Webabu
JF-Expert Member
- Apr 29, 2010
- 7,183
- 10,921
Inashangaza sana kuwa binadamu sasa wamekuwa na roho za kinyama sana kwa sababu wanyama ndio ambao mwenzao akiliwa wanakuwa na msaada mdogo sana japokuwa kwa umoja wao wangeamua wangeweza kumuokoa.
Kinachotokea Gaza kinalingana sana na unyama.Kiwango cha vifo vya wapalestina na kujeruhiwa ni kikubwa sana na huenda haijawahi kutokea katika dunia tangu kuumbwa kwake.Kule Hiroshima na Nagasaki wajapani walikufa wengi kwa mpigo lakini kutokana na aina ya silaha iliyotumika hata watu hawakuona mateso yale kiasi kwamba wangelaumiwa kwa kutokutoa msaada kwa wenzao.
Pale Gaza hali ni tofauti sana kwani Israel ni taifa lenye silaha nyingi za kisasa ikipigana na Hamas ambao ni wanamgambo silaha yao kubwa ikiwa ni RPG na makombora yanayoruka hewani kwa mfumo wa kizamani.Silaha nyengine inayowasaidia na kuwasukuma mbele Hamas ni kujua madhila yaliyowakuta wazazi wao na wenyewe ambayo wameona hakuna njia nyengine isipokuwa ni kufa huku wakijitetea badala ya kufa kitandani.
Muhimu tunachokizungumzia hapa ni vile ambavyo Israel inapiga na kuua na kujeruhi wanawake na watoto mpaka wagonjwa na kuvunja majumba yao waliyojenga kwa shida.
Wengine waliobaki hai mwanzoni walitakiwa wahamie kusini,maskini wengi wakatiii amri hiyo,lakini hii ilikuwa kama kuwacheleweshea adhabu zao au kuwapunguzia kwa wakati huo kwani hawakuwachwa huru moja kwa moja kutokana na mashambulizi hayo.
Baada ya muda sasa Israel imekuja kusini na kuwataka hata wale walio katikati nao wazidi kuelekea kusini mpakani na Misri.Maskini wapalestina wa rika zote wametii japo haikuwasaidia chochote kwani makombora yanaendelea kupigwa na kuuliwa kwa idadi kubwa kila siku.
Watu waliokuwa na utajiri na familia zao mara wanajikuta wamebaki wapweke na hata mikoba ya akiba zao imewapotea na wanajikuta omba omba na waokotaji kwenye magofu ili wapate cha kula bila kuchagua ubora.
Katika hali hiyo ya kusongamana kwenye kambi za wakimbizi au kwa ndugu waliobaki na majumba bado wapalesina hao wanatakiwa hapo walipo waende mashariki au magharibi ili itoe nafasi ya kuvurugwa muda mfupi ujao.kwa kisingizio kuwa hapo walipo kuna Hamas.Maskini wote wanatii na kukimbia bila kutaka kufanya mjadala kuwa hawajawaona hao Hamas.Wanafanya hivyo kwa kujua kuwa ikisemwa hivyo kinachofuata ni makombora ya kusambaratisha kila kitu.
Wakipata amri kama hizo ama kwa vipeperushi au namna nyengineyo wapalestina hukimbizana kwa miguu au kwa gari za punda ambazo wachache wamebaki nazo. Hata hivyo wale wanaochelewa kidogo hupatikana viungo vyao tu vilivyotapakaa baada ya kufa kwa mabomu.
Muhimu zaidi tunachotaka kukieleza ni kuwa huo ukatili unaofanyika unafanywa mbele ya macho ya walimwengu wote wa makabila na dini zote. Ukiondoa hisia za kidini basi kiubinadamu tu basi isingepaswa kufanyika mbele ya binadamu wengine.
Kama ni lawama basi tukisema tulaumu hizo lawama zitaanza kwa watu wenye imani moja na wapalestina ambayo ni uislamu na ambayo ni dini karibu ya raia wote wanaoizunguka Palestina na Israel kwa ujumla.Hiyo ndiyo dini ya viongozi wa nchi hizo.
Matendo ya kuuliwa na kuchomewa majumba waislamu wala hayapo na hayajaanza Palestina na Gaza yake pekee.Hayo yamefanyika sana India,Myamar na China.Japo kuna mengi yangeweza kufanyika kuokoa hali zile lalini kule yawezekana ikasemwa ni mbali na hata hayakuwa yakioneshwa wazi wazi.
Haya yanayofanyika Gaza katikati ya ndugu zao na bila kuchukua hatua yoyote ile hakuna namna ya kuyaelezea isipokuwa ni unyama ambao umeingia ndani ya mioyo ya binadamu.
Kuna wenye nyoyo za kinyama ambao wanaweza wakaleta maneno ya kejeli kwa kisingizio kuwa piga Hamas haoo! eti kwa vile walishambulia oktoba 7.Ukiondoa hisia za kinyama na mtuj akabaki na ubindadamu wake basi kwa kuangalia historia hakuna sababu ya kuilaumu Hamas kwa kushambulia na wala haipasi kuwalaumu kwa kutokuwa tayari kusalimu amri.
Lawama kubwa itabaki kwa unyama ulioingia ndani ya nyoyo za binadamu wa karne hizi zinazokariibiana na kiama.Kwa hali hiyo kama litatokea la kutokea kwa unyama wa binadamu basi asilaumu hali ya tabia nchi wala nini isipokuwa abaki kujutia na kulaumu nafisi yake aliyoibadilisha na kuwa ya kinyama.
