Wasira Kuna Njaa Kila Kona Nchini Acha UTYSON kwa Kuishi Ulimwengu wa Takwimu

Uwezo Tunao

JF-Expert Member
Nov 14, 2010
6,942
1,190
Wassira achukizwa Dk Slaa

Wednesday, 16 March 2011 20:02



Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais (Uratibu na Uhusiano), Steven Wassira

Sosthenes NyoniWAZIRI wa Nchi, Ofisi ya Rais (Uratibu na Uhusiano), Steven Wassira, amemtaka Katibu Mkuu wa Chadema,Dk Willibrod Slaa, kutumia elimu yake ya udaktari kuzungumza mambo ya kitaalamu badala ya kutaka kusikika.

Akizungumza kwenye mahojiano maalum na Kituo cha televisheni ya ITV juzi, Wassira alisema kinachofanywa na Dk Slaa ni kutaka kusikika.

"Kitendo cha Dk Slaa kupita jimboni kwangu Bunda na kuwaambia wananchi kwamba mimi sifai kwa kuwa nimewasababishia njaa, kinaonyesha jinsi anavyoshindwa kutumia taaluma yake kujenga hoja za msingi," alisema Wassira.

Kwa mujibu wa Wassira, Dk Slaa aliwaeleza wananchi hao kuwa amewaletea njaa licha ya kwamba alikuwa Waziri wa Kilimo, Chakula na Umwagiliaji."Simwelewi Dk Slaa, siasa sio kuzungumza zungumza tu hata kama huna hoja za msingi.

Kwanza yeye ni daktari halafu ni mtu mzima, anawaambia wananchi wangu kule Bunda kwamba mimi nimeleta njaa," alisema Wassira na kuhoji:"Amefanya utafiti akabaini njaa ya Bunda sababu ni mimi?

Sasa kuna Jumanne Magembe na Mwanga kuna ukame, je yeye ndio kasababisha?Wassira alisema akiwa waziri mwenye dhamana ya kuwatumia Watanzania wote, asingeweza kuchukua raslimali za sehemu nyingine na kuzipeleka Bunda kama Dk Slaa anavyotaka, isipokuwa maendeleo ya Bunda yatapatikana kwa jitihada za pamoja kati yake na wakazi wa jimbo hilo."Yeye anafikiri ukiwa waziri basi unaweza kufanya chochote.

Maendeleo ya jimbo yanapatikana kwa mipango na ushirikiano kati ya mbunge na wakazi wa jimbo husika. Huwezi kuchukua rasilimali za sehemu nyingine ya nchi na kuzipeleka kwenu, eti ukawafurahishe wananchi wakati umebeba dhamana ya Watanzania wote," alisema Wassira.

Pia, Wassira aliwataka viongozi wa Chadema kuacha sera za kuhamasisha wananchi kuondoa madarakani serikali iliyopo kwa njia ya maandamano.

Alisema sio sahihi kulinganisha mfumo wa siasa ya Tanzania na nchi kama Misri au Libya kwa sababu, hapa muda uliowekwa kikatiba kwa Rais kukaa madarakani ni miaka 10.Mwisho

SOURCE: Mwananchi
 
WASIRA TAIFA LA BUNDA NAKO KUNA NJAA KALI SAWA NA KOTE HUKU TANZANIA:
TAFADHALI ACHANA NA MAMBO YA UTAALAM WA KUJENGA HOJA KWA
WENZIO TUNAKUFA NA NJAA


Ni kwa miaka mingi sana viongozi wetu hasa wa upanda wa CCM wamekua wakipoteza muda wao mwingi kuwekeza kwenye kutafuta kwa bidii sana UTAALAM WA KUJENGA HOJA ZA NGUVU mbele ya macho ya umma huku maendeleo yakizidi kuwa ndoto kila kukicha.

Kwa ulimbukeni mkubwa zaidi, pia tunawafahamu baadhi yao hawa viongozi wa CCM ambao lao ni kujaribu kila wakati KUONEKANA KWENYE MAZUNGUMZO YAO WAKIZUNGUMZA KAMA MWALIMU NYERERE lakini kwa bahati mbaya sana matendo yao kila kukicha huwasaliti sana maana Baba wa Taifa alikua ni mtaalam wa kujenga hoja na ni muadilifu pia wa matendo.

