Invisible
Robot
- Feb 11, 2006
- 9,075
- 7,878
Heri mimi sijasema!Kwangu mimi alichokisema Yessir ni obvious na hakukuwa na haja ya dataz. Si kila mtu anaipenda hii forum. Si kila mtu anampenda Mzee Mwanakijiji. Siku ambapo watu wataacha kuisema vibaya hii Forum basi tujue tumepoteza dira! Forum kama hii haiwezi na haitakiwi impendezeshe kila mtu.
Yessir. Tofauti na wanavyosema, Mzee Mwanakijiji si sauti pekee inayosikika humu ndani. Yeye kama wanachama wengine hoja zake na michango yake inajadiliwa kutoka kila upande. Kuna wanaozikubali na kuna wanaozipinga kutegemea na hoja yenyewe. Sijaona dalili za yeye ku-corrupt hii forum. Hilo la ufisadi halistahili jibu maana siku hizi neno hilo limekuwa insult of choice. Kila tusiyekubaliana nae tunamuita fisadi.
Ni hayo, tu. Na karibu jamvini na usije ogopa kuchangia kutokana na reception uliyopata. Mawazo yote na michango yote inathaminiwa bila kujali umejiunga lini.
Amandla......