
Reactions: ydn
PhD holders wanamajukumu makuu ya aina tatu, Academics,Research/Innovation na Consultancy. Pamoja na kuwa weledi wao unawalazimisha kutumia muda wao zaidi katika kutoa maarifa yao kwa jamii kama vile kufundisha na kuresearch ila pia wanajukumu la kusaidia jamii katika ushauri na usimamizi ya kazi zinazohusiana na taaluma yao, kwahiyo anaweza kuchaguliwa kuwa waziri/katibu mkuu.... Hasa akifanya kazi hizo katika eneo alilobobea tunaamini atafanya vzr kuliko mtu asiye na ubobezi wa kutosha ktk sekta hiyo
 
Wasomi wetu fungukeni kama wenzetu hapa hapa Afrika (Nigeria, Kenya na Afrika kusini & Misri) fanyeni tafiti za maana, acheni kulilia UKUU WA WILAYA.

Funguka zaidi, siyo kulaumu tu kama ilivyo tabia ya watanzania. Huko Kenya, Nigeria na Afrika kusini wamefanya tafiti zipi unazozijua wewe?
 
  • Thanks
Reactions: SDG
Back
Top Bottom