Wanasheria wetu wametuonesha huko Mbeya jinsi walivyo na weledi mkubwa wa kushawishi na kuvuruga. Tatizo tunatumia vilaza kututengenezea mikataba

Dr Akili

JF-Expert Member
Aug 21, 2011
4,953
4,326
Tumejifunza mengi kutoka kwenye munyukano wa kisheria uliotokea kwenye Mahakama Kuu ya Mbeya kuhusiana na mkataba kati ya DP World na Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Tulichoshuhudia ni tofauti kabisa na kile ambacho baadhi yetu walikuwa wametuaminisha kwamba wanasheria wetu ni vilaza watupu na ndiyo sababu ya kuwa na mikataba mibovu na kushindwa kesi za kimataifa huko ICSID na kwingineko.

Tumeshuhudia jinsi wanasheria mawakili wa pande zote mbili walivyo na weledi mkubwa wa ku convince na ku confuse in a professional manner katika kuchambua sheria. Tumejifunza kuwa Katiba yetu ya nchi imempa Rais sovereign (aka supreme) power ya kufanya chochote ikimpendeza. Sovereign powers hizo wananchi humkabidhi kwenye uchaguzi mkuu.

Tumejifunza kwamba hicho wanasiasa wanachokiita kuuzwa kwa bandari zetu si kuuzwa in the literal meaning bali ni kuwapa hawa DPW sovereign powers ya bandari zetu zote. Tumepoteza sovereign powers zetu kwenye bandari zote na special economic zones.

Tumejifunza kuwa wabunge ndiyo wawakilishi halali wa wananchi. Na bunge huendeshwa kwa kanuni iliyojiwekea. Hao wadau si wawakilishi rasmi wa wanainchi, kuhusishwa kwao ni kwa kanuni tu za bunge, idadi yao na muda wa notisi ni kwa mapenzi ya Spika.

Kila fani (profession) vilaza huwaga hawakosekani. Kuna madaktari vilaza, waalimu vilaza, wahandisi vilaza, wanahabari vilaza, wanasiasa vilaza na kadhalika. Wahenga walishasema kwamba kwenye kundi la mamba, kenge huwa hawakosekani.

Tatizo letu huwa tunatafuta wale wanasheria vilaza aka kenge kututengenezea mikataba yetu, hivyo kuwa na mikataba mingi mibovu inayotusababishia kushindwa kesi huko ICSID.

Tatizo letu huwa mara nyingi tunachagua wanasiasa vilaza kuwa wabunge wetu na hivyo kusababisha mikataba mibovu ilidhiwe faster faster na kadhalika. Ila ikumbukwe rushwa ina uwezo wa kumfanya mtu ye yote mwelevu akaonekana kilaza wa kutupa. Money is the source of all evils and not the devil!
 
Huwa naamin hiv "watu wenye akili nyingi na uwezo mkubwa sana ,mara nyingi huwa nje kabisa ya circle, wanao stahili wako nje wasio stahili wako ndani".
Sijui nin huwa kinasababisha.Nadhan moja wapo ya sababu ni mbinu ya kuvipata hiv vichwa.

Unaenda kwwnye interview umemaliza miaka mi 3 au 4 iliopita, unakutana na watoto waliomaliza miezi kadhaa iliopita af wote mnapewa mtihani wa darasani 😂😂😂
 
Hili suala la DPW nikilitazama vizuri, limaonesha jinsi hii nchi ilivyooza kimuundo na kimfumo.

Samia anakabidhi mamlaka kwa mwarabu baada ya kuhongwa ufadhili wa Royal Tour, hajui kwa kufanya hivyo anamega sehemu ya ufalme wake na kumkabidhi mtawala wa Dubai.

Hata kama Katiba yetu imempa mamlaka makubwa, lakini anapoamua kugawa sehemu ya mamlaka hayo kwa wageni, anaonesha vile hafai na hatoshi kukali kiti.
 
Huwa naamin hiv "watu wenye akili nyingi na uwezo mkubwa sana ,mara nyingi huwa nje kabisa ya circle, wanao stahili wako nje wasio stahili wako ndani".
Sijui nin huwa kinasababisha.Nadhan moja wapo ya sababu ni mbinu ya kuvipata hiv vichwa.

Unaenda kwwnye interview umemaliza miaka mi 3 au 4 iliopita, unakutana na watoto waliomaliza miezi kadhaa iliopita af wote mnapewa mtihani wa darasani 😂😂😂
Siku zote Mungu hamnyimi mwanadamu vyote. Vilaza wamebarikiwa uwezo wa kujiamini sana ukilinganisha na wale wenye akili nyingi (werevu).

