Wapi nakosea kwenye mapishi ya keki?

Penelope

JF-Expert Member
Aug 23, 2012
713
641
Jameni,siku hizi nimekua nachukua video za you tube najipikilisha keki kwa ajili ya watoto na ili dada wangu wa nyumbani nae ajifunze kupika keki.(inaeza kuja kimsaidia mbeleni) ila wote wanafunzi mimi na yeye kupitia video hizo.

Mimi sio mzoefu sana nimepika mara moja moja na siku za mwanzo kwa kweli ilikua inatoka vizuri kiasi ila inakua na vikasoro kidogo tu..mfano mafuta kama yanakua yanazidi (sijajua hapo ni blueband au vip), inachambuka kiasi sio saaana,,na sijui shida nini lakini inakua ndani sio nyeupe,,inakua kama na brown kwa mbali..

Sasa siku mbili hizi napika keki naona haiivi katikati,,nishajitahidi kurudia tena kama mara mbili sijajua shida nini au nakosea wapi..

Wenye ideas tofauti tofauti ebu mniambie nakosea wapi, nishawaza ni oven au uzito wa keki au nini.
 
Jameni,siku hizi nimekua nachukua video za you tube najipikilisha keki kwa ajili ya watoto na ili
dada wangu wa nyumbani nae ajifunze kupika keki.(inaeza kuja kimsaidia mbeleni).ila wote wanafunzi.mimi na yeye kupitia video hizo.
mimi sio mzoefu sana nimepika mara moja moja na siku za mwanzo kwa kweli ilikua inatoka vizuri kiasi ila inakua na vikasoro kidogo tu..
mfano mafuta kama yanakua yanazidi(sijajua hapo ni blueband au vip),inachambuka kiasi sio saaana,,na sijui shida nini lakini inakua ndani sio nyeupe,,inakua kama na brown kwa mbali..
Sasa siku mbili hizi napika keki naona haivi katikati,,nishajitahidi kurudia tena kama mara mbili sijajua shida nini au nakosea wapi..
wenye ideas tofauti tofauti ebu mniambie nakosea wapi,nishawaza ni oven au uzito wa keki au nini.

Ili uweze Kupika Keki nzuri yakupasa hata akili yako tu nayo iwe Keki / Nzuri. Naomba niishie hapa tafadhali.
 
Unaweka mchanganyiko mzito sana ndio maana ndani haiivi....
Au moto unakua mdogo sana....

Angalia sababu hizo hapo mbili.
au mwepesi sana?ina maana ukieka moto mdogo si ndo itaiva vzr kuanzi ndani
 
Ingia facebook kuna group linaitwa "mapishi rahisi na fasta fasta" angalia kuna kila aina ya mapishi ya cake..me nimejifunza humo na nimeweza..cake lazma iende na VIPIMO

hio ni cake yangu ya pili kuipika.

IMG_20180414_193511.jpeg
 
Ingia facebook kuna group linaitwa "mapishi rahisi na fasta fasta" angalia kuna kila aina ya mapishi ya cake..me nimejifunza humo na nimeweza..cake lazma iende na VIPIMO

hio ni cake yangu ya pili kuipika.

View attachment 750661
inaonekana ni tamu balaa..asante! moto hua unaeka wa kiasi gani..hiyo facebook sikumbuki hata password long time siko huko.instagram au youtube hamna hiyo kitu?
 
Jameni,siku hizi nimekua nachukua video za you tube najipikilisha keki kwa ajili ya watoto na ili
dada wangu wa nyumbani nae ajifunze kupika keki.(inaeza kuja kimsaidia mbeleni).ila wote wanafunzi.mimi na yeye kupitia video hizo.
mimi sio mzoefu sana nimepika mara moja moja na siku za mwanzo kwa kweli ilikua inatoka vizuri kiasi ila inakua na vikasoro kidogo tu..
mfano mafuta kama yanakua yanazidi(sijajua hapo ni blueband au vip),inachambuka kiasi sio saaana,,na sijui shida nini lakini inakua ndani sio nyeupe,,inakua kama na brown kwa mbali..
Sasa siku mbili hizi napika keki naona haivi katikati,,nishajitahidi kurudia tena kama mara mbili sijajua shida nini au nakosea wapi..
wenye ideas tofauti tofauti ebu mniambie nakosea wapi,nishawaza ni oven au uzito wa keki au nini.
Jaribu hii..sukari robo ( tumia nyeupe), siagi robo(prestige), mayai km makubwa eka 5 km size eka 6, unga wa ngano robo(ppf), vanilla au harufu yyte utayoipenda..
Jinsi ya kupika
Changanya hivyo vitu vyote kasoro unga tu..tia kwenye bakuli AF mix mchanganyiko wako na ile mashine...kwa dk tano hv mpaka ile sukar iyeyuke..tia unga ugawe mafungu matatu..unatia kidogo unamix AF unatia tena hivyohivyo! Wakat huo moto wako upo tayari...km ni oven au mkaa!
Ukiona mchanganyiko wako uko tayar na oven limeshapata moto tia baking powder kijiko kimoja flat cha chakula! Unamix fastaaa..unamimina kwenye sufuria unaweka kwenye oven! Hakikisha haufungui fungui! Dk 30hv cake itakuwa tayar...acha ipowe itoe..sorry mwandiko mbaya
 
Jaribu hii..sukari robo ( tumia nyeupe), siagi robo(prestige), mayai km makubwa eka 5 km size eka 6, unga wa ngano robo(ppf), vanilla au harufu yyte utayoipenda..
Jinsi ya kupika
Changanya hivyo vitu vyote kasoro unga tu..tia kwenye bakuli AF mix mchanganyiko wako na ile mashine...kwa dk tano hv mpaka ile sukar iyeyuke..tia unga ugawe mafungu matatu..unatia kidogo unamix AF unatia tena hivyohivyo! Wakat huo moto wako upo tayari...km ni oven au mkaa!
Ukiona mchanganyiko wako uko tayar na oven limeshapata moto tia baking powder kijiko kimoja flat cha chakula! Unamix fastaaa..unamimina kwenye sufuria unaweka kwenye oven! Hakikisha haufungui fungui! Dk 30hv cake itakuwa tayar...acha ipowe itoe..sorry mwandiko mbaya
asante,,hapo kwenye kufungua fungua nafanyaga hivo sana,,lkn sijawahi kupika dk 30 ikaiva yani ni zaidi ya hapo,,
 
Nadhan tatizo ni kipimo cha hamira. Kwa kei ya unga robo tumia kijiko kimoja cha chakula kwa hamira ya baking powder ile ya box la blue
asante,,hapo kwenye kufungua fungua nafanyaga hivo sana,,lkn sijawahi kupika dk 30 ikaiva yani ni zaidi ya hapo,,
 
Weka kimoja kijae mpaka juu,pia wakati wa kuchanganya mchanganyiko wa sukari blue band na unga wa ngano uwe unatumia mkono kuweka kidogo kidogo huku ukichanganya inasaidia keki kuchambuka
 
Itakuwa ni moto, oven ya gas inazingua sana nikipikia ya umeme inatoka vzr
Mimi kuna siku niliangalia kipindi cha cake boss akawa anaelekeza kupika simple cake nyumbani nikajaribu...sina uhakika kama nilipika keki au ugali maana ni kichekesho
 
Back
Top Bottom