Wasaka ubunge ndani ya CHADEMA waanza kumzidi nguvu Tundu Lissu

Missile of the Nation

JF-Expert Member
May 24, 2018
13,505
51,109
Ni dhahiri ndani ya CHADEMA watu wanachekeana usoni ila mioyoni mwao watu wanapiga mahesabu ya 2025.

Baada ya uchaguzi wa 2020, Kamati kuu ya chama hicho ilitoa msimamo kuwa hakuna kushiriki uchaguzi wowote ujao bila uwepo wa Katiba mpya yenye Tume huru ya Uchaguzi.

Mwanzoni kabisa, msimamo huu ulitetewa kwa nguvu zote na makada na viongozi wa juu wa chama hiki. Lakini kadri siku zinavyosogea, Sura halisi ya viongozi hawa imeanza kuonekana. Wameanza kama kawaida yao kubadili msimamo huo taratiiib kwa kutuma meseji kuwa watashiriki ktk uchaguzi huo bila hata ya uwepo wa Katiba Mpya.

Hili limedhihirika katika ziara ambazo viongozi hawa wakubwa wa CHADEMA wataka ubunge wanazofanya mikoani. Sasa hivi hawaongei tena suala la kupatikana kwa Katiba Mpya kwanza ili kushiriki uchaguzi, Sasa hivi wanaongea namna watakavyorudi Bungeni mwaka 2025!

Hapo awali katika kutetea uamuzi wa kamati kuu wa kutoshiriki uchaguzi mkuu bila Katiba Mpya, walisema kuwa practically katika nchi hii haiwezekani kufanya uchaguzi huru na haki bila katiba mpya iliyobora kuliko ya sasa. Lakini cha ajabu ni kwamba CHADEMA sasa inadhani raia wamesahau "elimu" hii waliyoitoa, wanadhani raia mwaka 2025 wanaweza kuwachagua achilia mbali kujitokeza kwa wingi kushiriki uchaguzi ambao wameshaambiwa na haohao CHADEMA kuwa hauwezi kuwa huru na haki.

Kiongozi mkubwa wa CHADEMA aliyeshiriki kutoa elimu ya ubovu wa katiba ya sasa na kutofaa kwake katikauchaguzi ni Tundu Lissu, alifanya kazi hiyo kwa moyo mmoja na kwa weledi kabisa, Lakini inavyoonekana ni kwamba kuna kundi la viongozi wenzie ndani ya CHADEMA wanaona kuwa mwaka 2025 wana nafasi ya kurudi bungeni, na hawa ndo wanachombezachombeza kama siyo kushinikiza chama kiingie katika uchaguzi ili wapate ubunge tena ili wakalambe asali kama wenzao wa CCM.

CHADEMA inajulikana vyema kwenye kubadili gia angani, pale inapokana misimamo thabiti yenye maana na kukumbatia vitu vya kupita vyenye manufaa ya muda mfupi kwa nchi na chama chao. Walifanya hivyo pale walipoikana ajenda yao ya Ufisadi pale walipomkabidhi kijiti mtu waliyemuita fisadi kwa miaka zaidi ya Nane kuwa mgombea urais wa chama chao. Wao walikuwa wanawaza kutwaa madaraka tu kwa udi na uvumba bila kujali wanayetaka kumuweka madarani ni nani hata kama Chadema wanajua wazi kuwa ni fisadi na pia waliutangazia umma wao wenyewe hilo suala.

Leo wanatambua kabisa kuwa bila uwepo wa katiba mpya uchaguzi ujao bado utakuwa feki lakini wao kwa sababu wanadhani kuwa wana chance ya kurudi bungeni kula baada ya JPM kufariki, hata hizo conditions za kutoshiriki uchaguzi mpaka ipatikane katiba mpya yenye tume huru ya uchaguzi hawana mpango nazo tena.

Leo CHADEMA inasound kama chama cha ACT, viongozi wake wanasema kuwa ili washiriki uchaguzi "Mchakato" wa katiba uanze lakini Tuanze na Tume huru ya uchaguzi kwanza. Ningependa kuwauliza viongozi wa CHADEMA hasa Tundu Lissu, ni nani alimwambia kuwa "Mchakato wa katiba" ndo katiba mpya yenyewe?.