Na kutokana na kujiamini kwao, mwisho wa siku wanajikuta wanawaongoza/wanawatawala vilaza wenzao wengi, pamoja na wale wenye akili wachache.

Na wenye akili kutokana na kukosa/kunyimwa kipaji cha ujasiri, wanajikuta wanalalamikia tu pembeni pale viongozi vilaza wanapo vurunda.
 
Siku zote Mungu hamnyimi mwanadamu vyote. Vilaza wamebarikiwa uwezo wa kujiamini sana ukilinganisha na wale wenye akili nyingi.

Na kutokana na kujiamini kwao, mwisho wa siku wanajikuta wanawaongoza/wanawatawala vilaza wenzao wengi, pamoja na wale wenye akili wachache. Na wenye akili kutokana na kukosa ujasiri, wanajikuta wanalalamikia pembeni pale viongozi vilaza wanapo vurunda.
Inawwzekana.
UKiangalia Msukuma anavyojiamin mjinga yule, wakisimamishwa na Charles Kimei pale bungeni unaweza sema Msukuma ndio the brain 😂😂
 
Conflict of Interests Issue wala sio ukilaza.
Unamaanisha corruption au mlungula?


Mawakili Smart hawaajiliwi serikalini
Mbona ili graduate wa sheria aweze kuajiriwa kama wakili wa serikali (State Attorney) ni lazima ahudhurie mafunzo ya si chini ya mwaka mmoja pale Law School. Muziki wa pale Law School kila mmoja anaujua. Wadahiliwa huwa ni mia moja tu kwa mwaka na wanaofaulu pale huwa hawazidi asilimia 30%. Yaani wanaotoka pale ni majembe (brains) kweli kweli lakini hatuwatumii kututengenezea mikataba yetu.

Mbona ili graduate wa medicine ?MD) ili aweze kusajiliwa kufanya internship year ni lazima afanye na kufaulu vizuri mtihani wa Baraza la Taifa la Madaktari (MCT). Mtihani huo huwa si wa mchezo na ni asilimia 30% tu graduates ndiyo huwa wanaushinda. Majembe yanayoshinda ndiyo huajiriwa serikalini, wale vilaza huishia mitaani kwenye private hospitals.

Fani ya ualimu nayo iko mbioni kufanya hivyo ili kuepukana na vilaza kwenye shule zetu za serikali wanaoharibu ubora wa elimu kwa vijana wetu.

Inawwzekana.
UKiangalia Msukuma anavyojiamin mjinga yule, wakisimamishwa na Charles Kimei pale bungeni unaweza sema Msukuma ndio the brain 😂😂
Hili ndilo tatizo kuu la watanzania walio wengi. Wanapenda sana kuchagua aina ya akina Msukuma au Bajaji kuwa wawakilishi wao bungeni. Wanaamini siasa ni comedy na hivyo huchagua comedians kwenda bungeni. Bunge letu limekuwa bunge la comedy! Ni ngumu sana majembe ya aina ya Mpina au Mdee kuchaguliwa ubunge. Hivyo tuna kazi nzito ya kuelimisha watanzania wafahamu aina ya wanasiasa wanaofaa kuchaguliwa kuwa wabunge wao. Wachague majembe badala ya vilaza. Badala ya kuelimisha watanzania masuala ya DP World na Haki jinai, serikali ingejikita zaidi kwenye elimu hii ya kuchagua wabunge na madiwani majembe.
 
Inaonekana sio vilaza kama mtoa mada anavyotaka tuamini.

Jambo moja la kweli ambalo tutakubaliana kwa pamoja ni kuwa

Mawakili Smart hawaajiliwi serikalini...
Tell us, wewe ungekuwa mwanasheria umeajiliwa serikalini.... how should you deny rectifying contract brought before you by your superior?
Je, wewe ungeweza kuchagua kuacha kazi na hata hisiwe sababu ya kuzuia kataba husika kusainiwa?
 
Huwa naamin hiv "watu wenye akili nyingi na uwezo mkubwa sana ,mara nyingi huwa nje kabisa ya circle, wanao stahili wako nje wasio stahili wako ndani".
Sijui nin huwa kinasababisha.Nadhan moja wapo ya sababu ni mbinu ya kuvipata hiv vichwa.

Unaenda kwwnye interview umemaliza miaka mi 3 au 4 iliopita, unakutana na watoto waliomaliza miezi kadhaa iliopita af wote mnapewa mtihani wa darasani
Samahani kwa swali hili; kama unaamini katika histori je, wale watumwa waliouzwa na waafrika wenzao unadhani ni wale waliokuwa dhaifu au hodari na wenye akili sana kuliko watawala wa wakati ule?
 
Back
Top Bottom