Wanajamvi hivi Deus Kibamba na jukwaa la katiba kwa ujumla wameishiwa wapi?sijawasikia kwa muda mrefu sana,au harakati ndio zimefikia ukingoni?
tangu cdm wapate juisi pale magogoni na wao shughuli imekwisha.walikuwa wanatumika na cdm na wale wazungu koko wa scannavia hawawapi mshiko ndomana waona jamaa yupo kimya.
Wanajamvi hivi Deus Kibamba na jukwaa la katiba kwa ujumla wameishiwa wapi?sijawasikia kwa muda mrefu sana,au harakati ndio zimefikia ukingoni?
Ndugu,
Deus yupo na jukwaa lipo. Jukwaa linaendelea kujipanga vizuri, Kwa uhakika zaidi tafadhali tembelea ofisi zao zilizopo Mwenge nyuma ya TRA hasa siku ya Jumapili (22.01.2012) kuanzia saa nne asubuhi kwani watakuwa na mkutano na waandishi wa habari.
Mambo mazuri hayataki haraka, yote yatajulikana hapo. Njoo utoe dukuduku lako!
Deus kweli bado yupo na kama unafuatilia mambo ni kwamba hata jana walikuwa na kikao pale ubungo plaza kujadili mambo haya haya ya katiba na Deus ndiye aliyekuwa anaendesha kikao hicho.
Sio vizuri kuongozwa na hisia. Kama huna uhakika na kitu ni bora kuuliza kuliko mtu kuanza kuweka hitimisho lako!