Pili nani kawawmbia CHADEMA kuwa uwepo wa mchakato wa katiba bila katiba mpya ndo guarantee ya Uchaguzi Huru na haki mwaka 2025?

Mimi ningewaona CHADEMA wako serious na wana nia njema kabisa ya kusimamia kile walichokitangaza kwa umma baada ya uchaguzi wa hovyo wa 2020 kwa kusema kuwa ni heri katiba ya sasa ibadilishwe, Uchaguzi wa 2025 usogezwe mbele, ili tutafute katiba mpya kwanza halafu sote tuje tushiriki uchaguzi chini ya Katiba Mpya iliyobora.

Lakini hizi habari za kuuambia umma kuwa bila katiba mpya uchaguzi hauwezi kuwa huru na haki halafu baadae baada ya Rais Samia kuanza kuwapetipeti wanakuja kutwambia jinsi Samia alivyo raisi mzuri na hivyo basi kubadili gia angani na kusema uchaguzi unawezekana chini ya katiba hii mbovu ni kuwacheza shere wananchi, kudharau wanachama wake na kutokujua unapigania nini.

CHADEMA imekuwa ikisema kuwa hata kama una tume huru ya uchaguzi lakini as long as hakuna mahakama huru, Jeshi la Polisi huru huwezi kupata uchaguzi huru na haki chini ya katiba hii. Nashangaa sasa wazee wa kubadili gia angani wameshasahau nondo walizokuwa wakishusha kuelimisha watu juu ya hili.

Watanzania makini tunasema, bila Katiba Mpya Uchaguzi wowote ujao ni feki.
 
Mbowe aliwahi kusema kuna timu itaundwa kila mkoa kwa ajili ya kutoa elimu hiyo, sijui itaundwa lini, au kama imeshaundwa, lini itaanza kazi.

Inavyoonekana kuondoka kwa Lissu ghafla naona sasa kunaanza kuzua maswali, kama ni kweli aliondoka kwa sababu za matibabu, au palikuwepo na sababu nyingine nyuma ya pazia, time will tell.
 
Msimamo unaweza kuwa sahihi mda huo kitokana na Hali iliyokuwepo lakini kwa Sasa at least mamboo yamebadilika
 
Wewe baki na msimamo wako na Chadema waache na msimamo wao. Siamini kama kususia uchaguzi itakuwa na tija kwani CCM wataendelea ku dominate siasa za nchi na Chadema itakuwa imejizika rasmi. Kama awali walisema hawatashiriki na sasa wameona mazingjra ya kisiasa yamebadilika na wao wamebadili msimamo hakuna dhambi hapo. Matokeo ya mwisho ndiyo yatatoa jibu kama wako sahihi au hapana.

Sent from my Nokia 5.1 Plus using JamiiForums mobile app
 
Tafsiri yake ngumu kweli ,baada ya wikimbili (yaweza kua miaka)
Inawezekana Lissu keshastukia kuwa baadhi ya wenzie ndani ya Chadema wapo after Ubunge tu, kwao katiba mpya ni muhimu kama ubunge wao umeporwa, ila kama ubunge wao wanapewa basi hewala hata katiba hii ya sasa iliendelea kuwepo kwa miaka zaidi ya 100 kwao siyo ishu.
 
Ni dhahiri ndani ya CHADEMA watu wanachekeana usoni ila mioyoni mwao watu wanapiga mahesabu ya 2025.

Baada ya uchaguzi wa 2020, Kamati kuu ya chama hicho ilitoa msimamo kuwa hakuna kushiriki uchaguzi wowote ujao bila uwepo wa Katiba mpya yenye Tume huru ya Uchaguzi.

Mwanzoni kabisa, msimamo huu ulitetewa kwa nguvu zote na makada na viongozi wa juu wa chama hiki. Lakini kadri siku zinavyosogea, Sura halisi ya viongozi hawa imeanza kuonekana. Wameanza kama kawaida yao kubadili msimamo huo taratiiib kwa kutuma meseji kuwa watashiriki ktk uchaguzi huo bila hata ya uwepo wa Katiba Mpya.

