Mcheza Karate
JF-Expert Member
- Jun 30, 2011
- 690
- 350
Mpendwa rais wangu, je unakumbuka kuwa ulivyoingia madarakani mwaka 2005 watu tulikuamini sana na ukawa kama "mwenzetu?"
unakumbuka ulikuwa maarufu kuliko hata chama chetu(CCM) kwa wakati ule?
Je unakumbuka vizuri ulituahidi nini waTANZANIA?
Je unakumbuka uliwaahidi nini waislamu?
Unakumbuka wewe na tema member wako kinana uliwaahidi waislamu Kupitia BAKWATA kuwa utawapatia waislamu Mahakama ya kadhi na na Tanzania kujiunga na OIC?
Je si unakumbuka uliahidi kuwapa nafasi nyingi waislamu ktk uongozi? Umesahau?
Je unakumbuka kuwa uliahidi kukipanua chuo kikuu cha kiislamu Morogoro? Vipi tayari umeshapanua?
Rais wangu mpendwa wewe ni mdini na naomba ujue hivyo. Umetupandia mbegu mbaya sana na hadi sasa binafsi nina mashaka sana na wewe.
Kumbuka mwaka 2010 ktk kampeni zako za uchaguzi (ulieneza kwa maksudi au kushawishiwa na kinana) propaganda ya udini.
Si ulituambia waislamu kuwa tusichague Chama ambacho mgombea wake ni padri kwani wana lao jambo? Tukuchague wewe ambaye ni muislamu "MWENZETU"?
Umeona mbegu uliyopanda BAKWATA wakaipalilia, wakaeneza ujumbe huu misikitini? Au hukuwatuma wewe? Walijitungia kwa vile nayo BAKWATA ni TAASISI ya serikali?
Mpendwa rais wangu unakumbuka mara baada ya uchaguzi ulisema udini ulishamiri sana. Je ulivyowaita mashehe na maaskofu ndo basi? Mbona wote wapo uraiani na kinyongo? Kila mmoja wao anasema lake la kukulaumu?
Mpendwa rais, je una habari kuwa radio iman imefungiwa? Unajua shehe ponda yuko mahabusu na amenyimwa dhamana?
Mbona uko kimya? "UMETUSALITI"? Si uliahidi utakuwa bega kwa bega na sisi?
Hivi umewahi kusikiliza malalamiko ya wakristu kuwa bwana mkubwa unaongoza kwa upendeleo na ushabiki wa kidini? Umewahi kuwaita maaskofu ikulu ukanywa nao chai huku wakikueleza unapoteleza?
Mpendwa rais wangu, je huogopi hali ilivyo hivi sasa? Je wakristu hawatatupiga mapanga waislamu na waislamu hatutawachoma visu wakristu?
Je kwa ahadi ulizoahidi kuwatekelezea waislamu na ulivyo mgumu kuzitekeleza huoni ipo siku TUTACHOKA?
Mpendwa rais, kwanini wasaidizi wako wanakuogopa sana kukuambia ukweli? Au unawachagua ambao watakuridhisha ktk kauli zao tu?
Kwa nini unamtumia wassira kumaliza migogoro ya udini huku ukijua fika "WASSIRA ANAKUOGOPA?" Na si unajua Wassira huwa hakubali kushindwa anapotatua mizozo au migogoro?
Si unajua Wassira huwa anajiona mnyonge pale anaposhindwa na kuona kushindwa kwake ni kushindwa kwa serikali?
Kwa nini usiwatumie watu makini kumaliza tatizo la udini? Kwani suluhu inatafutwa na mawaziri tu? Kwa nini usiunde tume ikaja na majibu na mapendekezo juu ya mtafaruku huu baina yetu waislamu na wakristu?
Au kwako hili ni dogo tu na kama UPEPO WA SIASA UNAOPITA? Hivi ni nani huwa anakushauri ktk mambo yanayohitaji maamuzi magumu?
Mpendwa rais, unajua kikundi cha Boko haram kilianzaje? Unajua historia ya Alqaida au alshaabab? Punguza presha rais wangu. Kaa chini tulia jipange, tatua huu mzozo mapema.
Kama wasaidizi wako wanakudanganya kuwa tatizo la udini ni dogo hivi sasa na halina madhara basi amini wanaogopa kukuambia ukweli kwa vile wewe mwenyewe ndio mpandaji wa mbegu hii.
mpendwa rais, nakusihi kuwa macho na chuki za udini. Tunaipenda Tanzania, hatutaki tuipoteze.
