Wanasiasa wa Tanzania na PhD za Heshima na Vyeo vya Kijeshi.

Toosweet

JF-Expert Member
May 27, 2012
2,141
1,982
JF Kwenu,

Elimu humpa msomi kujiamini na kumfanya aheshimiwe na jamii. Kwa muda mrefu imekuwa tabia ya wanasiasa wetu kupenda kutajwa vyeo vyao vya kijeshi kabla ya majina yao, Luteni Yusufu Makamba, Kanali Jakaya Kikwete. Hupenda kuitwa hivyo hata kama wameachana na jeshi. Hii tabia naiona hapa Tanzania pekee.

Kagame na Kabila walikuwa majenerali, hawatumii tena vyeo hivyo baada ya kuingia kwenye siasa. Colin Powell, waziri wa zamani wa mambo ya nje wa Marekani alikuwa jenerali wa jeshi. Hakutumia cheo hicho alipoingia kwenye siasa.
Kwa sasa vyeo vya kijeshi vimeanza kuachwa ingawa tuna wanajeshi kwenye nafasi za kisiasa, Meja Jenerali mstaafu Mustafa Kijuu(RC wa Kagera) ingawa bado anavaa gwanda.

Mtindo wa sasa ni kujipa au kupewa udaktari wa falsafa wa heshima(honorary PhD).Pamoja na kupewa kwa heshima, viongozi wa nchi nyingine hawatumii hizi titles. Hubaki kwenye kumbukumbu. Hapa kwetu mtu hufurahi kuitwa 'dakta' ili awakoge watu wakati hajaufanyia kazi. Dk. Jakaya Kikwete, Dr. Reginald Mengi(si mwanasiasa) Kwani kuna ulazima?

Kuna marais na viongozi wengine waandamizi duniani ambao wamesoma kwa viwango vya profesa lakini hawatumii tena titles za kisomi baada ya kuingia kwenye siasa. Hapa kuna Barack Obama, rais wa 44 wa Marekani(katika sheria),kulikuwa na Woodrow Wilson, rais wa 28 wa Marekani, Ricardo Lagos, rais wa zamani wa Chile, Bingu wa Mutharika aliyekuwa rais wa Malawi.

Wako PhD holders wengi pia, nimtaje tu waziri mkuu wa zamani wa Libya aliyekuwa na PhD ya electrical engineering.
Robert Mugabe ndiye rais msomi kuliko wote duniani. Ana shahada saba, mbili kati ya hizo ni masters. Mugabe ana shahada kumi na moja 11,za heshima, tatu zimekuwa revoked. Katika marais kumi wasomi Afrika, wa kwetu hayumo. Rais wa 7 wa Marekani, Andrew Jackson wa 18 Ulysses Grant, wa 28 Dwight Eisenhower ,walikuwa majenerali wa jeshi. Hawakutumia titles za kijeshi waljpokuwa wanasiasa.

Ikiwa kuna wasomi waliopiga shule hawatumii title za elimu au majenerali wa jeshi, kwa nini wale waliopewa kwa heshima wang'ang'anie u-'dakta' au wanasiasa wanajeshi nao wang'ang'anie u-luteni jenerali mstaafu?
Wale tuliojifunza kwao,ukishaingia kwenye siasa, wewe si academician tena, ni politician. Lengo ni kulinda taaluma zisichafuliwe na siasa. Watu wengi wa vijijini wanapata shida rais au waziri mkuu anapoitwa 'daktari'. Siwaonei wivu wasomi wanasiasa.Ni vizuri tujifunze kutoka kwa wengine. Waziri wa zamani wa mambo ya nje wa Ujerumani alipogundulika amekwiba andiko ili kupata PhD, aliachia ngazi.
Tujadili.


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kuhusu kutumia tittle za kijeshi naona ni haki yao sababu hata sheria za kijeshi zinawaruhusu kuendelea kutumia tittle hata baada ya kustaafu maafisa kuanzia cheo cha kapteni kwenda juu.

Mkuu, they've earned those ranks!. Jeshini ranks zinatokana na uwezo wa mtu na ndio maana unaona wengine wamestaafu na vyeo vidogo kama Meja na wengine wamestaafu na vyeo vikubwa hadi luteni jenerali. Kwa hiyo hapo labda ungesema labda hao wa honorary doctorate ndio labda waache hizo tittle kwenye diary ila Kwa maafisa wastaafu wa jeshi a BIG NO please!
 
Kwa kuongezea tu ni kwamba ranks jeshini zina indicate uwezo wa mtu na sio kwamba mtu kutumia tittle baada ya kustaafu ni sifa, hapana. Mfano mbunge marehemu Brigedia jenerali Hassan Ngwilizi; Cheo cha brigedia jenerali anapewa mtu mweledi alieonyesha umahiri tokea akiwa kamanda wa platuni, kamanda wa kombania,kamanda wa kikosi na nafasi nyinginezo ukijumlisha na miaka ya uzoefu na utumishi wa nidhamu ya hali ya juu na kadhalika.
 
Kwa kuongezea tu ni kwamba ranks jeshini zina indicate uwezo wa mtu na sio kwamba mtu kutumia tittle baada ya kustaafu ni sifa, hapana. Mfano mbunge marehemu Brigedia jenerali Hassan Ngwilizi; Cheo cha brigedia jenerali anapewa mtu mweledi alieonyesha umahiri tokea akiwa kamanda wa platuni, kamanda wa kombania,kamanda wa kikosi na nafasi nyinginezo ukijumlisha na miaka ya uzoefu na utumishi wa nidhamu ya hali ya juu na kadhalika.
Hata wabunge wetu usipowaita waheshimiwa na uwakaita kwa marina Yao hawaitikii na huenda wasikusikilize chochote. Watanzania tunapenda kujikweza sana.
 
