TIMING
JF-Expert Member
- Apr 12, 2008
- 24,891
- 11,288
Leo nina hamu, tena hamu ni ya chai,
chai isiyo sanda, tena iso na viungo
tena nijibanze kona, wakati najifyonzea
chai iwe ya kweli, niinywe kwa kuivuta
Nina hamu nina hamu, kuliko hata ya jana,
sijui kwanini hamu, ati ije ijumaa
wakati leo wikendi, utamu wake ni bar
chai iwe ya kweli, niinywe kwa kuivuta
wajameni, nina hamu, chai ntapata wapi
hata ya kuinyatia, basi japo kodokolea
nipakate na kikombe, sukari ntaitilia
chai iwe ya kweli, niinywe kwa kuivuta
kikombe nacho napenda, kiwe cha mahanjamu
kwani nikianza kunywa, nisiwe nafunga macho
sikitaki cha mabati, nataka dongo rutuba
chai iwe ya kweli, niinywe kwa kuivuta
chai isiyo sanda, tena iso na viungo
tena nijibanze kona, wakati najifyonzea
chai iwe ya kweli, niinywe kwa kuivuta
Nina hamu nina hamu, kuliko hata ya jana,
sijui kwanini hamu, ati ije ijumaa
wakati leo wikendi, utamu wake ni bar
chai iwe ya kweli, niinywe kwa kuivuta
wajameni, nina hamu, chai ntapata wapi
hata ya kuinyatia, basi japo kodokolea
nipakate na kikombe, sukari ntaitilia
chai iwe ya kweli, niinywe kwa kuivuta
kikombe nacho napenda, kiwe cha mahanjamu
kwani nikianza kunywa, nisiwe nafunga macho
sikitaki cha mabati, nataka dongo rutuba
chai iwe ya kweli, niinywe kwa kuivuta