Unafanya juhudi gani kuondoa udini huu? Na je UTAWEZA?
"wahadha assalam alleykum, wabilah taufiq"
Tafakari!!!!
unakumbuka ulikuwa maarufu kuliko hata chama chetu(CCM) kwa wakati ule?
Je unakumbuka vizuri ulituahidi nini waTANZANIA?
Je unakumbuka uliwaahidi nini waislamu?
Unakumbuka wewe na tema member wako kinana uliwaahidi waislamu Kupitia BAKWATA kuwa utawapatia waislamu Mahakama ya kadhi na na Tanzania kujiunga na OIC?
Je si unakumbuka uliahidi kuwapa nafasi nyingi waislamu ktk uongozi? Umesahau?
Je unakumbuka kuwa uliahidi kukipanua chuo kikuu cha kiislamu Morogoro? Vipi tayari umeshapanua?
Rais wangu mpendwa wewe ni mdini na naomba ujue hivyo. Umetupandia mbegu mbaya sana na hadi sasa binafsi nina mashaka sana na wewe.
Kumbuka mwaka 2010 ktk kampeni zako za uchaguzi (ulieneza kwa maksudi au kushawishiwa na kinana) propaganda ya udini.
Si ulituambia waislamu kuwa tusichague Chama ambacho mgombea wake ni padri kwani wana lao jambo? Tukuchague wewe ambaye ni muislamu "MWENZETU"?
Umeona mbegu uliyopanda BAKWATA wakaipalilia, wakaeneza ujumbe huu misikitini? Au hukuwatuma wewe? Walijitungia kwa vile nayo BAKWATA ni TAASISI ya serikali?
Mpendwa rais wangu unakumbuka mara baada ya uchaguzi ulisema udini ulishamiri sana. Je ulivyowaita mashehe na maaskofu ndo basi? Mbona wote wapo uraiani na kinyongo? Kila mmoja wao anasema lake la kukulaumu?
Mpendwa rais, je una habari kuwa radio iman imefungiwa? Unajua shehe ponda yuko mahabusu na amenyimwa dhamana?
Mbona uko kimya? "UMETUSALITI"? Si uliahidi utakuwa bega kwa bega na sisi?
Hivi umewahi kusikiliza malalamiko ya wakristu kuwa bwana mkubwa unaongoza kwa upendeleo na ushabiki wa kidini? Umewahi kuwaita maaskofu ikulu ukanywa nao chai huku wakikueleza unapoteleza?
Mpendwa rais wangu, je huogopi hali ilivyo hivi sasa? Je wakristu hawatatupiga mapanga waislamu na waislamu hatutawachoma visu wakristu?
Je kwa ahadi ulizoahidi kuwatekelezea waislamu na ulivyo mgumu kuzitekeleza huoni ipo siku TUTACHOKA?
Mpendwa rais, kwanini wasaidizi wako wanakuogopa sana kukuambia ukweli? Au unawachagua ambao watakuridhisha ktk kauli zao tu?
Kwa nini unamtumia wassira kumaliza migogoro ya udini huku ukijua fika "WASSIRA ANAKUOGOPA?" Na si unajua Wassira huwa hakubali kushindwa anapotatua mizozo au migogoro?
Si unajua Wassira huwa anajiona mnyonge pale anaposhindwa na kuona kushindwa kwake ni kushindwa kwa serikali?
Kwa nini usiwatumie watu makini kumaliza tatizo la udini? Kwani suluhu inatafutwa na mawaziri tu? Kwa nini usiunde tume ikaja na majibu na mapendekezo juu ya mtafaruku huu baina yetu waislamu na wakristu?
Au kwako hili ni dogo tu na kama UPEPO WA SIASA UNAOPITA? Hivi ni nani huwa anakushauri ktk mambo yanayohitaji maamuzi magumu?
Mpendwa rais, unajua kikundi cha Boko haram kilianzaje? Unajua historia ya Alqaida au alshaabab? Punguza presha rais wangu. Kaa chini tulia jipange, tatua huu mzozo mapema.
Kama wasaidizi wako wanakudanganya kuwa tatizo la udini ni dogo hivi sasa na halina madhara basi amini wanaogopa kukuambia ukweli kwa vile wewe mwenyewe ndio mpandaji wa mbegu hii.
mpendwa rais, nakusihi kuwa macho na chuki za udini. Tunaipenda Tanzania, hatutaki tuipoteze.
Unafanya juhudi gani kuondoa udini huu? Na je UTAWEZA?
"wahadha assalam alleykum, wabilah taufiq"
Tafakari!!!!