Bw. Einstein alisema "in politics stupidity is not a handicap." Hata ukiwa na cheti feki unapwaga tu
 
Kuhusu kutumia tittle za kijeshi naona ni haki yao sababu hata sheria za kijeshi zinawaruhusu kuendelea kutumia tittle hata baada ya kustaafu maafisa kuanzia cheo cha kapteni kwenda juu.

Mkuu, they've earned those ranks!. Jeshini ranks zinatokana na uwezo wa mtu na ndio maana unaona wengine wamestaafu na vyeo vidogo kama Meja na wengine wamestaafu na vyeo vikubwa hadi luteni jenerali. Kwa hiyo hapo labda ungesema labda hao wa honorary doctorate ndio labda waache hizo tittle kwenye diary ila Kwa maafisa wastaafu wa jeshi a BIG NO please!
I respect your challenge, it is authentic in a way. Shida ni kuwa ukishaingia kwenye siasa unafanya mambo kinyume na taaluma yako/nidhamu ya jeshi. Lengo ni kulinda taaluma, kuzitenga na kashfa za kisiasa.

Mawaziri wakuu wa Israel, Ariel Sharon, Ehud Barack na Benjamin
Netanyahu walikuwa makommando, special forces inayoitwa kwa Kiyahudi Sayeret Matkal. Ariel Sharon akiwa kiongozi wa hao vijana(sasa watu wazima).Usipoambiwa walikuwa makomando ,huwezi kujua. Hakuna mahali wamelalamika kutotambuliwa fani zao.
Wenzetu wameshaacha kitambo kutaja vyeo vya jeshi. Tumebaki sisi.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
JF Kwenu,

Elimu humpa msomi kujiamini na kumfanya aheshimiwe na jamii. Kwa muda mrefu imekuwa tabia ya wanasiasa wetu kupenda kutajwa vyeo vyao vya kijeshi kabla ya majina yao, Luteni Yusufu Makamba, Kanali Jakaya Kikwete. Hupenda kuitwa hivyo hata kama wameachana na jeshi. Hii tabia naiona hapa Tanzania pekee.

Kagame na Kabila walikuwa majenerali, hawatumii tena vyeo hivyo baada ya kuingia kwenye siasa. Colin Powell, waziri wa zamani wa mambo ya nje wa Marekani alikuwa jenerali wa jeshi. Hakutumia cheo hicho alipoingia kwenye siasa.
Kwa sasa vyeo vya kijeshi vimeanza kuachwa ingawa tuna wanajeshi kwenye nafasi za kisiasa, Meja Jenerali mstaafu Mustafa Kijuu(RC wa Kagera) ingawa bado anavaa gwanda.

Mtindo wa sasa ni kujipa au kupewa udaktari wa falsafa wa heshima(honorary PhD).Pamoja na kupewa kwa heshima, viongozi wa nchi nyingine hawatumii hizi titles. Hubaki kwenye kumbukumbu. Hapa kwetu mtu hufurahi kuitwa 'dakta' ili awakoge watu wakati hajaufanyia kazi. Dk. Jakaya Kikwete, Dr. Reginald Mengi(si mwanasiasa) Kwani kuna ulazima?

Kuna marais na viongozi wengine waandamizi duniani ambao wamesoma kwa viwango vya profesa lakini hawatumii tena titles za kisomi baada ya kuingia kwenye siasa. Hapa kuna Barack Obama, rais wa 44 wa Marekani(katika sheria),kulikuwa na Woodrow Wilson, rais wa 28 wa Marekani, Ricardo Lagos, rais wa zamani wa Chile, Bingu wa Mutharika aliyekuwa rais wa Malawi.

Wako PhD holders wengi pia, nimtaje tu waziri mkuu wa zamani wa Libya aliyekuwa na PhD ya electrical engineering.
Robert Mugabe ndiye rais msomi kuliko wote duniani. Ana shahada saba, mbili kati ya hizo ni masters. Mugabe ana shahada kumi na moja 11,za heshima, tatu zimekuwa revoked. Katika marais kumi wasomi Afrika, wa kwetu hayumo. Rais wa 7 wa Marekani, Andrew Jackson wa 18 Ulysses Grant, wa 28 Dwight Eisenhower ,walikuwa majenerali wa jeshi. Hawakutumia titles za kijeshi waljpokuwa wanasiasa.

Ikiwa kuna wasomi waliopiga shule hawatumii title za elimu au majenerali wa jeshi, kwa nini wale waliopewa kwa heshima wang'ang'anie u-'dakta' au wanasiasa wanajeshi nao wang'ang'anie u-luteni jenerali mstaafu?
Wale tuliojifunza kwao,ukishaingia kwenye siasa, wewe si academician tena, ni politician. Lengo ni kulinda taaluma zisichafuliwe na siasa. Watu wengi wa vijijini wanapata shida rais au waziri mkuu anapoitwa 'daktari'. Siwaonei wivu wasomi wanasiasa.Ni vizuri tujifunze kutoka kwa wengine. Waziri wa zamani wa mambo ya nje wa Ujerumani alipogundulika amekwiba andiko ili kupata PhD, aliachia ngazi.
Tujadili.


Sent using Jamii Forums mobile app
Wabongo wanapenda sifa sana,hata kwenye makaburi yao huweka hizo title zao ndio majina yao yafuate.
Ushamba plus ulimbukeni!

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ni Ushamba tu mkuu, Mimi sipendi ata Kujitambulusha ni nani sehemu ambapo hapana umuhimu wajue tittle yako, Nimekaa na Wazungu jamaa ni Wasiri balaa unaweza inshi na mzungu life la kawaida kabisa mwisho wa siku akikuonesha ganda zake unakuta ana masters
 
Back
Top Bottom