Ajabu na kweli ni kwamba njaa ilivyopamba moto nchini na ugumu wa maisha kutukaba kila kona nchini huu Mhe Wasira yeye anataka kutuaminisha ya kwamba yeye kama waziri akishiba na familia yake basi tayari Wa-Tanzania wooote wa kule Taifa la Bunda nao tayari wanakua wamejishibia hivyo yote anayozungumza Dr Slaa ni kujifurahisha tu mdomo na 'kujitafutia sifa' tu.

Ukweli ni kwamba kama huko Bunda hakuna njaa na wote wamejitosheleza kama waziri huyu basi pale pale wangemuumbua Dr Slaa na kumfunulia mitumbo iliojaaa neema ili aweze kujithibitishia walivyoshibishwa vilivyo na Stephano Tyson Wasira.

Kama hilo halitoshi, kwake yeye Mzee Wasira SUALA LA CHAKULA WALA SI SWALA LA MSINGI KWAKE hivyo halikufaa kamwe kuzungumziwa na CHADEMA baada ya kulitembelea hilo taifa lake. Hata hivyo, kitaaluma alivyotaka Wasira, somo la Biashara kule shule za sekondari linatukumbusha kwamba kati ya MAHITAJI YA MSINGI MNO ILI MAISHA YA binadamu yaweze kuendelea vema ni pamoja na (1) Chakula, (2) Malazi na (3) Mavazi.

Sasa taaluma ya PhD ya Dr Slaa kutokuzungumzia vema SWALA NYETI LA NJAA BUNDA ni kwamba alikosa kutumia takwimu kudanganyia wenye njaa kwamba wala hakuna njaa nchini au ndio kusemaje kote hapa???

Wa-Tanzania TUWAKATAE KABISA VIONGOZI WANAOJIBIDISHA KILA LEO KUPATA UBUNGWA WA KUJENGA HOJA namna gani kutudanganya na maneno matupu au takwimu hewa zisizoendana na hali halisi maisha tunayoishi kama ambavyo Wasira angetamani Dr Slaa amuokolee sura kule Bunda kwa kuwadanganya wananchi wale wakati ukweli ni kilio cha njaa na maisha magumu kote nchini kufuatia UFISADI WA KUTISHA unaoendelezwa na CCM nchini!!!
 
CCM 2011 NA MAKAMBI YAKE MBALI MBALI NCHINI

Mhe Wassira kati ya hizi CCM mbali mbali hivi sasa nchini huko kwenu katika Taifa la Bunda kusikojulikana njaa wala 'wageni' wasije kuzungumzia NJAA kama kero sugu kwa wananchi, hivi enyi mko kwenye mchepuo gani hapa chini???

1. CCM- Uadilifu (Wazee wenzake na Mwalimu Nyerere ambao ni watulivu, wakomavu na masikini wa kutupwa kwa kuipenda sana nchi na wenye moyo kuitetea Tanzania).

2. CCM- Ufisadi ( Ni kundi dogo linalojiita Wanamtandao au kumbakumba wa kila dili / mchecheto wa kila senti irukayo hewani wenye utayari wa kuuza hata mtoto wake alimradi fedha ipatikane zaidi kufanyia kila aina ya uchafu unaoweza kufikiria; ni wale ambao mpaka hivi sasa wamepepetwana pembeni wasio na kitu na kubakia RA + EL).

3. CCM-Unguja (Chama cha Wazanzibara kama Vuai wa Kondoa na Hussein Mwinyi wa Kisarawe Umatumbini).

4. CCM-Yatima (Ni wale akina Sumaye, Kigoda, Mungai, banduka, Komanya, Ngulume, na wengine waliokua chini ya BWM).

5. CCM-Bongo Flava (Rizi1, Februari Ma-Ropes, Ndungai, Malisa, Nchimbi, ... hawa hawana hela ila kamsimamo wa uongo na kweli)

6. CCM-Mwandosya / Mangula (Kanda ya Juu Kusini)

7. CCM- Six/John Liquor Ma-Padlocks (Kanda ya Ziwa)

8. CCM- Two Coins Mramba / Mrema / Mbatia (moshi Vijijini)

9. CCM-Uislamu (Pwani/ Tanga / Mashariki na Pemba)

Sasa hapa mtu unapoongelea CCM ni sharti uwe makini sana sana na ijulikane kwamba unazungumzia CCM ipi hasa.
 
Back
Top Bottom