Nimekua na rafiki yangu ambaye nilimjua kupitia kwa mpenzi wangu ambaye ni rafiki ya mke wake. Shughuli zote za jikoni, kuosha mtoto, kuandaa mtoto shuleni baba lizima lafanya tena mbele ya shemeji zake huku mke kajistarehesha kutazama televisheni na nduguze. ninajua mapenzi kwa wawili yanaweza kudhihirika kupitia njia mbali mbali lakini kwa haya yake nayatilia shaka kwani yananikumbusha hadithi moja ya mwanamume aliyelishwa chapatti iliyokaliwa ikampumbaza akawa zuzu kila kitu mke akisema anaitika AMINA. Juzi kasimamishwa kazi, mimi kama rafiki pamoja na wenzangu tuliamua kumpa support ya kodi ya nyumba pamoja na ada ya mtoto mpaka atakapo pata kazi. Lakushangaza ni kwamba kati yetu palikua na mmoja ambaye alichukua ile fursa ya shida za yule jamaa na kuanza kurusha ndoano kwa mkewe. Amini na usiamini tabia za yule mama zilibadilika tena vibaya. Mara kaanza biashara ya kusafiri na kulala nje hata wiki. Nilifanya uchunguzi wa kina na nikawafumania siku moja katika hoteli moja ila wao hawakuniona. Nilimweleza mpenzi wangu nae akafanya udadisi wake kubaini ukweli. Yule mama hakumficha alimweleza mpenzi wangu ukweli wa mambo na akamwambia kuwa aliona afanye hivyo maana mumewe hana akili. Alikiri kuwa hiyo haikuwa mara yake ya kwanza ni kitu ambacho amekizoea kwa wanaume tofauti. Kwa kuwa jamaa ni rafiki yangu nashindwa kama nimweleze au ninyamaze. Niwaeleze wale marafiki ambao tuliamua kumpa support yule jamaa au ninyamaze.
Jamani nipo katika njia panda na sitaweza kuyavumilia haya.
Jamani nipo katika njia panda na sitaweza kuyavumilia haya.