Wanaume-utu jamani!

charndams

JF-Expert Member
Nov 12, 2010
436
128
Nimekua na rafiki yangu ambaye nilimjua kupitia kwa mpenzi wangu ambaye ni rafiki ya mke wake. Shughuli zote za jikoni, kuosha mtoto, kuandaa mtoto shuleni baba lizima lafanya tena mbele ya shemeji zake huku mke kajistarehesha kutazama televisheni na nduguze. ninajua mapenzi kwa wawili yanaweza kudhihirika kupitia njia mbali mbali lakini kwa haya yake nayatilia shaka kwani yananikumbusha hadithi moja ya mwanamume aliyelishwa chapatti iliyokaliwa ikampumbaza akawa zuzu kila kitu mke akisema anaitika AMINA. Juzi kasimamishwa kazi, mimi kama rafiki pamoja na wenzangu tuliamua kumpa support ya kodi ya nyumba pamoja na ada ya mtoto mpaka atakapo pata kazi. Lakushangaza ni kwamba kati yetu palikua na mmoja ambaye alichukua ile fursa ya shida za yule jamaa na kuanza kurusha ndoano kwa mkewe. Amini na usiamini tabia za yule mama zilibadilika tena vibaya. Mara kaanza biashara ya kusafiri na kulala nje hata wiki. Nilifanya uchunguzi wa kina na nikawafumania siku moja katika hoteli moja ila wao hawakuniona. Nilimweleza mpenzi wangu nae akafanya udadisi wake kubaini ukweli. Yule mama hakumficha alimweleza mpenzi wangu ukweli wa mambo na akamwambia kuwa aliona afanye hivyo maana mumewe hana akili. Alikiri kuwa hiyo haikuwa mara yake ya kwanza ni kitu ambacho amekizoea kwa wanaume tofauti. Kwa kuwa jamaa ni rafiki yangu nashindwa kama nimweleze au ninyamaze. Niwaeleze wale marafiki ambao tuliamua kumpa support yule jamaa au ninyamaze.
Jamani nipo katika njia panda na sitaweza kuyavumilia haya.
 
mmewe hana akili kivp?
hafanyi vyema
ata km tunapenda tusaidiwe vjikaz bt isnt much...dah tena mbele ya wadogo zangu?ahh apana...km tukiwa waili poa bt km kuna wengne madogo ivi mme wangu HATAGUSA ata kijiko

huyo mama hampend jamaa na ashamfanya km haus boy ivi ndo mana anafanya madudu ivi
 
Tafuta njia ya kumsaidia na kumtoa kwenye kifungo cha mkewe.

aongee na mke wa jamaa na kumweleza kwamba anajua
na amwambie anachokifanya isnt gud kwa mungu ata kibnadamu aifai

dah..NA IVI SASA HANA KAZ UYO MAMA NDO ATAZD KUMDHARAU JAMAA
 
aongee na mke wa jamaa na kumweleza kwamba anajuana amwambie anachokifanya isnt gud kwa mungu ata kibnadamu aifaidah..NA IVI SASA HANA KAZ UYO MAMA NDO ATAZD KUMDHARAU JAMAA
Kama kutoka nje ya ndoa imeshakua mazoea kwa hiyo mama basi dharau imejaa gunia tayari!
 
mmewe hana akili kivp?
hafanyi vyema
ata km tunapenda tusaidiwe vjikaz bt isnt much...dah tena mbele ya wadogo zangu?ahh apana...km tukiwa waili poa bt km kuna wengne madogo ivi mme wangu HATAGUSA ata kijiko

huyo mama hampend jamaa na ashamfanya km haus boy ivi ndo mana anafanya madudu ivi

ilifika wakati ambapo yule hawara wa mke anakuja kwa yule bwana kisha anaingia ndani kuongea na mke wakinywa chai huku jibaba liko nje linafua. mpaka hapa nilipo nashindwa jinsi ya kumsaidia manake ukijaribu kumshauri huyoo hadi kwa mkewe na kumweleza kila kitu. hatimaye ugomvi kambini
 
That is a very serious problem. Inabidi yaandaliwe mazingira ya kuongea na huyo bwana ili aelewe kila kitu, hatua kwa hatua. Kushirikiana kazi za ndani kupo ikiwa kama sehemu ya mapenzi, lakini kwa jama kufanya kazi zote na mama akiwa anaanalia TV saa zote, kazi yake kubwa ikiwa ni kushika remote control, that is completely unacceptable! Nadhani amekuwa too humble ndiyo maan hata mkewe anatoka nje ya ndoa atakavyo. Msahuri awe ngangari bwana. Asiwe anazubaa zubaa!
 
Kama kutoka nje ya ndoa imeshakua mazoea kwa hiyo mama basi dharau imejaa gunia tayari!
mke wangu alijaribu kumshauri ila huyo mama akasema achana na baba fulani alalie masikio tu-yeye itakuwa kushika pembe wenzake wanakamua. kiswahili kikafika mfukoni
 
huyo mke wa jamaa inaonekana kabobea na sidhani kama ni rahisi kuacha kwani anamdharau mumewe...sidhani kama ni busara kumuambia jamaa kwani anaweza asikuamini kwa namna anamuamini mkewe.
kaa mbali na mahusiano ya watu mkuu
 
mke wangu alijaribu kumshauri ila huyo mama akasema achana na baba fulani alalie masikio tu-yeye itakuwa kushika pembe wenzake wanakamua. kiswahili kikafika mfukoni

wakat anafanya kaz vp uyo baba ALIKUWA NA PESA KUMZID MKEWE?
ATA KM MKEWE ANAPOKEA LAKI 1 AFU MMEWE ANAPOKEA LAKI 1.5?

jamaa alikuwa anahudumia nyumba fresh?
 
wakat anafanya kaz vp uyo baba ALIKUWA NA PESA KUMZID MKEWE?
ATA KM MKEWE ANAPOKEA LAKI 1 AFU MMEWE ANAPOKEA LAKI 1.5?

jamaa alikuwa anahudumia nyumba fresh?

yes kabisa. imagine yeye mume hakuwa anagusa mshahara wake laki 250000 kwa ajili ya kulea familia. mkewe hakuwa na kazi. mama ndie alikuwa anauchukua. jamaa alikua anasurvive na hela za tuition
 
huyo mke wa jamaa inaonekana kabobea na sidhani kama ni rahisi kuacha kwani anamdharau mumewe...sidhani kama ni busara kumuambia jamaa kwani anaweza asikuamini kwa namna anamuamini mkewe.
kaa mbali na mahusiano ya watu mkuu
ni kweli kabisa boss, hapa ni kuacha wafu wazike wafu wao kwani huyo bwana ameshakua zuzu. cha kushangaza mpaka saa hii zaidi ya miezi 3 hana kazi wala hajishughulishi sisi ndo tunamtafutia kibarua-wonders my broda ohh
 
Back
Top Bottom