Hili limedhihirika katika ziara ambazo viongozi hawa wakubwa wa CHADEMA wataka ubunge wanazofanya mikoani. Sasa hivi hawaongei tena suala la kupatikana kwa Katiba Mpya kwanza ili kushiriki uchaguzi, Sasa hivi wanaongea namna watakavyorudi Bungeni mwaka 2025!

Hapo awali katika kutetea uamuzi wa kamati kuu wa kutoshiriki uchaguzi mkuu bila Katiba Mpya, walisema kuwa practically katika nchi hii haiwezekani kufanya uchaguzi huru na haki bila katiba mpya iliyobora kuliko ya sasa. Lakini cha ajabu ni kwamba CHADEMA sasa inadhani raia wamesahau "elimu" hii waliyoitoa, wanadhani raia mwaka 2025 wanaweza kuwachagua achilia mbali kujitokeza kwa wingi kushiriki uchaguzi ambao wameshaambiwa na haohao CHADEMA kuwa hauwezi kuwa huru na haki.

Kiongozi mkubwa wa CHADEMA aliyeshiriki kutoa elimu ya ubovu wa katiba ya sasa na kutofaa kwake katikauchaguzi ni Tundu Lissu, alifanya kazi hiyo kwa moyo mmoja na kwa weledi kabisa, Lakini inavyoonekana ni kwamba kuna kundi la viongozi wenzie ndani ya CHADEMA wanaona kuwa mwaka 2025 wana nafasi ya kurudi bungeni, na hawa ndo wanachombezachombeza kama siyo kushinikiza chama kiingie katika uchaguzi ili wapate ubunge tena ili wakalambe asali kama wenzao wa CCM.

CHADEMA inajulikana vyema kwenye kubadili gia angani, pale inapokana misimamo thabiti yenye maana na kukumbatia vitu vya kupita vyenye manufaa ya muda mfupi kwa nchi na chama chao. Walifanya hivyo pale walipoikana ajenda yao ya Ufisadi pale walipomkabidhi kijiti mtu waliyemuita fisadi kwa miaka zaidi ya Nane kuwa mgombea urais wa chama chao. Wao walikuwa wanawaza kutwaa madaraka tu kwa udi na uvumba bila kujali wanayetaka kumuweka madarani ni nani hata kama Chadema wanajua wazi kuwa ni fisadi na pia waliutangazia umma wao wenyewe hilo suala.

Leo wanatambua kabisa kuwa bila uwepo wa katiba mpya uchaguzi ujao bado utakuwa feki lakini wao kwa sababu wanadhani kuwa wana chance ya kurudi bungeni kula baada ya JPM kufariki, hata hizo conditions za kutoshiriki uchaguzi mpaka ipatikane katiba mpya yenye tume huru ya uchaguzi hawana mpango nazo tena.

Leo CHADEMA inasound kama chama cha ACT, viongozi wake wanasema kuwa ili washiriki uchaguzi "Mchakato" wa katiba uanze lakini Tuanze na Tume huru ya uchaguzi kwanza. Ningependa kuwauliza viongozi wa CHADEMA hasa Tundu Lissu, ni nani alimwambia kuwa "Mchakato wa katiba" ndo katiba mpya yenyewe?.

Pili nani kawawmbia CHADEMA kuwa uwepo wa mchakato wa katiba bila katiba mpya ndo guarantee ya Uchaguzi Huru na haki mwaka 2025?

Mimi ningewaona CHADEMA wako serious na wana nia njema kabisa ya kusimamia kile walichokitangaza kwa umma baada ya uchaguzi wa hovyo wa 2020 kwa kusema kuwa ni heri katiba ya sasa ibadilishwe, Uchaguzi wa 2025 usogezwe mbele, ili tutafute katiba mpya kwanza halafu sote tuje tushiriki uchaguzi chini ya Katiba Mpya iliyobora.

Lakini hizi habari za kuuambia umma kuwa bila katiba mpya uchaguzi hauwezi kuwa huru na haki halafu baadae baada ya Rais Samia kuanza kuwapetipeti wanakuja kutwambia jinsi Samia alivyo raisi mzuri na hivyo basi kubadili gia angani na kusema uchaguzi unawezekana chini ya katiba hii mbovu ni kuwacheza shere wananchi, kudharau wanachama wake na kutokujua unapigania nini.

