Wanaume wengine SI Ovyo!

Pdidy

JF-Expert Member
Nov 22, 2007
50,956
22,148
Wanaume wengine Ovyo!

Mwanaume ajulikanaye kwa jina la Bakari akimsaidia mke wake hawa kuosha vyombo baada ya mlo huko Senegal.
Huyu mwanaume si ovyo!Umemfanyia vitu vyote ambavyo mwanaume anastahili kupata wa mke wake hapa duniani.
Umejitahidi kufanya vyote unaweza ili ajue wewe unawajibika kama mke ni yeye tu kusherehekea, hata hivyo matokeo yamekuwa zero!

Sasa swali linakuja
Je, ni kweli kuna wanaume wengine ni ovyo kabisa?
Naamini jibu ni ndiyo, wapo wengi tu iwe mjini au vijijini hali ni sawa.
Je, mwanaume ovyo yupoje?
Mwanaume ovyo ni yule ambaye hataki mabadiliko, na mojawapo ya mifano ya wanaume ovyo ni kama ifuatavyo:-

1. MWANAUME MLEVI (alcoholic)
Ni mwanaume mzuri sana (wonderful) akiwa hajalewa, tatizo ni kwamba si rahisi kumkuta hajalewa.
Anautwika siku nzima, tangu akitokea kazini kwenda nyumbani anakuwa tayari amelewa, anaporudi nyumbani huanza kufungua mlango wa nyumba kwa kelele tangu mita mia kabla ya kuufikia, akifika nyumbani anaanza kuangalia TV na anaenda kulala hapohapo kwenye kiti chake na siku zingine na haja ndogo hapohapo.
Kila siku au muda mwingine ananukia breweries na hii mke hujikuta yupo turned off completely idara zote.

2. MWANAUME ASIYEMWAMINIFU
ndani yake kuna kitu kinamuambia bila mwanamke mwingine yeye si mwanaume tena, hata mke wake ampe zawadi ya mwili kila siku bado akimuona mwanamke mwingine akili zake zinamruka na anachanganyikiwa bila kujali kinachoelea ni dhahabu au maluweluwe.

3. MWANAUME WA PESA, MALI NA MAFANIKIO
Ahadi yake ni kwamba siku tukipata milioni tutaanza kufurahia maisha, baada ya kupata hiyo milioni sasa anasema tukipata milioni 2 ndo tutaanza maisha, baada ya kupata milioni 2 sasa anasema tukipata milioni tatu ndipo tutaanza kufurahia maisha, inaendelea na kuendelea hadi uzeeni.
Ukweli huu ni ugonjwa ila hataki kukubali kwamba ni ugonjwa na kwamba anaumwa.
Eti atacheza na watoto akipata milioni 5, kumbuka watoto hawabaki watoto bali ipi siku wanakuwa watu wazima na kuondoka zao.
Hataki tufurahie tendo la ndoa eti yupo busy kutafuta hizo milioni, hajui miili ikizeeka inaishi kwa medication na hakuna nguvu tena za ku-enjoy sex kama wanandoa.

4. MWANAUME KATARI , JAMII YA AKINA HITLLER
unajua ilivyongumu kuishi na mwanaume mwenye mtazamo kwamba kila kitu unafanya fanya kama ninavyokuelekeza au in my way na anaamini huo ndio ushirikiana wa wanandoa.
Ni kama anajitahidi kufidia yale mama yake alikuwa anamfanyia na ni kweli kwake mwanamke ni kifaa fulani si mtu, si kiumbe sibinadamu.

5. MWANAUME BARIDI
Pole sana, huyu Ukitaka suala la sex amekufa, hana hamu, havutiwi na anaweza kukaa na mke miezi sita bila kufanya mapenzi na akaona ni kawaida.

Anaogopa kuongea na Daktari au mtu yeyote ili kupata msaada wa ushauri.
Anamuonya mke wake hakuna kutaka au kuongelea hili suala mahali popote na mtu yeyote.
Ni kama anamlazimisha mke kuwa na maamuzi ambayo mke hapendi na hakutegemea kama yangempata kwenye ndoa yao.

6. MWANAUME MWENYE WIVU WA KUPINDUKIA
Humuamsha mke wake usiku wa manane ajibu maswali yake ya nani aliongea naye mchana, ilikuwaje akawa ana smile alipokutana na James, nani alikuwa anaongea naye kwenye siku nk.
Mke huchoka kwa visa vya kutiliwa mashaka na kujiona mtumwa au yupo jela ndani ya ndoa yake.
Hii orodha ya wanaume hopeless huendelea hadi 7, 8, 9 hadi 116

Hizi ni ndoa ambazo kama ni daraja basi upande mmoja limevunjika na mmoja amegoma kufanya repair kwa ule upande umeharibika.
Katika ndoa za aina hii kuna mambo mawili yanaweza kutokea nayo ni
(a) Mwanamke huweza kuchukua kile tu anaona anakipata na kuamua kuishi katika uhusiano huu na zaidi mke hujijengea aina ya maisha yake anayayajua ndani ya ndoa aina hii na kuendelea kama vile hakuna matatizo yoyote
(b) Mwanamke huamua kuanza mbele (check out)

Na kama mwanamke ameamua kuchukua uamuzi (b) basi kuna maswali magumu na mazito yanahitaji majibu.
Utafanya nini kuhusiano na kipato,
Je utaondoka kwenda wapi?
Je watoto itakuwaje?
Je, Utakuwa mpweke bila yeye au siku moja hali itabadilika?

Kuna usemi wa kingereza kwamba:-
“Divorce doesn’t help a person prone to excessive anxiety and emotional upset”.

Wapo watu huendelea na safari kutoka kushindwa ndoa moja hadi nyingine au kutoka ya kwanza kwenda ya pili na kushindwa na kuendelea na tatu na kushindwa hadi nne, tano na nk, hadi pale wakibadili tabia na mitazamo yao.

Wanasaikolojia wanaita hii tabia ni symbiotics kwa maana kwamba kawaida tatizo hutafuta tatizo lingine (problems looking for matching problem) na hutokea ndiyo maana mara nyingi mwanamke anayemuacha mwanaume hopeless huenda kumpata mwanaume hopeless mwingine mwenye matatizo mapya kabisa.

Kuna data zinaonesha kwamba kati ya wanandoa 4 ambao hupeana talaka na kuoa tena 4 huishia kuachwa au kuachana tena.

NB:
Kumbuka kuna matumaini kwa mwanaume yeyote ambaye yupo ovyo au hopeless katika ndoa yako.
Hivyo basi ukimwamini Mungu ndoa yako inaweza kurudia katika matumaini mapya bila kujalisha ipo katika hali tete kiasi gani.

Kwani kwa Mungu yote yanawezekana.
(Mathayo 19:26)
 
Wanaume wengine Ovyo!


6. MWANAUME MWENYE WIVU WA KUPINDUKIA
Humuamsha mke wake usiku wa manane ajibu maswali yake ya nani aliongea naye mchana, ilikuwaje akawa ana smile alipokutana na James, nani alikuwa anaongea naye kwenye siku nk.
Mke huchoka kwa visa vya kutiliwa mashaka na kujiona mtumwa au yupo jela ndani ya ndoa yake.


Jamani! Usiombe ukutane na mwanaume kama huyu ......utajuuuuuta KUMFAHAMU!
 
Back
Top Bottom