Kinachotokea Gaza kinalingana sana na unyama.Kiwango cha vifo vya wapalestina na kujeruhiwa ni kikubwa sana na huenda haijawahi kutokea katika dunia tangu kuumbwa kwake.Kule Hiroshima na Nagasaki wajapani walikufa wengi kwa mpigo lakini kutokana na aina ya silaha iliyotumika hata watu hawakuona mateso yale kiasi kwamba wangelaumiwa kwa kutokutoa msaada kwa wenzao.
Pale Gaza hali ni tofauti sana kwani Israel ni taifa lenye silaha nyingi za kisasa ikipigana na Hamas ambao ni wanamgambo silaha yao kubwa ikiwa ni RPG na makombora yanayoruka hewani kwa mfumo wa kizamani.Silaha nyengine inayowasaidia na kuwasukuma mbele Hamas ni kujua madhila yaliyowakuta wazazi wao na wenyewe ambayo wameona hakuna njia nyengine isipokuwa ni kufa huku wakijitetea badala ya kufa kitandani.
Muhimu tunachokizungumzia hapa ni vile ambavyo Israel inapiga na kuua na kujeruhi wanawake na watoto mpaka wagonjwa na kuvunja majumba yao waliyojenga kwa shida.
Wengine waliobaki hai mwanzoni walitakiwa wahamie kusini,maskini wengi wakatiii amri hiyo,lakini hii ilikuwa kama kuwacheleweshea adhabu zao au kuwapunguzia kwa wakati huo kwani hawakuwachwa huru moja kwa moja kutokana na mashambulizi hayo.
Baada ya muda sasa Israel imekuja kusini na kuwataka hata wale walio katikati nao wazidi kuelekea kusini mpakani na Misri.Maskini wapalestina wa rika zote wametii japo haikuwasaidia chochote kwani makombora yanaendelea kupigwa na kuuliwa kwa idadi kubwa kila siku.
Watu waliokuwa na utajiri na familia zao mara wanajikuta wamebaki wapweke na hata mikoba ya akiba zao imewapotea na wanajikuta omba omba na waokotaji kwenye magofu ili wapate cha kula bila kuchagua ubora.
Katika hali hiyo ya kusongamana kwenye kambi za wakimbizi au kwa ndugu waliobaki na majumba bado wapalesina hao wanatakiwa hapo walipo waende mashariki au magharibi ili itoe nafasi ya kuvurugwa muda mfupi ujao.kwa kisingizio kuwa hapo walipo kuna Hamas.Maskini wote wanatii na kukimbia bila kutaka kufanya mjadala kuwa hawajawaona hao Hamas.Wanafanya hivyo kwa kujua kuwa ikisemwa hivyo kinachofuata ni makombora ya kusambaratisha kila kitu.
Wakipata amri kama hizo ama kwa vipeperushi au namna nyengineyo wapalestina hukimbizana kwa miguu au kwa gari za punda ambazo wachache wamebaki nazo. Hata hivyo wale wanaochelewa kidogo hupatikana viungo vyao tu vilivyotapakaa baada ya kufa kwa mabomu.
Muhimu zaidi tunachotaka kukieleza ni kuwa huo ukatili unaofanyika unafanywa mbele ya macho ya walimwengu wote wa makabila na dini zote. Ukiondoa hisia za kidini basi kiubinadamu tu basi isingepaswa kufanyika mbele ya binadamu wengine.
Kama ni lawama basi tukisema tulaumu hizo lawama zitaanza kwa watu wenye imani moja na wapalestina ambayo ni uislamu na ambayo ni dini karibu ya raia wote wanaoizunguka Palestina na Israel kwa ujumla.Hiyo ndiyo dini ya viongozi wa nchi hizo.
Matendo ya kuuliwa na kuchomewa majumba waislamu wala hayapo na hayajaanza Palestina na Gaza yake pekee.Hayo yamefanyika sana India,Myamar na China.Japo kuna mengi yangeweza kufanyika kuokoa hali zile lalini kule yawezekana ikasemwa ni mbali na hata hayakuwa yakioneshwa wazi wazi.
Haya yanayofanyika Gaza katikati ya ndugu zao na bila kuchukua hatua yoyote ile hakuna namna ya kuyaelezea isipokuwa ni unyama ambao umeingia ndani ya mioyo ya binadamu.
Kuna wenye nyoyo za kinyama ambao wanaweza wakaleta maneno ya kejeli kwa kisingizio kuwa piga Hamas haoo! eti kwa vile walishambulia oktoba 7.Ukiondoa hisia za kinyama na mtuj akabaki na ubindadamu wake basi kwa kuangalia historia hakuna sababu ya kuilaumu Hamas kwa kushambulia na wala haipasi kuwalaumu kwa kutokuwa tayari kusalimu amri.
Lawama kubwa itabaki kwa unyama ulioingia ndani ya nyoyo za binadamu wa karne hizi zinazokariibiana na kiama.Kwa hali hiyo kama litatokea la kutokea kwa unyama wa binadamu basi asilaumu hali ya tabia nchi wala nini isipokuwa abaki kujutia na kulaumu nafisi yake aliyoibadilisha na kuwa ya kinyama.