CHADEMA imekuwa ikisema kuwa hata kama una tume huru ya uchaguzi lakini as long as hakuna mahakama huru, Jeshi la Polisi huru huwezi kupata uchaguzi huru na haki chini ya katiba hii. Nashangaa sasa wazee wa kubadili gia angani wameshasahau nondo walizokuwa wakishusha kuelimisha watu juu ya hili.

Watanzania makini tunasema, bila Katiba Mpya Uchaguzi wowote ujao ni feki.

Ninaunga mkono hoja. Kwa hakika umedadavua vyema.

Niliwahi kuandika uzi huu wenye kushahibika Aug 2022:

Magumu yetu Viongozi wa Upinzani mkwepe lawama vipi?

Aya hii ikiwa ni nukuu humo:

"Viongozi wanaohofia kufa au jela tafadhali wapishe madarakani. Damu mpya zipo. Hatuhitaji vyama vipya. Tubanane na hawa hawa. Hawataki kutoka madarakani, shime wanathaura tuanze kwa kuwafurusha wao kwanza."

Hiki chama wametoka nacho mbali na ni kweli wameteseka sana.

Haitoshi kuishia hapo. Hata siye tumetoka nacho mbali na tumeteseka sana. Kwamba hatujuani tokea kwenye ID za mchongo tusitishane kwani hatujuani.

Tunao wajibu wa kuwataka walioko uongozini kufanya tunayoyataka sisi kama wanachama.
 
Mbowe aliwahi kusema kuna timu itaundwa kila mkoa kwa ajili ya kutoa elimu hiyo, sijui itaundwa lini.

Inavyoonekana kuondoka kwa Lissu ghafla sasa kunaanza kuzua maswali

Ninadhani pana ombwe la kukosekana chief strategist wa chama. Chief strategist si kiungozi huyo ni mpanga mikakati kama ilivyokuwa kocha wa mpira.

Kiongozi wa chama hawezi kuwa mpanga mikakati. Kiongozi huweka malengo ya chama.

Magumu yetu Viongozi wa Upinzani mkwepe lawama vipi?

Tufike mahala tumfunge paka kengele.
 
Jifunze ku summarise. Itawasaidia wasomaji wako kujua whats your point.
Hakuna mtu ana muda wa kusoma andiko reefu. People want points.
Kwa ufupi|
=
Hili ni bandiko kuwahusu CHADEMA, chama kikuu cha upinzani nchini Tanzania. Baada ya uchaguzi mkuu wa 2020, kamati kuu ya chama hicho ilisema kuwa hawatahudhuria uchaguzi wowote ujao bila katiba mpya yenye tume huru ya uchaguzi. Hata hivyo, viongozi wa CHADEMA sasa wanabadili msimamo huo na kuongea juu ya kushiriki uchaguzi wa mwaka 2025 bila uwepo wa katiba mpya. Wakati mwingine, wanaonekana kubadili msimamo mara kwa mara na kukumbatia mambo ya kupita yenye manufaa ya muda mfupi kwa nchi na chama chao.
=
Ila mleta mada bado anatuachia maswali mengi zaidi.
 
Tulia mjomba hii ngoma siyo saizi yenu. Makwetu ambako chawa na kinguni hawana nafasi kujipanga, kujikosoa na kufanya maboresho hakunaga mwisho.

Mstari wa chino, bila katiba mpya hakuna uchaguzi mkuu.
Katiba mpya ataleta Lema?
 
Mbowe aliwahi kusema kuna timu itaundwa kila mkoa kwa ajili ya kutoa elimu hiyo, sijui itaundwa lini.

Inavyoonekana kuondoka kwa Lissu ghafla sasa kunaanza kuzua maswali
Mbona una presha sana, ziara iliyobaki Bado magharibi, Kanda ya kati, kusini, kaskazini n.k wakishazindua mikutano Kila Kanda ndio Sasa hizo timu za katiba mpya zitaundwa.

What's the rush, everything is under control.
 
Back
Top Bottom